Hata ikiwa uongo watu watahisi kweli, tatizo mnaharibu sana kuliko kujenga ndugu zangu.
Tatizo letu watanzania ni kutokuwa makini kwa kila jambo, tumekuwa ni watu wa kubabaisha babaisha mno hata mahali palipo na usahihi wa hoja, Tabia hii tunayoiendekeza itaendele kututafuna kwa karne nyingi zijazo isipokuwa tumejifunga mkanda kuondoa udhaifu wa watawala. NASEMA hivi kwa sababu hatutakiwa kuwasaidia wamasai wa Loliondo tu kuna wamakonde pia wa Mtwara ambao wanapangiwa kudhulumiwa gesi bila majadiliano; Munapokaa kimya kwa hili na kuangalia mahali fulani hatutafika kokote. Namkumbuka mwanajamii fulani aliandika humu kuwa "walipokuwa wanawapiga wagiriki sisi tulikaa kimya kwa sababu sisi siyo wagiriki. Wakawaendea wasomali kuwapiga tukakaa kimya kwa sababu sisi siyo wasomali, SASA wamekuja kutupiga sisi, lo hayupo hata wa kutusaidia kwa sababu wagiriki na wasomali wote ambao wangetusaidia wamekwisha uawa wote"