Mwanaume kimbia

Anatuvuruga mkuu
 
Kwani hata wanasikia. Nilikuwa naye wakati anapitia kipindi kigumu sana hata hela ya kula ilikuwa shida. Kafanikiwa kakata mawasiliano na karudi kwa mwanamke aliyemkimbia wakati hana kitu. Huyo mwanamke alikuwa naye wakati mambo super, alipoona jamaa hela imekata akawa hana habari naye. Haya ndio maisha
 
Kila mbuzi ale kwa urefu wa kamba yake, kila mmoja wetu atabeba mzigo wake mwenyewe. Kuoa zama hizi ni adhabu ya kujitakia.
Naam nikweli kabisa nimeshuhudia hayo , kuwa mwanaume halafu ukaoa ni Moja ya adhabu 1 kubwa Sana
 
Ndugu acha kabisaa watoto ni kitu kingine aiseee! Ni dhamana aliotupa Mungu haijalishi nitapita wapi niwaaache.
Haujajibu hoja , Swali --- ukifa hao watoto wataishi katika mazingira gani ,
Ukifungwa jela hao watoto wata hudumiwa na Nani ,!?

Binafsi nilitegemea utoe majibu ya hayo maswali
 
Haujajibu hoja , Swali --- ukifa hao watoto wataishi katika mazingira gani ,
Ukifungwa jela hao watoto wata hudumiwa na Nani ,!?

Binafsi nilitegemea utoe majibu ya hayo maswali
Swala la kufa na kufungwa hiyo ni dharura ilio nje ya uwezo, automatically hapo sita kuwa nimekimbia bali dharura ilio nje ya uwezo imetokea.

Lakini hali nina macho, mikono , miguu, nguvu na maarifa kitu kama hicho hapana aisee!

Na hata kama hivyo havitakuwepo bado haitoshi kuwa sababu ya kukimbia ndugu yangu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…