Kiongozi nimesimuliwa majuzi nikashangaa sana. Yote niliyosimuliwa yanashabihiana na uliyoandika. Kwanza ni kweli Ndugai anahusika, pili Mwanjelwa anaona hana chake.
Mojawapo la kosa kubwa alilolifanya Tulia ni kwenda Mbeya Mjini akimtambulisha Mwaselela. Watu wakawa hawajui kama Tulia atagombea Tukuyu au Mbeya, na yamkini anataka amsaidie Mwaselela kugombea jimbo la Mbeya jiji. Tukuyu itakuwa changamoto sana kwa Tulia kupata ubunge. Lakini pia Tulia akiwa Mbeya mjini atatoa uwakilishi mzuri.
Sasa kumeingizwa ukabila. Wasafwa wote wameamua kumsapoti Mwaselela. Mwaselela ni msafwa lakini wana asili ya Unyakyusani. Pia Mwaselela anapewa sapoti na wasafwa wenzake kama Benson Mpesya, Advocate Shitambala na wengine wengi. Hata yule MC maarufu kwenye mikutano ya kisiasa ndugu Mwakipesile yuko upande wa Mwaselela.
Mimi nawashauri wana Mbeya, wachague mtu ambaye ni influential. Haya mambo ya kuchagua mbunge kwa sababu ya kabila na kukomoana yanawaumiza wenyewe. Kwa sasa mtu influential kwao upande wa CCM ni Tulia Ackson. Hao wakina Mwaselela they are not political material. Watapoteza muda tu.
Ila pia ningekuwa Mwaselela ningetulia kwanza. Ataharibu future yake ya biashara kwa mikwaruzano ya kisiasa. Kwa sasa siasa inalipa kwa watu wachache sana.