Mwendo kasi usafiri wa kishamba

Mwendo kasi usafiri wa kishamba

kagombe

JF-Expert Member
Joined
Mar 1, 2015
Posts
3,624
Reaction score
1,827
Mabasi yamepaki abiria wanaangaika usafiri.
Huu ni ushamba waendeshaji wanasababisha usumbufu na kero kubwa.

Badilikeni mtu amekata tiketi anakaa kituoni dakika 30.
Ushamba au dharau
 
Hujajuliza juu ya watu kupanda na kushuka kwenye vituo vya kabla wakiwa wengi nayo ni sababu kubwa!?
 
Nimesota hapo gerezani muda sio mrefu,huduma ni mbovu hakuna uwiano wanavyonadi na huduma inayotolewa
 
Wa kijanja ndo UPI kwani?

Kwani wee kabla ya hapo ulikua unatumia usafiri gani?

Rudi uko uko kwny UDA na vidaladala uone thamani ya kutoka nusu Saa kituoni
 
Mimi nadhani hawakufanya utafiti wa kutosha. Kama wanajua kuna tatizo wangekuwa wanatoa taarifa mapema na kuruhusu daladala zinafanya rout ili kuondoa tatizo la usafiri. Kinachokera ni kwamba mabasi yao hayafanyi kazi bado zile daladala tulizozoea zinazuiwa kupakia abilia!
 
Rudi kwny daladala za kawaida

Kituoni fasta ushapanda gari, barabarani utakaa masaa matatu ubungo - mbezii
 
kuna mijitu imeingia juzi mjini humu.
before " mwendo haraka" watu walikaa masaa 3 kituoni na wwkiingia wanapitia dirishani!
 
Sijawahi kuona usafiri wenye kero kama mwendo kasi nimekata tiketi ya kwenda gereza nakaa kituoni zaidi ya lisaa mpk nimejuta kwann nimekata alafu gari inafika tunagombania tena aagrrrrr [emoji35][emoji35]
 
Wale madereva kuna tatizo..

Kama hakuna wasimamizi kila kituo wataua biashara..

Ikifika mchana wakifika mfano pale kivukoni au morocco (ambapo ndio natumia sana) wanaegesha magari kama hawafanyi kazi vile... Wanangoja mpaka abiria wawe Mara mbili ya uwezo Wa gari ndio wanaleta gari.moja... Huu ni ushamba.. Aliyetufundisha kuwa lazima daladala ijae mpaka wasimame ni mshamba pia...

Hii imepelekea watu turudi.kwenye mafoleni tu.. Maana haina maana.. Unapendeza uende kazini/kwenye kikao unashuka hueleweki umetafunwa na mbuzi au Nn! Mnasimama mpaka watu wanapumuliana ?! Hapa wabadilike.. Wao ndio mfano kuwa pioneer sometimes lazima ukubali hasara .. Kuna mabasi miaka Fulani yalikuwa yanaenda hata na abiria 3arusha kwakuwa walikuwa wanajenga reputation and it worked sasa hivi arusha hamsafiri na kuku na bata ndani... Mnaaka kwenye Viti wote ...sio kama kwenda Handeni huko.

Kwa kifupi UDART wanaenda kupoteza lengo halisi LA wao kuwepo.. Ndio wanatakiwa kupata faida kidogo itakayosaidia kujiendesha..ila lengo lao kuu ni kutoa huduma.. Wanapaswa kwenda na muda kuliko kuwa kama kamjingijingi trans.. Nilitegemea kwa muda huu wawe na gari zinapita vituoni kila baada ya dk 10 kama jua.. Kwa ratiba.. Unadhani watu wangekuwa wanajazana mpaka wanavunja milango ya magari?!

Wajipange waache ujinga.
 
Mabasi yamepaki abiria wanaangaika usafiri.
Huu ni ushamba waendeshaji wanasababisha usumbufu na kero kubwa.

Badilikeni mtu amekata tiketi anakaa kituoni dakika 30.
Ushamba au dharau
Tatizo unasubiri basi la moja kwa moja unakoenda, utachoma sana mahindi. Tumia akili, tiketi hiyo hiyo, fanya connection.
Au unakuta mtu kilaza, anaogopa express kutoka kimara sababu anashukia usalama, panda express ikisimama fire au dit, rudi na basi nyingine usalama! Umeokoa muda.
 
Biashara ikishakua ya mtu mmoja anafanya anavyotaka kwani hakuna ushindani. Wasimamizi nao (serikali) wanaangalia mapato tu bila kuangalia huduma inayotolewa na huyo waliyemuamini. Hili ndio tatizo linalokumba Tanzania sekta zote za umma
 
Kwa ufupi huu mradi umegongelea msumari kwenye tatizo kubwa la nchi zetu za afrika na sisi wenyewe Poor administration.

Mradi umefeli vibaya sana. Nchi za wenzetu haijalishi basi limejaa au halijajaa kinachoangaliwa ni mapato tuu na muda ulipangwa ni lazima basi lipakie sasa hapa wanacheza singeli kwenye mradi.
 
Msiwaponde kabisa hao kwanza nampongeza aliefikiria hilo maana imesaidia sana Nchi kama SA mwendokasi ilipelekwa kabla ya 2010 kombe la Dunia kwa hiyo nina imani ni changamoto ambayo wataifanyia kazi vizuri tuu...ukipanda Kkoo dakika chache upo kimara...
 
jinsi UDA ilivyouzwa kifisadi tulitegemea mzalendo magu angechukua hatua lakini badala yake alibariki uhuni ule!!!
 
Wa kijanja ndo UPI kwani?

Kwani wee kabla ya hapo ulikua unatumia usafiri gani?

Rudi uko uko kwny UDA na vidaladala uone thamani ya kutoka nusu Saa kituoni
Aliposema ushamba mimi nimemwelewe. Duniani kote mabasi ya Rapid uenda kwa muda uliopangwa regardless kuna abiria au hakuna. Ni mabasi yanayokwenda kwa ratiba siyo kusubiri abiria kujaza. Sasa ushamba wa hawa ni pale wanapoanza kuangalia wingi wa abiria na kuaharibu ratiba
 
Back
Top Bottom