Mwanyamaki aitisha CCM Kyela

Mwanyamaki aitisha CCM Kyela

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
137,558
Reaction score
272,302
Wakuu natanguliza salamu,

Niko Kyela ila bila kuficha kitu CCM wana hali mbaya mno !

Baada ya kujua uwezo mkubwa wa ushawishi alionao mgombea wa CHADEMA ndugu Mwanyamaki, wamejaza udongo mchafu kwenye barabara zote za mjini ( tena kwa hati ya dharula ) ili kuwalaghai wananchi , ionekane kama vile wamedhamiria kukarabati barabara zilizowashinda kwa karibu miaka 60.

Hata hivyo wananchi wameshtukia ulaghai huo na wameapa kuitosa CCM kama walivyofanya kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa.

Pole Mwakyembe,pole CCM jimbo limekwenda. Mlipewa muda mkauchezea tusilaumiane.
 
Barabara mbovu za mji wa Kyela ndio kitanzi cha CCM hawana pa kutokea .
 
Hamjaweza washawishi watu wa ngonga kule wenyewe hawambiliki kuhusu CCM, wiki iliyopita nilikua huko kila nikijaribu kutoa elimu ya uraia hawaelewi
 
barabara mbovu za mji wa kyela ndio kitanzi cha ccm hawana pa kutokea .

Unajua barabara mbovu wewe? Nenda manispaa ya Tabora ukajifunze kutofautisha barabara mbovu . Kyela ina hali nzuri kuliko hata makao makuu ya Mikoa mingi tu Tanzania. Kinachokosekana Kyela ni ubunifu wa kutumia mito mingi waliyojaaliwa pamoja nz ziwa kuwe na kilimo cha umwagiliaji.
 
Unajua barabara mbovu wewe? Nenda manispaa ya Tabora ukajifunze kutofautisha barabara mbovu . Kyela ina hali nzuri kuliko hata makao makuu ya Mikoa mingi tu Tanzania. Kinachokosekana Kyela ni ubunifu wa kutumia mito mingi waliyojaaliwa pamoja nz ziwa kuwe na kilimo cha umwagiliaji.
kwa neema iliyopo kyela haikutakiwa kuwa na vumbi kiasi hiki , halafu kama kweli barabara za kyela ni nzuri kilichowafanya ccm kuhangaika na udongo mchafu wenye vumbi kali na zito ni nini ? tena kuelekea uchaguzi , kiasi cha wafanyabiashara kushindwa kabisa kufanya biashara zao ? hauko kyela mkuu , hali ni mbaya kuliko maelezo .
 
hamjaweza washawishi watu wa ngonga kule wenyewe hawambiliki kuhusu ccm, wiki iliyopita nilikua huko kila nikijaribu kutoa elimu ya uraia hawaelewi
kwa mipango iliyopangwa kuelekea uchaguzi ccm ikiambulia hata kata moja wafanye sherehe .
 
Mkuu basi jambo Jema nimeshuudia pale kwetu ccm wanajisifu sana

tutahakikisha ccm inatokomezwa kyela , ushahidi usio na shaka ni ule uchaguzi hafifu wa serikali za mitaa .
 
Ila bwana red blood cell umenichanganya! Huyo Mwanyamaki ni mgombea wa ccm au cdm? Nifafanulie tafadhali
 
Hali halisi kisiasa pale Kyela iko hivi:-
Kama CCM watampitisha mh Mwakyembe huenda CCM ikapoteza jimbo
Lakini wakimpitisha jamaa mmoja anaitwa Mwakalinga yule mmiliki wa Kyela FM wanaweza kutetea kiti chao,,,,,
Ni juu ya CCM kuamua hayo matokeo... kwani kwa upande wa upinzani hakuna wa kuweza kusimama na Mwakalinga lakini wanaweza kukosoa utendaji wa Mwakyembe kwa kiasi kikubwa.
 
Vipi kuhusu masdiwani apo kyela sisi kule ngonga tunae kileo hajui kusoma kuandika anajua jina lake tu
 
Mpigie Kura George Mwakalinga au Mtanzańia wa Jamiiforums ambaye ni mmoja wa waliokuwepo mwanzo JF.

 
Last edited by a moderator:
Mpigie Kura George Mwakalinga au Mtanzańia wa Jamiiforums ambaye ni mmoja wa waliokuwepo mwanzo JF.


nakujulisha ili ujiandae kiakili na kimwili , kyela hatakiwi mtu yeyote anayeshabihiana na ccm , inyeshe mvua au liwake jua , tumechoka kabisa na vumbi kali mjini na maji yenye vimelea vya kichocho , tukuti mma ! apa batutwele abha ccm pafwene , ubhulondo twemma tukanile kikolo .
 
Last edited by a moderator:
Hali halisi kisiasa pale Kyela iko hivi:-
Kama CCM watampitisha mh Mwakyembe huenda CCM ikapoteza jimbo
Lakini wakimpitisha jamaa mmoja anaitwa Mwakalinga yule mmiliki wa Kyela FM wanaweza kutetea kiti chao,,,,,
Ni juu ya CCM kuamua hayo matokeo... kwani kwa upande wa upinzani hakuna wa kuweza kusimama na Mwakalinga lakini wanaweza kukosoa utendaji wa Mwakyembe kwa kiasi kikubwa.
kwanini unadhani mwakalinga anaweza kushinda , kwa lipi alilowahi kulifanya ( lete mifano ) , nakuhakikishia kwamba ccm haitakiwi kyela hata akija kinana kugombea .
 
halafu wanajf na hasa wana kyela hamna sababu ya kuogopa changes , ushindi wa serikali za mitaa kuna mabadiliko makubwa sana yanayoonekana na yasiyoonekana kwa jicho la kawaida , visima vya mani vimefufuliwa kwa muda mfupi sana , lakini kuna hili la viongozi wa ccm kutisha na kushughulikia wafanyabiashara wanaounga mkono upinzani , hili lilikuwa jambo kubwa na baya sana ( rip mwakasumi ) , lakini cdm wamefutilia mbali kabisa jambo hili na sasa kila mtu ruksa kushiriki siasa bila hofu wala uoga .
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom