Mwanasheria wa NEMC akamatwa na TAKUKURU..

Mwanasheria wa NEMC akamatwa na TAKUKURU..

beth

JF-Expert Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
3,881
Reaction score
6,377
DRQE3FzX0AAjQWG.jpg


Naona Takukuru ya sasa imenoa meno!

Mwanasheria wa Baraza la Taifa la Hifadhi ya Mazingira(NEMC), Bernard Kongola na Polisi wawili wa kituo cha Mbweni wanashikiliwa na TAKUKURU kwa mada ya kuomba Rushwa ya Shilingi milioni 1 kutoka kwa Mkalimani binafsi wa Kiwanda cha Yong Long Plastic Co. Ltd

Watu wa vitengo amkeni, acheni michezo ya Rushwa. Nyakati zime-change!
 
Mbona Ngosha ajakamatwa hivi takukuru kwanini mko biased kiasi hicho. ? Sadists at work.
 
DRQE3FzX0AAjQWG.jpg


Naona Takukuru ya sasa imenoa meno!

Mwanasheria wa Baraza la Taifa la Hifadhi ya Mazingira(NEMC), Bernard Kongola na Polisi wawili wa kituo cha Mbweni wanashikiliwa na TAKUKURU kwa mada ya kuomba Rushwa ya Shilingi milioni 1 kutoka kwa Mkalimani binafsi wa Kiwanda cha Yong Long Plastic Co. Ltd

Watu wa vitengo amkeni, acheni michezo ya Rushwa. Nyakati zime-change!
Nawaona wanafiki tuu kuna watu hawawakamati hata wangepeana rushwa mbele ua ofisa mkuu wa TAKUKURU tena nadhan ndio atawamba mbinu mzuri zaid ya kupeana rushwa mchezo huu wa TAKUKURU kujifanya wanafanya kazi wanao weza kushikwa masikio ni wajinga tuu
 
Nawaona wanafiki tuu kuna watu hawawakamati hata wangepeana rushwa mbele ua ofisa mkuu wa TAKUKURU tena nadhan ndio atawamba mbinu mzuri zaid ya kupeana rushwa mchezo huu wa TAKUKURU kujifanya wanafanya kazi wanao weza kushikwa masikio ni wajinga tuu
Uongozi siyo kitu kidogo nyie, msijidai kuwa skeptical tu kila wakati. Nendeni mgombea basi ili mje mtufanyie hayo mnayojidai kukosoa kosoa. Viongozi wetu ni watu kama wengine so hata awe nani, hawezi kusimamia kwa ubora kila jambo kwa namna inayokupendeza.
Tuwa-judge kwa vitendo vyao but zaidi kwa dhamira zao. Tumekuwa na watangulizi wa JPM wote tuliona walivyokuwa wazito kwenye rushwa, amekuja huyu, sasa ndio tunajidai kumnyooshea kidole wakati yeye wenyewe ndo kaanzisha kampeni hiyo huku sisi ukiwa hatuamini kama atasimamia kwa mafanikio kama anavyofanya. Inawezekana Wewe ni mmojawapo wa walioathirika na kampeni za Mzilankende, hilo ni kosa lako, acha rushwa.
 
Walikuwa wanatafuta hela ya bia hao

Ova
 
hiyo sio pesa ya kiwi ya viatu kweli?
 
Kukamata hata polisi angeweza, Takukuru ya nini nchi masikini hii?!Yani nchi ndoogo na masikiniii lakini serikali kuubwa bila sababu. Takukuru ivunjwe kukamata, kupeleleza na kufungua mashitaka ibaki kuwa kazi ya polisi tu. Hawa takukuru ni mzigo tu kwa walipa kodi. Unaunda taasisi kuubwa kazi zake ni zilezile za kipolisi. Rushwa haiishi wala haipungui kwanini wawepo?! Majeshi meengi halafu tunalia hatuendelei. Tutaendeleaje kwa kujiingiza gharama zisizo za lazima hivi?! Ondoa takukuru tubaki kama zamani.
 
Takokuru acheni hizo. Hawa trafiki wa gerezani wanachukua kila dereva wa daladala kila siku kwa daladala za Temeke na gongo la mboto sh 5000 mnakula nao. Leo mhasibu kaomba chai tu mnajitangaza. Acheni double standards
 
Mwanasheria msomi Njaa huyo ....rushwa ya Mln1 inamtoa nishai

Ova
 
Vyuma vimekaza kweli... Mwanasheria mzima wa NEMC unaomba rushwa 1 M.. na atasulubiwa ili ajifunze..
 
Back
Top Bottom