toplemon
JF-Expert Member
- Mar 26, 2017
- 4,581
- 4,631
Mwanaume aliyezoea mapenzi kinyume na maumbile atakua radhi kutembea hata na wanaume wenzake
Mzuka humu ndani?
Basi leo nakuja hili jambo na kwanza samahanini sana kwa ambao mtakwazika na hii mada ila ndo uhalisia wa mambo ulivyo.
Ni hivi katika mahusiano kati ya mume na mke au boyfriend na girlfriend, kunaweza ikatokea mwanaume anapenda kufanya mapenzi kinyume na maumbile (anal sex), na wengine wanawaforce wake zao, na hata wengine tabia hizo na hiyo michezo wanayo sasa linakuja suala la kufanya ambapo anaweza kufanya girlfriend wake au mke wake kwa kumforce au kumlazimisha.
Mwanaume wa aina hii siku akichoka au akikukinai na akikosa kabisa huo mchezo atakua radhi hata atembee na wanaume wenzake yaani mashoga au hata wengine wanafanya matendo ya ajabu ajabu. Unasikia kesi za ulawiti wa watoto na ndugu michezo inayoendelea majumbani inashika kasi kwa sababu ya matendo kama haya.
Anaweza akawa anataka kitu kama hicho wewe kama mkewe au girlfriend wake ukamgomea, basi ujue huyo atakua radhi hata akatembee na wanaume wenzake tu ili aridhishe haja zake. Ninayo mifano ya cases nyingi za mambo ya aina hii.
Ushauri bure kwa kina dada na kina mama: Msikubali kutendewa hiki kitendo wala msikubali kuwa na mpenzi anayeku-force kufanya hayo au kukuomba, achana naye. Na kama ni mchumba anakuomba huo mchezo mkatalie tu maana ukikubali ujuwe hatokaa akuoe au kukuoa ni muhali.
Mimi nawaonea huruma kina dada na kina mama ambao haya mambo hawayapendi na unakuta sio mdau kabisa sasa kufundishwa hii michezo sio jambo jema kabisa.Tujifunze kuwaheshimu wanawake tuepuke kusambaza huu mchezo kwani wasiokua na hatia ndo wanaumia