Mwanaume kuzaa nje ya ndoa

Mwanaume kuzaa nje ya ndoa

Haya mambo wachie wenyewe. Mm kila msichana nikukutana nae anapata mimba waliozaliwa ni 2 aliepo tumboni 1 sas juzi kati nimesema nioe daahh mtihn mgumu nimuoe nani n nwache nanI
Mpendwa hujui kinga?? Njia za kuzuia mimba zipo kibao. Kila siku unajisahau au? Ushajijua wewe ni gusa uvimbe juu, kwa nini usichukue tahadhari? Mnawapa shida watoto mnaowazaa. Mtoto kulelewa na mama yake mzazi ni tofauti kabisa na kulelewa na mama mwingine.

Na wanawake tuache kuwazalia boyfriends. Nyuzi nyingi za namtafuta baba yangu, ni za watoto waliozaliwa nje ya ndoa (kabla hajaoa na za michepuko). Tuwahurumieni watoto wetu
 
Wat if mwanaume aka-regret what he has been doing toka mwanzo, cz alisham-cheat mara nyingi, ila hii ya sasa ndo mpk mtoto. Akaregret na situation ya kuwa mama watatu na watoto watatu, atlast akaamua kwa ridhaa yke amuache huyo mwanamke kwa amani ili huyo mwanamke asiendelee kumchukia maisha yke yote, kwa sababu hili ni bifu la maisha.
 
Kuvunja ndoa sio kutatua tatizo , hivyo cha muhimu ni maelewano ya jinsi ya kumlea huyo mwanao.

Na kama kiwango cha mapenzi hakiwezi kuwa kama mwanzo lazima kitapungua na kinaweza kurudi katika hali ya kawaida kadri ya muda unavyokwenda.
 
Kukuta hata na Watoto sita Ndo tukaoana haina shida kabisa ila tupo wote tena ukaongeze mwingine kwa kweli changamoto

Kubwa inategemea na wewe utakavojieleza na kukiri kosa kuzidisha upendo labda ntakaa ila ndo wale amekosea bado anakuwa mkali tena sijui kwa kweli

Mapenzi yanauma ukisalitiwa sidhani Kama ntakupenda Kama awali

Ukitaka kukaa na mkeo vizuri mfanye akuamini na mtreat vizuri Hivi nkivikosa mweeeee inakuwa mtihani kidogo
Kwa kweli ni bora niolewe tu na single daddy, maana mtoto nimemkuta na nikakubali kwa hiari yangu kuwa ntakuwa mama yake, nikaamua mwenyewe nipende boga na ua lake. Kuliko mtu aniletee mtoto wa nje (mchepuko) ndani ya ndoa. Mungu aniepushe na kikombe hicho, maana heeeeeeeee
 
Mpendwa hujui kinga?? Njia za kuzuia mimba zipo kibao. Kila siku unajisahau au? Ushajijua wewe ni gusa uvimbe juu, kwa nini usichukue tahadhari? Mnawapa shida watoto mnaowazaa. Mtoto kulelewa na mama yake mzazi ni tofauti kabisa na kulelewa na mama mwingine.

Na wanawake tuache kuwazalia boyfriends. Nyuzi nyingi za namtafuta baba yangu, ni za watoto waliozaliwa nje ya ndoa (kabla hajaoa na za michepuko). Tuwahurumieni watoto wetu
Kama wanahitji wenyewe .na kila Mmoja anahitaji nimsaidieJe
 
Haya mambo wachie wenyewe. Mm kila msichana nikukutana nae anapata mimba waliozaliwa ni 2 aliepo tumboni 1 sas juzi kati nimesema nioe daahh mtihn mgumu nimuoe nani n nwache nanI
Hao wawili waliozaliwa na aliyepo tumboni WOTE ni mama tofauti?? I mean kila mmoja na mama yke?
 
Mtu akizaa nje ya ndoa sio bahati mbaya kaamua. Wacha azae awezavyo ila siri zangu hazimuhusu tena namchukulia kawaida maana najua mkiongea kitu nyeti lazima ataeaambia hawara zake! Hivyo ntamuheshimu tu kama mume ila mambo mengi hatutahusiana kuanzia uchumi n.k Hadi kifo kitutenganishe.
 
Habari zenu wakuu,

Naombeni kuuliza, hasa wanawake wanaweza kuwa katika position nzuri sana. Inapotokea mume wako umemkuta na mtoto, ukakubali akakuoa na mkafanikiwa katika ndoa kupata nae mtoto mmoja. Lakini ikatokea huyo mume wako akazaa na binti mwingine tena nje ya ndoa.
1. Utaweza kuendelea na relationship hiyo?
2. Kama utaendelea, je unaweza kuwa na kiwango kile kile cha mapenzi kama mwanzo?
3. Je, unaweza ukatamani kuvunja ndoa ila kwa sababu wewe ni mwanamke ukashindwa? Au utaendelea kwa sababu ya neno "uvumilivu"

Nawasilisha.

Kuendelea inategemea na upendo wako kwake? Na pia je anakudharau? Kama hapana unaweza komaa na ndoa yako as long as unampenda na mnaelewana ila kama hivyo havipo basi we jiondokee aingie ndani huyo mama mtoto .. je dini yako inaruhusu , ndoa za mitala kama ndiyo awe mke mdogo.. mama yangu alikomaa na baba lakini kubwa ili kuwa upendo na mpaka sasa hivi wapo mtoto anasomeshwa aliyezalishwa hana mbele wala nyuma..

Tatizo ndoa zetu hizi za kikristu hazivunjiki hadi kifo. . . Ningevumilia ila upendo na uaminifu kwa mume wangu ungepungua

Ila kama ni uislam taraka fasta

umemkuta na mtoto wa nje ukapotezea akadunga tena nje akaleta tena mtoto mara amedunga tena nje mtoto yaani ni series ww upo tu unavumilia itakuwa una ganzi ama nini??

Mhhhhhh sina experience na hii situation....kwa niliowahi shuhudia walipitia hii hali waliishia kuvunja ndoa zaoo
Nikirudi kukupa ushauri..angalia tuu moyo wako unasemajee jipe muda utafakari kwa umakini pima pande zote mbili za maamuzi yakoo,mshirikishe sana Mungu akupe hekima na busara kwenye maamuzi yako


Kuna muda mwanamke kwa udhaifu wetu kma binadamu, ni ngumu sn kuvumilia. Muda wowote atakapohitajika kuwasiliana na mtoto au kuambiwa shida za mtoto, mwanamke ukijua atakuwa ni kama anatonesha kidonda upya kbs. Kuna muda inawezekana baba akatakiwa kutimiza majukumu fulani nyumban, mathalani fedha au chochote, na atakaposhindwa kutimiza, wazo litakalokuijia kichwani ni kwmb amehudumia sehemu nyingine, hta kma kweli hana. Kiukweli ni rahisi sana kufanya revenge na jamaa akakosa nguvu ya kureact kwani yy ndo mkosefu namba moja

Yaani mtoto wa nje umpate ndani ya ndoa halafu umtambulishe kwa mkeo?

Haiwezekani ng'ombe dume atoke zizini kwako akazae zizi lingine halafu udai ndama wako!

Ni dharau sana kwa mkeo, na familia nzima.
 
Mtu akizaa nje ya ndoa sio bahati mbaya kaamua. Wacha azae awezavyo ila siri zangu hazimuhusu tena namchukulia kawaida maana najua mkiongea kitu nyeti lazima ataeaambia hawara zake! Hivyo ntamuheshimu tu kama mume ila mambo mengi hatutahusiana kuanzia uchumi n.k Hadi kifo kitutenganishe.
Hahaha "Mpaka kifo kiwatenganishe"
 
Yaani mtoto wa nje umpate ndani ya ndoa halafu umtambulishe kwa mkeo?

Haiwezekani ng'ombe dume atoke zizini kwako akazae zizi lingine halafu udai ndama wako!

Ni dharau sana kwa mkeo, na familia nzima.
Solution yaweza kuwa nini, maana tayar mke kwa kutumia intelijensia yake ameshagundua.
 
Back
Top Bottom