Elections 2010 Mwandosya ataja sababu za kumpigia kampeni JK

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,318
33,125
Mwandosya%2810%29.jpg

Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Profesa Mark Mwandosya



Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Profesa Mark Mwandosya, ameainisha sababu kadhaa za kumpigia kampeni Rais Jakaya Kikwete kwa wananchi wa mkoa wa Mbeya, ili wamchague katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 31, mwaka huu.
Profesa Mwandosya, alikuwa miongoni mwa wanachama watatu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), waliofuzu kuingia `tatu bora' ya kuomba ridhaa ya chama hicho kuwania urais mwaka 2005.
Wengine walikuwa ni Waziri Mkuu mstaafu, Dk Salim Ahmed Salim na Jakaya Kikwete aliyeibuka kuwa mshindi.
Profesa Mwandosya ambaye pia ni mgombea ubunge wa jimbo la Rungwe mkoani hapa, alitoa sababu hizo jana katika viwanja vya kata ya Nzovwe mjini hapa, wakati akizindua kampeni za CCM katika jimbo la Mbeya Mjini.
Alizitaja sababu hizo kuwa ni mafanikio yake (Kikwete) katika kuleta na kusimamia umoja, amani na utulivu, kupunguza utegemezi wa Taifa kwa wahisani kutoka asilimia 49 hadi 28 kwa kipindi cha kati ya 2005 na 2010.
Alifafanua kuwa suala la kupunguza utegemezi, limeiwezesha nchi kuendesha miradi mikubwa kama wa maji kutoka ziwa Victoria hadi Kahama mkoani Shinyanga kwa kutumia fedha za ndani.
Manufaa mengine kwa mujibu wa Profesa Mwandosya, ni ujenzi wa uwanja wa ndege wa Songwe unaogharimu zaidi ya Sh bilioni 70 ambapo kati ya hizo, Sh bilioni 15 zinatoka kwa wahisani.
Alitaja sababu nyingine kuwa ni heshima aliyoijengea Tanzania nje ya nchi, kuleta mustakabali wa kisiasa Zanzibar na kudhibiti ujambazi.
Profesa Mwandosya alisema zipo sababu nyingine ambazo Rais Kikwete hawezi kuzisema mwenyewe, isipokuwa yeye kwa vile anamfahamu vizuri baada ya kufanya naye kazi kwa miaka zaidi ya 20, aliamua kumsemea.
Alizitaja sababu nyingine kuwa ni upole wake (Kikwete), mchangamfu na mwenye tabasamu na anayependa makundi ya rika zote bila ubaguzi.
Hata hivyo, alisema kwa upande wa pili Rais Kikwete ni mkali wakati wa ufuatiliaji wa utekelezaji wa mambo aliyowaahidi wananchi.
“Ukali huu wa Rais Kikwete ninausema hadharani, kwa sababu mimi nauona kama ni sifa, kwa kweli anapofuatilia mambo aliyowaahidi wananchi anakuwa mkali sana, hapendi masihara,” alisema .



CHANZO: NIPASHE
 
Alizitaja sababu nyingine kuwa ni upole wake (Kikwete), mchangamfu na mwenye tabasamu na anayependa makundi ya rika zote bila ubaguzi

Hapa anamaanisha mafisadi lowassa, rostam, manji, jeetu patel na wenzake
 
Mwandosya%2810%29.jpg

Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Profesa Mark Mwandosya



Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Profesa Mark Mwandosya, ameainisha sababu kadhaa za kumpigia kampeni Rais Jakaya Kikwete kwa wananchi wa mkoa wa Mbeya, ili wamchague katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 31, mwaka huu.
Profesa Mwandosya, alikuwa miongoni mwa wanachama watatu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), waliofuzu kuingia `tatu bora' ya kuomba ridhaa ya chama hicho kuwania urais mwaka 2005.
Wengine walikuwa ni Waziri Mkuu mstaafu, Dk Salim Ahmed Salim na Jakaya Kikwete aliyeibuka kuwa mshindi.
Profesa Mwandosya ambaye pia ni mgombea ubunge wa jimbo la Rungwe mkoani hapa, alitoa sababu hizo jana katika viwanja vya kata ya Nzovwe mjini hapa, wakati akizindua kampeni za CCM katika jimbo la Mbeya Mjini.
Alizitaja sababu hizo kuwa ni mafanikio yake (Kikwete) katika kuleta na kusimamia umoja, amani na utulivu, kupunguza utegemezi wa Taifa kwa wahisani kutoka asilimia 49 hadi 28 kwa kipindi cha kati ya 2005 na 2010.
Alifafanua kuwa suala la kupunguza utegemezi, limeiwezesha nchi kuendesha miradi mikubwa kama wa maji kutoka ziwa Victoria hadi Kahama mkoani Shinyanga kwa kutumia fedha za ndani.
Manufaa mengine kwa mujibu wa Profesa Mwandosya, ni ujenzi wa uwanja wa ndege wa Songwe unaogharimu zaidi ya Sh bilioni 70 ambapo kati ya hizo, Sh bilioni 15 zinatoka kwa wahisani.

Alitaja sababu nyingine kuwa ni heshima aliyoijengea Tanzania nje ya nchi, kuleta mustakabali wa kisiasa Zanzibar na kudhibiti ujambazi.
Profesa Mwandosya alisema zipo sababu nyingine ambazo Rais Kikwete hawezi kuzisema mwenyewe, isipokuwa yeye kwa vile anamfahamu vizuri baada ya kufanya naye kazi kwa miaka zaidi ya 20, aliamua kumsemea.
Alizitaja sababu nyingine kuwa ni upole wake (Kikwete), mchangamfu na mwenye tabasamu na anayependa makundi ya rika zote bila ubaguzi.
Hata hivyo, alisema kwa upande wa pili Rais Kikwete ni mkali wakati wa ufuatiliaji wa utekelezaji wa mambo aliyowaahidi wananchi.
"Ukali huu wa Rais Kikwete ninausema hadharani, kwa sababu mimi nauona kama ni sifa, kwa kweli anapofuatilia mambo aliyowaahidi wananchi anakuwa mkali sana, hapendi masihara," alisema .



CHANZO: NIPASHE

..........Dahh hawa mashemeji sasa naona wameanza kuchanganyikiwa..........mpaka wanasema UONGO..........duuhh........huu uchaguzi mwaka huu...............
 
..........Dahh hawa mashemeji sasa naona wameanza kuchanganyikiwa..........mpaka wanasema UONGO..........duuhh........huu uchaguzi mwaka huu...............

sasa ukweli ndo upi tena...lete data
 
Naona bora angekaa kimya tu..kuliko kuanza kuchemka
Hawa ndio 'maprofesa' wasio hata na website au hata ka-page ka kuzugia na haieleweki when was the last time walicontribute kwene field zao(?). Nways siasani kunamfaa maana ni wazi challenge ya dunia ya leo vimemshinda kwene field yake.
 
Profesa Mswandosya anasema Kikwete amepunguza utegemezi wetu wa misaada. Alinyimwa misaada. Kama anavyoandika Fumbuka Ng'wanakilala katika gazeti la The Econiomic Monitor la Mei 14, 2010:


Donors have slashed funding pledges for Tanzania's 2010/11 (July-June) budget by nearly a quarter of a billion dollars to $534 million due to concerns about the slow pace of reforms in the country.


The east African nation of 40 million people is among the continent's biggest per capita aid recipients. Foreign assistance made up 33 percent of Tanzania's 2009/10 budget and hard currency donor inflows help support the currency.


"This commitment is $220 million less than ... financial year 2009/10 and raises concerns of GBS (general budget support) decreasing to the lower levels disbursed in 2005 and 2006," a group of donors said in a statement seen by Reuters on Friday.


http://www.ibtimes.com/articles/23727/20100514/donors-to-slash-tanzania-budget-aid.htm


Mradi wa maji toka Ziwa Victoria hadi Kahama ni wa Mkapa. Kikwete hangeuweza. Anatumia fedha vibaya mno. Kumbukeni ameteua mawaziri zaidi ya 60, akiwemo Profesa Mwandosya.


Profesa hajui kwamba Tanzania imekosa amani na utulivu kipindi hiki cha Kikwete zaidi ya wakati mwingine wowote? Kumejaa chuki za UDINI, dharau za walionacho na wasionacho, na kukata tamaa, kuliko wakati mwingine wowote.


Profesa Mwandosya anashabikia mpango wa kujenga kiwanja cha ndege Songwe cha bilioni 70. Ndege zenyewe ziko wapi? It is a white elephant.


Rais Kikwete alitembelea Cuba, na akapokelewa na Makamu wa Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje. Yaani hata Cuba inatudharau siku hizi. Si kweli kwamba Kikwete amejenga heshima ya Tanzania nje. Ameirudisha nyuma, tena sana.

Nasikitika kuona mtu kama Profesa Mwandosya anaweza kuwa hivi. He used to be Presidential material.
 
Hawa ndio 'maprofesa' wasio hata na website au hata ka-page ka kuzugia na haieleweki when was the last time walicontribute kwene field zao(?). Nways siasani kunamfaa maana ni wazi challenge ya dunia ya leo vimemshinda kwene field yake.

Kama huna data bora usiseme, prof. Mwandosya hana contribution kwenye field yake?
 
Kawambwa ahimiza ujenzi wa Kiwanja cha ndege Songwe


na Gordon Kalulunga, Mbeya



WAZIRI wa Miundombinu, Dk. Shukuru Kawambwa, amehamasisha ukamilishaji wa Kiwanja cha Ndege cha Songwe, kilichopo mkoani Mbeya, baada ya kutembelea uwanja huo na kuukagua, kisha kuzungumza na mkandarasi na mhandisi mshauri wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege nchini uwanjani hapo.
Kawambwa alitembelea na kuukagua uwanja huo juzi na kuwahimiza Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Mkandarasi Kampuni ya Kundan Singh Construction Ltd ya nchini Kenya na mhandisi mshauri kutoka Falme za Kiarabu kuhakikisha ujenzi wa uwanja huo unakamilika mapema iwezekanavyo.
Waziri huyo alisema kuwa kwa sababu awali kikwazo cha uendelezaji wa ujenzi wa uwanja huo kilikuwa ni kutolipwa malipo ya awali mkandarasi anayejenga uwanja huo, lakini kwa sasa tayari serikali imekwisha kulipa deni hilo, hivyo hatarajii kuendelea kusuasua kwa ujenzi katika kiwanja hicho.
"'Kwa sababu serikali imelipa fedha zote za malipo ya awali kwa mkandarasi, hivyo hatutarajii kuona ujenzi wa uwanja huu ukisuasua kama mwanzo, maana kikwazo kilikuwa ni fedha,"' alisema Waziri Kawambwa.
Aidha, alifafanua kuwa ifikapo Januari mwaka 2010 anatarajia kupata taarifa nzuri zaidi za maendeleo ya ujenzi wa uwanja huo, ambao ni tegemeo kubwa la wananchi wa Kanda ya Nyanda za Juu Kusini na taifa kwa ujumla.
"'Kwa kipindi cha mwaka wa bajeti 2008/2009 serikali imetenga sh bilioni 18 kwa ajili ya umaliziaji wa ujenzi wa kiwanja hiki ambacho kina umuhimu sana kwa taifa letu, hivyo ni muhimi pia nanyi kama wataalamu mkaona kuwa ni jinsi gani serikali ilivyoupa kipaumbele uwanja huu," alisema Kawambwa kwa matumaini ya kumalizika kwa uwanja huo kama matarajio ya serikali yalivyo.
Akitoa taarifa ya maendeleo ya ujenzi wa kiwanja hicho mbele ya Waziri huyo wa Miundombinu kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania, Prosper Tesha, Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Ufundi na Uhandisi, White Majula, alisema mkandarasi tayari amemaliza kukata na kujaza udongo njia za kuruka na kutua ndege ambazo waziri alizitembelea na kuzikagua.
"Maeneo yote ya usalama katika njia ya kuruka na kutua ndege yenye urefu wa mita 1,800 tayari mkandarasi ameyakamilisha kwa asilimia 65 na amekamilisha kazi ya ufungaji wa mitambo ya kusaga mawe kwa ajili ya kokoto na ameanza kufunga mtambo wa lami," alisema Majula.
Kwa mujibu wa vyanzo vyetu vya uhakika vya habari, imeelezwa kuwa kampuni hiyo kutoka Falme za Kiarabu tayari imelipwa shilingi bilioni 3.1, ambapo kiwango hicho cha fedha kinajumuisha gharama za kazi za kufanya marejeo ya usanifu wa njia za kuruka na kutua ndege pia usimamizi wa utekelezaji wa ujenzi unaoendelea.
Kandarasi ya kumalizia kazi za ujenzi wa kiwanja hicho cha Songwe ilisainiwa Septemba 12 mwaka 2008 na kukabidhiwa Oktoba 19, mwaka huo huo, inatakiwa kazi hiyo ikamilike kwa kipindi cha miezi 18 kwa gharama ya sh bilioni 32.


CHANZO; Tanzania Daima
 
Amani na utulivu wimbo wa kila siku wa CCM. Hivi niulize CCM wamefanya nini na hii amani? Before CCM tulikuwa na vita au mauaji ya kimbari?. If not why do they always claim something they haven't worked for?. Prof (sijui wa nini) unataja amani na utulivu kama mafanikio katika nchi ambayo haijawahi kupigana vita huo ni ulemavu wa akili mkubwa sana!
Can you imagine kwa miaka 5 mafanikio ya CCM ambayo inaweza kujivunia ni 2 tu. Kapunguza utegemezi, sio kweli (ukweli ni kwamba tumenyimwa misaada baada ya kuona usanii ni mwingi, na licha ya hilo amatembeza sana bakuli), tumejenga uwanja wa ndege wa Songwa amabo si yeye aliyeanzisha huo mradi kaudandia toka kwa Mkapa!
Nina uhakika kabisa kama kungelikuwa na jingine la kujivunia CCM wasingesita kulisema ukweli ni kwamba hakuna!!
 
hivi kwa sasa hivi ni ndege ngapi zina tua kwa siku mbeya? hadi kuhalalisha uwanja huo? hata za cargo tu
na kuhusu bajeti na kujitegemea je ameweka mikopo ya stanbic, barclays? ni vizuri akatupa mchanga nuo wa mapato yetu na matumizi kuhalalisha anacho sema.
angelianza na issue ya dry port ningemuelewa saana
 
Naona bora angekaa kimya tu..kuliko kuanza kuchemka

Ni kweli afadhali angekaa kimya ;huyu bwana hii tabia ya kujikomba komba kwa wana mtandao ameanza lini? If he has decided to join them it is a sign that he has given up his political ambition for the ultimate prize!!
 
Back
Top Bottom