Mwanasheria mpya Zanzibar hataki kurudi nchini

Mwanasheria mpya Zanzibar hataki kurudi nchini

Mwiba

JF-Expert Member
Joined
Oct 23, 2007
Posts
7,607
Reaction score
1,760
Habari nilizogusiwa juu juu tu ,kumbe Dr Shein amemteua Mwanasheria Mkuu Mpya wakati mwanasheria huyo hayupo nchini ,yupo majuu na huenda alijiripua huko japo alikuwa ni chini ya Mwanasheria alieondoshwa ,alikimbia mapema baada ya kuona kuna mtikisiko katika bunge la Katiba na haswa baada ya Othman kukacha kuhudhuria.
Hizo ni tetesi tu kuwa jamaa hayupo nchini na hakuna tamaa ya kurudi tena Zanzibar ,ila kama kuna mwenye uhakika kuwa yupo si vibaya akanisahihisha.
 
Duh!!! kumbe hilo likitabu kwa upande wa zanzibar limepokelewa bila uwepo wa mwanasheria wa huko?
 
Kuludi ndio nini? Akh, hata sitaki kusoma. Mwatia kichefuchefu na Kiswahili chenu cha
 
Mwaka 1964 wakati Tanganyika inaimeza Zanzibar mwanasheria mkuu wa Zanzibar Dourado alitimuliwa, mwaka 1984 wakati Tanganyika inataka kuimiliki Zanzibar , Rais wa Zanzibar Jumbe alifukuzwa, mwaka 1988 wakati Tanganyika ikishona koti lake waziri Kiongozi Seif Shariff Hamad alifukuzwa , mwaka 2014 wakati Tanganyika ikishona kanzu ya Muungano badala ya koti mwanasheria mkuu wa Zanzibar Othman Masoud amefukuzwa kazi ......tarakuri ......
 
Mwaka 1964 wakati Tanganyika inaimeza Zanzibar mwanasheria mkuu wa Zanzibar Dourado alitimuliwa, mwaka 1984 wakati Tanganyika inataka kuimiliki Zanzibar , Rais wa Zanzibar Jumbe alifukuzwa, mwaka 1988 wakati Tanganyika ikishona koti lake waziri Kiongozi Seif Shariff Hamad alifukuzwa , mwaka 2014 wakati Tanganyika ikishona kanzu ya Muungano badala ya koti mwanasheria mkuu wa Zanzibar Othman Masoud amefukuzwa kazi ......tarakuri ......

mmmh! Kisa ni Muungano..... naona dalili za ndala kutoboka... siku wakiinama kuzivua ili wazishone msumari wa inchi 6 utawaingia kunako we ngoja waendelee kuwatimua.....
 
Atamuapisha kwa njia ya nukushi ni shidaaa tu naona majanga kweli kweli hawa ccm
 
Taarifa ipo juujuu tuu, mtoa taarifa inaelekea nae ni walewale wenye nia ya kumuombea mtu mabaya tuu kwa maslahi binafsi.

We unajua huko nje kafuata nini? nani kakwambia hatorudi.
Asiporudi kwani atakosekana mtu wa sheria kujaza hiyo nafasi?

WACHA UNAFIQ
 
Ni kweli Mwanasheria aliyechaguliwa hayupo nchini na yupo Ujerumani yapata wiki moja sasa lakini kihistoria huyu jamaa ni kada wa Chama chao naamini atarudi tuu
 
Huyo mwanasheria lazima atakuwa kada mwenzao. Kwa hiyo ameteuliwa kulinda maslahi ya ccm na sio ya zanzibar.
 
Back
Top Bottom