Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 34,095
- 43,305
- Kiongozi anayetewala kwa vitisho, ameishiwa maono
- Mtu akikutisha maana yake ameshindwa kukushawishi
- Wakianza kuzungumzia umwagikaji damu, wanajiandaaa kuimwaga
- Ukiona watu wanapiga kelele, usidhani wote wanashangilia; wengine wanalia!
- Ukiona watu wazima wanachekacheka mbele ya bosi, ujue wanajikomba!
- Haki haitolewi bila gharama
- Shawishi upewe haki yako, ukikataliwa lazimisha kwani hauna cha kupoteza isipokuwa haki yako!
- Historia ya watawala duniani ni kuwaridhisha matajiri, hadi maskini watakapoamka kutaka kubadilisha historia na watawala!
- Usiwasukumize maskini hadi wakakosa pa kusimamia; wakianza kukusukumiza utakosa pa kuhamia!
- Mfumo wa utawala wa kifisadi hauwezi kubadilishwa na wanufaikaji wake wakuu! Yaani, uwaambie fisi wabadili utaratibu wa kula mifupa?
- CCM haiwezi kuondolewa madarakani kwa kuombewa au kungojewa; itaondolewa kwa kusababishwa!
- Katika demokrasia wananchi wana haki ya kuchagua ubovu; na wana haki ya kuishi na matokeo ya uchaguzi wao huo hadi watakapoamka na kuchagua vyema!
- Hakuna haki ya kuipenda serikali; katika demokrasia kuichukia serikali ndio msingi wa kuipigia kura ya kuiondoa! Hivyo, chuki dhidi ya serikali siyo uhaini ni sehemu ya demokrasia!
- Sehemu moja ya ushiriki wa wananchi katika demokrasia ni katika kuwahoji, kuwapinga na kuwakosoa viongozi wao; pasipo kuwaomba msamaha kwanza!
- Wafanyakazi wakisalimu amri watawala watawapangia mishahara kwa amri!
- Mtawala akizungumza sana na kwa kirefu tena kwa jazba na manjonjo akimaliza wewe kataa! itabidi akushawishi vinginevyo atarudia tena!
Zote na M.M.