Teh Teh
Zinduna umenifanya nicheke sana na hii thread yako na umenikumbusha mbali sana..na umenikumbusha hasira nilizo zipata baada yakukumbana na hiyo hasa namba nne!
Muda mwingine sisi wanaume huwa tuna kosea sana tena sana maana huwa tunaamini mwanamke hawezi kukukubali au kukupenda bila kuwepo na hisi za mapenzi ndani yake kumbe sivyo!Na yanayo tudanganya zaidi ni matendo na hisia wanazo onesha muda mwingine zinazo tupelekea tuzichanganye na hisia za mapenzi!
Na kumbuka ilikuwa 2008 kuna binti alitokea kunizoea sana na ilikuwa haiwezi kupita siku bila kunitafuta au kuonana tukapiga story na muda mwingine alikuwa hadi aniletea zawadi na ikifika muda wa chakula cha mchana ananishitua tukale..na uwezi amini mimi mwanzo nilimchukulia kama rafiki wa kawaida kabisa..lakini baadhi ya watu walifikiri nina uhusiano nae.
Huyu binti ilikuwa hawezi kulala kabla hatujaongea au kuchati na kutakiana usiku mwema na alikuwa anaonekana mwenye furaha sana hadi marafiki zake wakawa wanasema huyu lazima umuoe kabisa hapo hata sitamtongoza hata sikuwa na fikiri kufanya hivyo maana nilimuona kama rafiki tuu!
Baadae nilianza kupata hisia za kutaka kumtongoza na nilipata msukumo zaidi kutoka kwa marafiki zangu wakiniambia hatuamini kama huna uhusiano na fulani...na anavyo onekana anakupenda ...acha uongo wewe..haiwezekani..daaa
Baadae nilifikiria nikasema lazima nifunguke sasa na haitakuwa shida maana ni wazi ana nipenda kabisa kwanza ataanzie wapi kukataa? niliangalia mazingira yote nikaona hayampi nafasi kukataa kabisa na haiwezekani!
Sasa kwakuwa ulikuwa ndio mwezi wa Valentine nilisema nitaitumia siku hiyo kumsprise na kumfungukia...nilikwenda dukani nikanunua card,mau na zawadi ya pochi..nikavianda vizuri hii ilikuwa siku tano kabla ya Valentine(nilifanya maandalizi mapema sikujua yatakayo nikuta)
Ilipo baki siku moja kabla ya tukio nikamtumia sms kuwa leo jioni nataka tuka kae sehemu tupige story..akasema "poa tena nitakuwa wa kwanza kufika utanikuta" daa nilifurahi sana na nikajisemea moyoni daa tayari nimepewa ushindi wa mezani.
Ulipo fika muda nilia andaa zawadi zangu nilijongea eneo la tukio na kuanza kunywa soda.. baada ya dakika ishirini alifika na kukaa ..cha kwanza akaniambia "Siamini hujaniletea zawadi nika mwambia usiwe na wasi wasi... nikashika kifurushi nika mkabidhi akachunguliaa akacheka akasema nimezipenda lakini nitaziangalia baadae asante...daaa..nikasema nisichelewe nikaanza kufunguka..duuu nikamweleza kila kitu...
Niliishiwa nguvu alipo niambia ruttashobolwa samahani kakaangu mimi "nilikuwa na kuheshimu na nitakuheshimu na upendo nilio nao kwako ni wadada na kaka tuu na sikutegemea kama tutafika huku na siwezi kabisa maana kweli wewe ni muhimu kwangu lakini si jinsi ulivyo fikiri...na zawadi zako siwezi kuzichukua maana haitakuwa fair..samahani naomba niende" nilijaribu kubembeleza wapi ndio kwanza alibadilika na kuchukia na sikuwai kuona amechukia kiasi kile..aliondoka na kuniachia zawadi zangu duuu..niliishiwa nguvu kabisa na kumbuka pale bar nilikuja kuondoka saa 5 na huwezi amini urafiki ulikufa na akabadili namba kabisa....sikuamini kilicho nitokea na ilikuwa funzo kwangu....
Hakuna kazi iliyo ngumu kama kujua mwanamke anataka nini...kwakweli nilipatwa hasira sana na aibu juu