Mwanaume mwenye mke mmoja bila mchepuko au mtoto wa nje ya ndoa. Je unapointi gani ya maana na ukusema kwa wanaume wenye watoto nje tukakuelewa?

Mwanaume mwenye mke mmoja bila mchepuko au mtoto wa nje ya ndoa. Je unapointi gani ya maana na ukusema kwa wanaume wenye watoto nje tukakuelewa?

Nikifa MkeWangu Asiolewe

JF-Expert Member
Joined
Feb 26, 2024
Posts
11,250
Reaction score
24,081
Binafisi huwa najiuliza mwanaume unawezaje kutoboa miaka hadi 50 kwenye ndoa huna mtoto nje ya ndoa na hata mchepuko huna yaani niwewe na ulokole wewe na usabato bahati mbaya kabisa unakuta mke wako kashakuambia kuzaa mwisho watoto 3 tu.

Na baada ya hapo kafunga uzazi na wewe bila hila ukalipokea hilo je huwa mnaweza vipi?

Mbaya zaidi kuna wanaume wenzetu hudiriki hadi na wao kufunga uzazi yaani kukatwa mirija yao.

Wanaume aina hii mara zote remote ya familia huwa inamilikiwa na mke wake muda wote.

Ebu tuambie una point gani ya maana ya kutueleza ama kutushauri kwenye kikao cha wanaume tulio zaa nje ya ndoa tukakuelewa na kufuata ushauri wako?

Karibu sana
 
Sio mlengwa wa wito, lakini nikiwa nimetoka njia ya msalaba, nakumbusha tu aliwahi kusema yule baba aliyebarikiwa hekima na maarifa na utajiri kuliko wote Duniani kwamba, Mwisho wa siku yote ni Ubatili mtupu..
 
Epuka kuzalisha michepuko kupunguza migogoro ya mali na mirathi kati ya watoto wako wa nje na wale wa ndani ya ndoa

Watoto hawatakuwa na mshikamano na upendo baada ya kifo chako
 
Sio mlengwa wa wito, lakini nikiwa nimetoka njia ya msalaba, nakumbusha tu aliwahi kusema yule baba aliyebarikiwa hekima na maarifa na utajiri kuliko wote Duniani kwamba, Mwisho wa siku yote ni Ubatili mtupu..
Suleiman alisema yote ni ubatili na kujirisha upepo. Maana yake hakuna jema hapa chini ya jua hakuna !
 
Epuka kuzalisha michepuko kupunguza migogoro ya mali na mirathi kati ya watoto wako wa nje na wale wa ndani ya ndoa

Watoto hawatakuwa na mshikamano na upendo baada ya kifo chako
Kama unaweza kuzalisha nje,unashindwaje kumuandalia mazingira mazuri huyo mtoto wa nje?
Tumeshuhudia hata watoto wa Mama mmoja na baba mmoja wakigombea mali mpaka wanauana baada ya wazazi kutangulia mbele ya Haki.
 
Back
Top Bottom