Mwenye kupinga 'kauli ya Pinda', huyo ni adui wa nchi.

Wana-JF!

Ingawa kumekuwa na upotoshaji wa aina yake humu jamvini na kwengineko, kuhusu kauli ya mhe. Pinda, ila ukweli utabaki palepale kuwa mhe. Pinda ametoa kauli sahihi kwa wakati sahihi.

Kauli ya mhe. Pinda imepewa tafsiri ya uongo, kuwa imevunja katiba, hali iliyo pelekea wengi wenu kustaajabu kuwa ina kuwaje mwanasheria mkongwe kama mhe. Pinda kufanya hivyo, ila ukweli wa kauli yake mhe. Pinda ni huu hapa;

Mhe. Pinda alivyosema polisi wapige tu, hakuwa ana maanisha kuwa polisi wapige tu raia hovyo hovyo, lah hasha, bali alimaanisha polisi wadhibiti kwa maana ya kuwapiga raia wenye kukaidi maagizo ya dola.

Wote humu jamvini tunajua ni wajibu wa polisi kulinda raia na mali zao, lakini kwa vurugu za hivi karibuni, usalama wa raia umekuwa hatarini, kutokana na fujo za vyama vya siasa, kwa hali kama hiyo, serikali ni lazima ingetoa kauli, kauli yenyewe ndio hiyo ya mhe. Pinda.

Kauli ya mhe. Pinda imekuwa faraja kwa wapenda amani na utulivu wa hapa nchini, lakini imekuwa ni mwiba kwa wapenda fujo na maandamano yasiyo na tija yoyote kwa taifa.

Mhe. Pinda asante, TAIFA LIPO SALAMA SASA.

sina uhakik kama unafahamu ulichoandika. Hakuna mtu anaruhusiwa kumpiga au kumtesa au kutoa adhabu yoyote yenye kudhalilisha. tena katiba imesrma wazi kwa kutumia nen
o maarufuku. police wanatumia nguvu pisipo na uazima. wanapaswa tumia silaha kwa mtu mwenye siaha n au kipigo kwa mtu anartumia nguvu ili wamkamate. nyie mshanfilieni tu huyu mzee lakini mtaona mwisho wake.
 
Katika watu wasiofikiria jambo na kukurupuka kuandika ni huyu jamaa mleta thread. Ni mweupe sana kichwani.
 
Watanzania tulio wengi tunaunga mkono kauli ya pinda. Hutaki unaacha
 
Katika watu wasiofikiria jambo na kukurupuka kuandika ni huyu jamaa mleta thread. Ni mweupe sana kichwani.
 
Katika watu wasiofikiria jambo na kukurupuka kuandika ni huyu jamaa mleta thread. Ni mweuoe sana kichwani.

ww ni mweusi kichwani ndio humwelewi mleta mada, he is very smart and critical. Tumechoshwa na matukio ya umwagaji damu na mauaji
 
Katika watu wasiofikiria jambo na kukurupuka kuandika ni huyu jamaa mleta thread. Ni mweupe sana kichwani.

unatujazia saver na page kwa ujinga wako huu, delete huko bana. Ww ndio unaeua watu ndio mana umechukizwa na kauli ya pinda
 
Hivi huwa unalala saa ngapi? maana unaishi Tanzania na unaanzisha thread saa kumi usiku!! this is more than interesting.

Anyway ndio fursa zenyewe hizo, buku saba per day si haba, zidisha juhudi.
 
unatujazia saver na page kwa ujinga wako huu, delete huko bana. Ww ndio unaeua watu ndio mana umechukizwa na kauli ya pinda

Wewe ni mpumbavu sana. Hiyo saver ninayojaza ni ya kwako? Shenzi type eti mimi ndo naua watu. Yani humu ndani kuna vilaza mpaka basi
 
Wana-JF!

Ingawa kumekuwa na upotoshaji wa aina yake humu jamvini na kwengineko, kuhusu kauli ya mhe. Pinda, ila ukweli utabaki palepale kuwa mhe. Pinda ametoa kauli sahihi kwa wakati sahihi.

Kauli ya mhe. Pinda imepewa tafsiri ya uongo, kuwa imevunja katiba, hali iliyo pelekea wengi wenu kustaajabu kuwa ina kuwaje mwanasheria mkongwe kama mhe. Pinda kufanya hivyo, ila ukweli wa kauli yake mhe. Pinda ni huu hapa;

Mhe. Pinda alivyosema polisi wapige tu, hakuwa ana maanisha kuwa polisi wapige tu raia hovyo hovyo, lah hasha, bali alimaanisha polisi wadhibiti kwa maana ya kuwapiga raia wenye kukaidi maagizo ya dola.

Wote humu jamvini tunajua ni wajibu wa polisi kulinda raia na mali zao, lakini kwa vurugu za hivi karibuni, usalama wa raia umekuwa hatarini, kutokana na fujo za vyama vya siasa, kwa hali kama hiyo, serikali ni lazima ingetoa kauli, kauli yenyewe ndio hiyo ya mhe. Pinda.

Kauli ya mhe. Pinda imekuwa faraja kwa wapenda amani na utulivu wa hapa nchini, lakini imekuwa ni mwiba kwa wapenda fujo na maandamano yasiyo na tija yoyote kwa taifa.

Mhe. Pinda asante, TAIFA LIPO SALAMA SASA.

WAPIGWE TU;Hata kama ni risasi ya kichwa wapigwe tu ya kiuno wapigwe tu ya mgongo wapigwe tu kama yatakufa yatajijuwa yenyewe.Eti ninyi ndiyo siyo maadui wa nchi na ni wapenda amani munaofarijika na vitendo hivyo.
 
Hakuna maneno yoyote yanayoweza kuhalalisha kauli ya Pinda, hata yapambwe kiasi gani.

Mzee huyu amelewa madaraka, mnaomtetea Pinda mnajua ni kwa kiasi gani ameumiza mioyo ya waathirika wa vipigo, mabomu na hata risasi za polisi? Waliouwawa? waliotiwa vilema? yatima? wagane? wajane? Pinda is the most bogus PM tangu 1961.

Kauli ya Pinda bado si halali na haina uhalali katika mazingira yoyote yale, mbaya zaidi ameitoa in a formal way.
 
Wana-JF!

Ingawa kumekuwa na upotoshaji wa aina yake humu jamvini na kwengineko, kuhusu kauli ya mhe. Pinda, ila ukweli utabaki palepale kuwa mhe. Pinda ametoa kauli sahihi kwa wakati sahihi.

Kauli ya mhe. Pinda imepewa tafsiri ya uongo, kuwa imevunja katiba, hali iliyo pelekea wengi wenu kustaajabu kuwa ina kuwaje mwanasheria mkongwe kama mhe. Pinda kufanya hivyo, ila ukweli wa kauli yake mhe. Pinda ni huu hapa;

Mhe. Pinda alivyosema polisi wapige tu, hakuwa ana maanisha kuwa polisi wapige tu raia hovyo hovyo, lah hasha, bali alimaanisha polisi wadhibiti kwa maana ya kuwapiga raia wenye kukaidi maagizo ya dola.

Wote humu jamvini tunajua ni wajibu wa polisi kulinda raia na mali zao, lakini kwa vurugu za hivi karibuni, usalama wa raia umekuwa hatarini, kutokana na fujo za vyama vya siasa, kwa hali kama hiyo, serikali ni lazima ingetoa kauli, kauli yenyewe ndio hiyo ya mhe. Pinda.

Kauli ya mhe. Pinda imekuwa faraja kwa wapenda amani na utulivu wa hapa nchini, lakini imekuwa ni mwiba kwa wapenda fujo na maandamano yasiyo na tija yoyote kwa taifa.

Mhe. Pinda asante, TAIFA LIPO SALAMA SASA.

Umelipwa bei gani kwa utumbo huu??
Kama kweli kazi ya polisi ni kulinda amani, yule mtoto aliyetoka TUITION alikuwa wa chama gani?
Ni polisi wa aina gani anayelinda amani kwa kuua raia wasiyokuwa na bunduki?
Hii kauli ya "Mhe. Pinda alivyosema polisi wapige tu", wewe uliwahi kufuga mbwa halafu ukamwambie kamata na huyo mbwa asikutii kwa kuuma huyo aliye mmwambia amkamate???
Fikiri kwanza kabla hujatoa tamko ambalo kesho litaruhusu kila mmoja kutafsiri kwa uelewa wake. Kauli ya Mh. Pinda ni mbaya na inaruhusu polisi kuua raia kinyume na kazi ya kulinda raia na mali zao.
 
aboubakr.jpg


Mtoto: polisi walinipiga risasi

...Halafu huyu HAMY-D anaunga mkono kauli ya kikatili kama ya Hitler!
 
Last edited by a moderator:
Na kulialia kama toto jinga vile! Oh! Nimenukuliwa vibaya! Anaulilia Uwaziri Mkuu. Sasa mwisho wako umefika. Subiri Tundu Lissu arudi huko Bungeni

Sikutarajia kama Lissu nae angetii maamuzi ya Mbowe, mtu ambae amemzidi kila kitu.

Sasa kisa tu Mwenyekiti wake ndio aheshimu maamuzi yake ya kipuuzi?
 
katiba hairuhusu kupiga na ndio maana polis wanasema tukimshika muharifu tusimpige bali tumpeleke polis

Wewe wa wapi?

Ni kweli ilipaswa iwe hivyo! lakini kwa fujo za raia hapa nchini hiyo sheria haiwezi kutekelezwa, watu wanakuja na mawe na magongo una tarajia polisi wafanyaje?
 
HAMY-D

na hiyo uliyoitowa wewe ni tafsiri yako binafsi ya maneno ya Mhe Pinda hapa tunaanza kukuona wewe kama vile msemaji wa Mhe Pinda usiyekuwa official au wewe una Phd ya kumuelwa Pinda zaidi?

Ikiwa wewe umemfasiri hivo ujuwe na wengine wanauwezo wa kumfasiri vyengine na wakiwemo hao polisi.

Mkuu si unajuwa kwamba Pinda na yeye ni mswahili na anajuwa maana na tofauti baina ya maneno PIGA na DHIBITI,

sasa nikuomba uwache kumtilia maneno mdomoni mwake, kinachotoka mdomoni mwa mtu huanzia moyoni kwake kwahivo alichokisema ndio alichokikusidia.

Mhe Pinda ikiwa kama kiongozi wa dola anajuwa wazi kwamba anapashwa kutoa kauli ambazo hazina utata, lazima awe anatowa kauli ambazo hata mtoto mdogo afahamu anachokizungumia na makusidio yake.

Ni kweli ni tafsiri yangu, ila ndio tafsiri halisi ya kauli ya mhe. Pinda.

Nimeona ni vyema nitanue wigo wenu wa kufikiri, maana wengi wenu mmejifunga kuwa mhe Pinda alikuwa na lengo baya kwa kusema vile, ila hapana, yule ni kiongozi, ni mlezi wa wananchi kwa nafasi yake ya PM, kwa mantiki hii, hawezi kuwa na dira ya kuumiza raia wake.
 
Hiroshima,

ukichunguza kiundani utaona hivi

CCM ndio imo hivo katika kujiandaa na uchaguzi wa 2015, si unajuwa kutakuwa na kasheshe kubwa uchaguzi ujao na Mhe Pinda anayo good chance ya kuwa mgombea kwa tiketi ya CCM. tanganyika munaweza kumwaga damu nyingi sana kama muhanga wa kiti cha urais

Kwanza si kweli kama Pinda atagombea, lakini vilevile sio mpango wa CCM kutumia mabavu kwenye uchaguzi 2015.
 
Kama Mawaziri wakuu wa Uturuki,Brazil,Ufaransa,Kenya na Marekani wangekuwa na kauli kama za Pinda, nchi zao zingekuwa zimejaa makaburi mpaka barabarani. Polisi wapo kwa ajili ya wananchi lakini wananchi hawapo kwa maslahi ya polisi.Raia hawatakiwi kuwa watumwa wa jeshi la polisi lakini jeshi la polisi ni 'watumwa halali' wa wananchi na wanakula,wanavaa,wanalala,wanasoma,wanasafiri na kutibiwa kupitia kodi za wananchi. Je, jeshi la polisi Miungu watu Tanzania? Je, hawatii amri za wakuu wa wilaya na mikoa? Je,wakuu wa wilaya na mikoa ni wawakilishi wa wananchi au Rais? Je, siyo wajumbe wa kamati za siasa ya chama cha mapinduzi? Je, wananchi wenye akili timamu watii kila amri hata kama haina maslahi kwao ila kwa polisi waliotumwa na watawala? Kama ndivyo, kwanini katika mazingira ya upinzani pekee?
 
Watu wote wangekua wana akili kama yako na Pinda, amani na utulivu tulionao leo nchini usingekuwepo. Hivi ni sheria gani inayoruhusu raia kupigwa kwa kosa la kuandamana au kufanya mkusanyiko usio halali? Sheria za nchi zipo wazi kuwa anaefanya kosa flani atapata adhabu fulani, sidhani kama sheria inasema kabla ya kupelekwa mahakamani mtu apigwe na polisi.

Nje ya hilo, sidhani kama Pinda na wanaomtetea kama wamelitafakari kwa makini hilo manake ukiangalia matukio ya Arusha na Mtwara, utagundua asilimia kubwa ya waliopigwa au kuuliwa ni wale wasiokua na hatia. Je, kwa kauli ya Pinda na wanaomtetea, inamaanisha watu wasio na hatia waendelee kupigwa na kuuliwa? Je, katika kundi la watu barabarani, polisi watawatambuaje wenye kosa na wasio na kosa? Kwa mtazamo wangu ni kwamba Pinda alipitiwa na wanaomtetea wamepungukiwa maono.
 
sasa hapa ndio umesema nini? kuna tofauti gani kati ya unachosema wewe na alichosema Pinda na kile ambacho watu wametafsiri? Halafu hiyo maana wewe umejuaje?

Mzee Mwanakijiji,

Heshima kwako,

Ambacho nimejaribu kusisitiza hapo ni kwamba, watu wanaostaili kupewa kipigo na polisi sio tu raia yeyote, bali ni wale tu wanaokaidi maagizo ya vyombo vya dola, tena wengine wana kaidi na mpaka kujaribu kupambana na polisi, sasa hali hii ikilelewa una tarajia nini hapo baadae?

Lakini watu wengi humu tafsiri yenu kwenye kauli ya Pinda ni kama vile mhe. Pinda amehalalisha polisi wapige tu raia.

Nchi inaendeshwa kwa misingi ya sheria, na kama ikifuatwa, hakuna haja ya hayo maandamano, sasa ifike wakati tutafute njia za kistaarabu na zinazo kubalika.

Njia hizo zisiwe zile za wewe upate, wenzako waumie, au wafe, mali za wenzako ziharibe na athari zinginezo kwa wenzako.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom