Mwandishi Christopher Gamaina na wenzake watatu waachiwa huru, Walihukumiwa miaka 30 jela

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,812
11,986
Waandishi hao awali walihukumiwa kifungo cha miaka 30 jela kwa kosa la unyang'anyi wa kutumia nguvu na baada ya kukata rufaa Mahakama kuu ya Tanzania kanda ya Ziwa iliamuru kesi hiyo kusikilizwa upya chini ya hakimu mwingine.

Mahakama kuu kanda ya Mwanza leo hii tarehe 20 Disemba 2019 imefuta kesi hii chini ya Kifungu cha 98 cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai ambapo waandishi wa Habari Christopher Gamaina, Wilfred Makuna, Manga Msalaba na Zephania Mandia wapo huru kuanzia sasa.

Vilevile, ufutwaji wa kesi hii ni kufuatia serikali kuonesha kutokua na nia ya kuendelea na kesi hii.

Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania
20 Disemba 2019
1576835376127.png

Pichani chini: Waandishi wawili Christopher Gamaina (kushoto) na Zephania Mandia (kulia) wakiwa wameshikana mikono na Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mwanza, Bw. Edwin Soko (katikati)

Zaidi, soma:


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wajiulize mwenendo wa maisha yao ukoje. Kama hawakuhusika, wamshukuru Mungu. Kama walihusika, wajirekebishe maana kuwa waandishi hakuwaondolei tabia zisizofaa.
 
Justice snatched, justice released. Fabricated cases will never prevail in Tanzania. Shame on Jiwe's lousy regime
 
Hao bila shaka walionekana kuwa ni Anti-Juhudi, ndipo nchi ilipofika.

Tujifunze sana, tuliwashutumu mno akina Amin, Mobutu nk kwa haya haya kumbe "Our food was still cooking in the kitchen".
 
Waandishi hao awali walihukumiwa kifungo cha miaka 30 jela kwa kosa la unyang'anyi wa kutumia nguvu na baada ya kukata rufaa Mahakama kuu ya Tanzania kanda ya Ziwa iliamuru kesi hiyo kusikilizwa upya chini ya hakimu mwingine.

Mahakama kuu kanda ya Mwanza leo hii tarehe 20 Disemba 2019 imefuta kesi hii chini ya Kifungu cha 98 cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai ambapo waandishi wa Habari Christopher Gamaina, Wilfred Makuna, Manga Msalaba na Zephania Mandia wapo huru kuanzia sasa.

Vilevile, ufutwaji wa kesi hii ni kufuatia serikali kuonesha kutokua na nia ya kuendelea na kesi hii.

Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania
20 Disemba 2019
View attachment 1298069
Pichani chini: Waandishi wawili Christopher Gamaina (kushoto) na Zephania Mandia (kulia) wakiwa wameshikana mikono na Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mwanza, Bw. Edwin Soko (katikati)

Zaidi, soma:


Sent using Jamii Forums mobile app

Kwa hiyo ina maana kuwa walisingiziwa mashitaka, jee waliowazulia mashitaka watafikishwa mahakamani?
 
Ilitakiwa wahusika wote waliotumia madaraka yao vibaya kuwabambikia makosa hao waandishi wawajibishwe!

Ila kwa bahati mbaya nchi yetu ina udhaifu mkubwa kwenye kipengele cha kuwajibishana, hivyo mambo yataisha kimya kimya! huku jamaa wakiwa wamepata mateso ya kila aina.
 
Tokea wiki iliyopita Niko Mwanza kwa shughuli zangu. Jana niliposoma thread hii na nilikuwa na mudabwa kutosha sana nikawa interested kuingia machimboni kufuatilia kesi hiyo walao kupata kujua nini hasa kilichojiri?
Nimegundua mambo kadhaa na nikashikwa na butwaa.
1. Mwanza yaweza kuwa ni mkoa wenye waandishi wa habari wengi sana baada ya Dar es salaam pengine ni kutokana na wingi wa vyombo vya habari tulivyo navyo Dar.
2. Mwanza inaweza kushika nafasi ya kwanza nchini kuwa na waandishi wengi wasio na elimu. Yaani wababaishaji na walio jaa unafiki wa kutungiana mambo yasiyo kweli. Mmoja wao apatapo jambo lisilo na chembe yeyote ya ukweli basi wana tengenezeana mbinu za kumalizana hasa kwa kuangalia wealth ya mtu. Hili ni zao la waajiriwa wengi wa StarTv na RFA ambao wengi waliajiriwa makanjanja kwa mfumo wa cheap labour alio uasisi Diallo.
3. Kesi hii inaonyesha kuna kosa lingine la kimaadili lilifanyika ambalo lilistahili onyo la kitaaluma lakini sio mashtaka ya unyanganyi yaliyo tengenezeana na jeshi la Polisi kupitia aliyekuwa RPC aliye ondolewa Sikh zilizo pita.(Hilo nitalizungumza baadae nitakaporudi Mwanza kupata ushahidi).
4. Kuna chama chao cha waandishi kinaitwa MCP, kinaonyesha kina viongozi lakini ni mmoja au wawili tuu wanaojua nini wajibu wao na wajibu wa chama. Wengine wamekalia eitha kusubiri posho au kupiga majungu tuu.
Haiwezekani ndani ya chama hicho kiongozi mmoja atetee mwandishi huku mwingine anaeneza majungu kuhusu mwandishi huyo huyo. (Nitakapo pata majina yao kwa uhakika nirudipo nitayaweka hapa)
Hitimisho;
Nimeweka yote hapa kujaribu kuonyesha kuwa Polisi wanapopata usaidizi wa fitna katika nia zao ovu, wanaweza kuleta madhara makubwa sana kwa jamii. Fikiria hao vijana kupotezwa miaka 30 hali zao na familia zao zingekuwaje? Ni sawa na kuruhusu vivo.
Na kwa hao waandishi wanao shabikia mateso kwa wenzao wanadhani wanaisaidia jamii ya wenzao?
Tukutane baadae ya sikukuu Mwanza
 
Tokea wiki iliyopita Niko Mwanza kwa shughuli zangu. Jana niliposoma thread hii na nilikuwa na mudabwa kutosha sana nikawa interested kuingia machimboni kufuatilia kesi hiyo walao kupata kujua nini hasa kilichojiri?
Nimegundua mambo kadhaa na nikashikwa na butwaa.
1. Mwanza yaweza kuwa ni mkoa wenye waandishi wa habari wengi sana baada ya Dar es salaam pengine ni kutokana na wingi wa vyombo vya habari tulivyo navyo Dar.
2. Mwanza inaweza kushika nafasi ya kwanza nchini kuwa na waandishi wengi wasio na elimu. Yaani wababaishaji na walio jaa unafiki wa kutungiana mambo yasiyo kweli. Mmoja wao apatapo jambo lisilo na chembe yeyote ya ukweli basi wana tengenezeana mbinu za kumalizana hasa kwa kuangalia wealth ya mtu. Hili ni zao la waajiriwa wengi wa StarTv na RFA ambao wengi waliajiriwa makanjanja kwa mfumo wa cheap labour alio uasisi Diallo.
3. Kesi hii inaonyesha kuna kosa lingine la kimaadili lilifanyika ambalo lilistahili onyo la kitaaluma lakini sio mashtaka ya unyanganyi yaliyo tengenezeana na jeshi la Polisi kupitia aliyekuwa RPC aliye ondolewa Sikh zilizo pita.(Hilo nitalizungumza baadae nitakaporudi Mwanza kupata ushahidi).
4. Kuna chama chao cha waandishi kinaitwa MCP, kinaonyesha kina viongozi lakini ni mmoja au wawili tuu wanaojua nini wajibu wao na wajibu wa chama. Wengine wamekalia eitha kusubiri posho au kupiga majungu tuu.
Haiwezekani ndani ya chama hicho kiongozi mmoja atetee mwandishi huku mwingine anaeneza majungu kuhusu mwandishi huyo huyo. (Nitakapo pata majina yao kwa uhakika nirudipo nitayaweka hapa)
Hitimisho;
Nimeweka yote hapa kujaribu kuonyesha kuwa Polisi wanapopata usaidizi wa fitna katika nia zao ovu, wanaweza kuleta madhara makubwa sana kwa jamii. Fikiria hao vijana kupotezwa miaka 30 hali zao na familia zao zingekuwaje? Ni sawa na kuruhusu vivo.
Na kwa hao waandishi wanao shabikia mateso kwa wenzao wanadhani wanaisaidia jamii ya wenzao?
Tukutane baadae ya sikukuu Mwanza

Mkuu usiishie kutuonjesha fanya urudi mapema baada ya sikukuu
 
Back
Top Bottom