Mwanajamii
JF-Expert Member
- Mar 5, 2008
- 7,063
- 68
Kama una uchungu wa dhati na nchi hii habari hii haitakuwa ndefu kusoma. Imeletwa kwenu na mchungaji Christopher Mtikila kupitia gazeti la uhuru.
Tumefurahishwa na taarifa za kizalendo kutoka ndani ya TAKUKURU kwamba thamani ya shirika la Usafiri Dar es salaam (UDA) ambalo ni mali ya wananchi siyo shilingi bilioni 11 tu kama ilivyokisiwa awali, bali ni zaidi ya shilingi bilioni 20.
Kwani shirika la UDA siyo tu lina karakana ya uhandisi ambayo ni moja ya kubwa kuliko zote katika Afrika Mashariki, ikiwa na mashine za kila aina na mitambo ya kila huduma, tulivyopewa na Wajerumani ambao dunia inawaheshimu kwa ubingwa wao katika uhandisi, bali pia shirika lina mali nyingi sana zisizohamishika.
Kwa mujibu wa Ibara ya 27 ya katiba ya nchi, inayomuwajibisha kila raia kulinda mali asilia ya taifa letu, mali ya mamlaka ya nchi na mali yote inayomilikiwa kwa pamoja na wananchi, na kututaka sisi sote tutunze vizuri mali yote ya mamalaka ya nchi na ya pamoja kama shirika letu la UDA, na kupiga vita aina zote za uharibifu na ubadhirifu na kuendesha uchumi wa taifa letu kwa makini kama watu ambao ndio waamuzi wa hali ya baadaye ya nchi yao, tunatoa tamko kwamba:
1. Wahusika wote katika serikali yetu yaani Waziri wa Fedha, Waziri wa Uchukuzi na Waziri wa tawala za Mikoa na serikali za Mitaa wanapaswa kufikishwa Mahakamani mara moja kwa uharibifu na ubadhirifu wa mali za mabilioni ya fedha za shirika letu la UDA.....saa ya ukombozi ni sasa.
2. shirika la thamani ya zaidi shilingi bilioni 22 kuuziwa Robert Kisena kwa shilingi bilioni moja tu na robo, bila kutangaza tenda ya wazi kama inavyopasa kisheria na kupata mwekezaji wa kweli mwenye zaidi ya hizo bilioni 22, lakini huyo Robet kisena akalipa shilingi milioni 285 tu na kukabidhiwa mali ya wananchi ya shilingi bilioni 22 ni Ufisadi kichaa! Mauzo yabadilishwe mara moja, na Robert Kisena pamoja na hao watumishi wa umma waliokula naye dili hii wakamatwe na kufikishwa mbele ya sheria ndani ya siku saba! Uharamia huu ndio unaopaswa kumalizwa kwa risasi hadharani! tutahakikisha kuwa sheria ya adhabu hii inatungwa upesi sana, ...saa ya ukombozi ni sasa.
3. Shirika la UDA ni usafiri wa wananchi katika jiji la Dar es salaam, hivyo mwekezaji anayetakiwa ni wa kuliboresha kwa ajili ya huduma hiyo, siyo wa kuliua! Robert Kisena ameharibu na kukongoloa kabisa mitambo na mashine zote za UDA za mabilioni ya fedha mashine nyingine zimekatwa na kuuzwa kama chuma chakavu 'scrap'! Karakana ya UDA yeye (kisena) anazipangisha kama maghala ya kuweka mtama wa kampuni ya pombe, na uwanja wa mabasi yeye anakodisha wenye makontena kama bandari kavu! kuharibu mitambo na mashine za umma za mabilioni ya fedha kama mwendawazimu ni kosa kubwa sana la jinai, ni lazima Robert Kisena akamatwe mara moja na kufikishwa mbele ya sheria kwa uharibifu kuu wa kutisha.
4. Mali zote za Robert Kisena anazomiliki kwa jina lake au kwa majina ya kibiashara zikamatwe kwa amri ya Mahakama tayari kwa kuuzwa, ili kurejesha mashine na mitambo ya UDA alizoharibu, pamoja na mali zingine alizofuja. Ikiwa mali zake zimekopewa mapesa katika mabenki, wanaomdai watakatiwa sehemu yao baada ya kulipia mali za UDA.
5. Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU ameshangaza ulimwengu kwa kuwafikisha mahakamani akina Iddi simba kwa kupokea rushwa ya kisena, lakini yeye mtoaji wa hiyo rushwa amemwacha, kinyume kabisa cha sheria! Robert Kisena anayo hatia ya wazi kabisa ya utoaji wa rushwa ya shilingi 320 iliyo dhahiri hata kwa kipofu! Ni lazima Robert Kisena akamatwe mara moja na kuunganishwa na wenzake aliowapa hiyo rushwa.
6. Robert Kisena apigwe marufuku kuonekana UDA kwa sababu hana mpango kabisa wa kuboresha shirika letu la usafiri., kwani hata mabasi yaliyotolewa na benki ya CRDB kusaidia kusafirisha wanafunzi jijini ameshindwa kuyaendesha kwa ajili ya watoto wetu, mpaka benki imelazimika kuyavuta kutoka kurasini wiki hii.
7. Tunataka ripoti ya Mkaguzi Mkuu wa Mahesabu ya Fedha za serikali iwekwe wazi bungeni haraka, na wabunge wa Dar es salaam wahakikishe kwamba yaliyoagizwa na Mkaguzi Mkuu huyo yanatekelezwa kwa ajili ya ya maslahi ya taifa letu.
Kuhusu uvumi uliozagaa kwamba Robert Kisena eti analindwa na Rais Kikwete katika uharibifu na ubadhirifu huu wa kutisha, tunasema kwamba yaweza kuwa hila tu ya hawa waporaji ya kujificha katika jina la KIKWETE! Nchi yetu haingozwi na majina ya watu bali na katiba na sheria. Hawa ni wabaya wa Kikwete, wanaotaka kumharibia maisha yake baada ya kuondoka madarakani yawe machungu.
Hivyo, kama alivyowaondoa mara moja Mawaziri waporaji wa nchi yetu kutokana na ripoti ya Mkaguzi Mkuu wa Fedha za Umma, ambo ni lazima awafikishe mbele ya sheria, Kikwete analazimika pia kuwatupa kizimbani mara moja vigogo wote walioimemena UDA yetu pamoja na Robert Kisena... saa ya ukombozi ni sasa!
Kama tulivyotamkwa katika kipengere 1 - 7 hapo juu yataonekana kuchelewa kutekelezwa na kuendelea kuwaudhi wanannchi, DP kwa nguvu ya Ibara ya 27 ya katiba ya nchi itachukua hatua kali. saa ya ukombozi ni sasa!
MCHUNGAJI C. MTIKILA
MWENYEKITI DP
2 JUNI, 2012
SOURCE: GAZETI LA UHURU 5 JUNI, 2012 UKURASA WA TATU.
Tumefurahishwa na taarifa za kizalendo kutoka ndani ya TAKUKURU kwamba thamani ya shirika la Usafiri Dar es salaam (UDA) ambalo ni mali ya wananchi siyo shilingi bilioni 11 tu kama ilivyokisiwa awali, bali ni zaidi ya shilingi bilioni 20.
Kwani shirika la UDA siyo tu lina karakana ya uhandisi ambayo ni moja ya kubwa kuliko zote katika Afrika Mashariki, ikiwa na mashine za kila aina na mitambo ya kila huduma, tulivyopewa na Wajerumani ambao dunia inawaheshimu kwa ubingwa wao katika uhandisi, bali pia shirika lina mali nyingi sana zisizohamishika.
Kwa mujibu wa Ibara ya 27 ya katiba ya nchi, inayomuwajibisha kila raia kulinda mali asilia ya taifa letu, mali ya mamlaka ya nchi na mali yote inayomilikiwa kwa pamoja na wananchi, na kututaka sisi sote tutunze vizuri mali yote ya mamalaka ya nchi na ya pamoja kama shirika letu la UDA, na kupiga vita aina zote za uharibifu na ubadhirifu na kuendesha uchumi wa taifa letu kwa makini kama watu ambao ndio waamuzi wa hali ya baadaye ya nchi yao, tunatoa tamko kwamba:
1. Wahusika wote katika serikali yetu yaani Waziri wa Fedha, Waziri wa Uchukuzi na Waziri wa tawala za Mikoa na serikali za Mitaa wanapaswa kufikishwa Mahakamani mara moja kwa uharibifu na ubadhirifu wa mali za mabilioni ya fedha za shirika letu la UDA.....saa ya ukombozi ni sasa.
2. shirika la thamani ya zaidi shilingi bilioni 22 kuuziwa Robert Kisena kwa shilingi bilioni moja tu na robo, bila kutangaza tenda ya wazi kama inavyopasa kisheria na kupata mwekezaji wa kweli mwenye zaidi ya hizo bilioni 22, lakini huyo Robet kisena akalipa shilingi milioni 285 tu na kukabidhiwa mali ya wananchi ya shilingi bilioni 22 ni Ufisadi kichaa! Mauzo yabadilishwe mara moja, na Robert Kisena pamoja na hao watumishi wa umma waliokula naye dili hii wakamatwe na kufikishwa mbele ya sheria ndani ya siku saba! Uharamia huu ndio unaopaswa kumalizwa kwa risasi hadharani! tutahakikisha kuwa sheria ya adhabu hii inatungwa upesi sana, ...saa ya ukombozi ni sasa.
3. Shirika la UDA ni usafiri wa wananchi katika jiji la Dar es salaam, hivyo mwekezaji anayetakiwa ni wa kuliboresha kwa ajili ya huduma hiyo, siyo wa kuliua! Robert Kisena ameharibu na kukongoloa kabisa mitambo na mashine zote za UDA za mabilioni ya fedha mashine nyingine zimekatwa na kuuzwa kama chuma chakavu 'scrap'! Karakana ya UDA yeye (kisena) anazipangisha kama maghala ya kuweka mtama wa kampuni ya pombe, na uwanja wa mabasi yeye anakodisha wenye makontena kama bandari kavu! kuharibu mitambo na mashine za umma za mabilioni ya fedha kama mwendawazimu ni kosa kubwa sana la jinai, ni lazima Robert Kisena akamatwe mara moja na kufikishwa mbele ya sheria kwa uharibifu kuu wa kutisha.
4. Mali zote za Robert Kisena anazomiliki kwa jina lake au kwa majina ya kibiashara zikamatwe kwa amri ya Mahakama tayari kwa kuuzwa, ili kurejesha mashine na mitambo ya UDA alizoharibu, pamoja na mali zingine alizofuja. Ikiwa mali zake zimekopewa mapesa katika mabenki, wanaomdai watakatiwa sehemu yao baada ya kulipia mali za UDA.
5. Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU ameshangaza ulimwengu kwa kuwafikisha mahakamani akina Iddi simba kwa kupokea rushwa ya kisena, lakini yeye mtoaji wa hiyo rushwa amemwacha, kinyume kabisa cha sheria! Robert Kisena anayo hatia ya wazi kabisa ya utoaji wa rushwa ya shilingi 320 iliyo dhahiri hata kwa kipofu! Ni lazima Robert Kisena akamatwe mara moja na kuunganishwa na wenzake aliowapa hiyo rushwa.
6. Robert Kisena apigwe marufuku kuonekana UDA kwa sababu hana mpango kabisa wa kuboresha shirika letu la usafiri., kwani hata mabasi yaliyotolewa na benki ya CRDB kusaidia kusafirisha wanafunzi jijini ameshindwa kuyaendesha kwa ajili ya watoto wetu, mpaka benki imelazimika kuyavuta kutoka kurasini wiki hii.
7. Tunataka ripoti ya Mkaguzi Mkuu wa Mahesabu ya Fedha za serikali iwekwe wazi bungeni haraka, na wabunge wa Dar es salaam wahakikishe kwamba yaliyoagizwa na Mkaguzi Mkuu huyo yanatekelezwa kwa ajili ya ya maslahi ya taifa letu.
Kuhusu uvumi uliozagaa kwamba Robert Kisena eti analindwa na Rais Kikwete katika uharibifu na ubadhirifu huu wa kutisha, tunasema kwamba yaweza kuwa hila tu ya hawa waporaji ya kujificha katika jina la KIKWETE! Nchi yetu haingozwi na majina ya watu bali na katiba na sheria. Hawa ni wabaya wa Kikwete, wanaotaka kumharibia maisha yake baada ya kuondoka madarakani yawe machungu.
Hivyo, kama alivyowaondoa mara moja Mawaziri waporaji wa nchi yetu kutokana na ripoti ya Mkaguzi Mkuu wa Fedha za Umma, ambo ni lazima awafikishe mbele ya sheria, Kikwete analazimika pia kuwatupa kizimbani mara moja vigogo wote walioimemena UDA yetu pamoja na Robert Kisena... saa ya ukombozi ni sasa!
Kama tulivyotamkwa katika kipengere 1 - 7 hapo juu yataonekana kuchelewa kutekelezwa na kuendelea kuwaudhi wanannchi, DP kwa nguvu ya Ibara ya 27 ya katiba ya nchi itachukua hatua kali. saa ya ukombozi ni sasa!
MCHUNGAJI C. MTIKILA
MWENYEKITI DP
2 JUNI, 2012
SOURCE: GAZETI LA UHURU 5 JUNI, 2012 UKURASA WA TATU.