A
Anonymous
Guest
Kuanzia mwezi Aprili, 2026, jirani yetu mmoja amefungua gereji isiyo rasmi (garage bubu) ndani ya mtaa huu wa makazi, na ameigeuza kuwa sehemu ya kupakia na kushushia mizigo ya malori makubwa. Kutokana na hali hiyo, malori hayo yamekuwa yakipaki nje ya mageti ya nyumba zetu, jambo linalosababisha usumbufu mkubwa kwa wakazi.
Tulifika kwa Mwenyekiti wa Mtaa ili kupata ufumbuzi, lakini hadi sasa hakuna hatua madhubuti zilizochukuliwa. Inasemekana kuwa ameshapewa ushawishi usio rasmi, hali inayozua wasiwasi juu ya uwajibikaji wake. Pia tulitoa taarifa kwa TARURA, lakini hatujapata ushirikiano wowote hadi sasa.
Kutokana na hali hiyo, tunaomba mamlaka husika ziingilie kati haraka iwezekanavyo ili: Kusitisha matumizi ya eneo hilo kama kituo cha malori, Kuchukua hatua za kisheria dhidi ya mhusika, Kulinda usalama na haki za wakazi wa eneo hili.
Tunaamini mamlaka itachukua hatua stahiki ili kurejesha utulivu na usalama katika mtaa wetu.