simplemind
JF-Expert Member
- Apr 10, 2009
- 16,409
- 9,183
Hatimaye, Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa atua Chadema baada ya kukubaliana rasmi katika kikao cha Kamati Kuu ya chama hicho kilichomalizika saa 8 usiku kuamkia leo.
Kamati Kuu ya CHADEMA, ilikutana jana katika kikao cha dharura kwenye hoteli ya Bahari Beach, Kunduchi Dar es Salaam, na kufikia uamuzi wa kumpokea Lowassa.
Atatangazwa rasmi kesho Jumanne, Bahari Beach Hotel Dar es Salaam kwa tukio ambalo litarushwa live na ITV, saa 10 jioni. Mamia ya watanzania watashuhudia kupitia kwenye tv zao.
Lowassa alikuwa miongoni mwa wanaCCM 38, waliyotia nia kugombea urais wa Tanzania kwa mwenvuli wa chama hicho. Alikatwa katika hatua ya awali na Kamati ya Maadili ya CCM.
Aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar na kutimuliwa baada ya Bunge la Katiba, Othman Masoud ametajwa kuwa Mgombea Mwenza wa Edward Lowassa.
Mwanasheria huyo aliyebobea ndani ya taaluma hiyo, kesho atachukua kadi ya CHADEMA na kuwa mwanachama kamili ili kuweza kukidhi taratibu, kanuni na sharia za Tanzania za mfumo wa vyama vingi na za uchaguzi.
Aidha, kuna tetesi kuwa Othman Masoud, anaandaliwa kuwa mgombea urais kwa mwaka 2020 ama kwa nafasi ya Muungano au Zanzibar.
Othman Masoud ni Mwanasheria wa Kwanza kujitokeza wazi wazi kuitetea Zanzibar, bila kutanguliza maslahi yake. Othman Masoud kwa sasa si mwanachama wa chama chochote cha siasa..
Kamati Kuu ya CHADEMA, ilikutana jana katika kikao cha dharura kwenye hoteli ya Bahari Beach, Kunduchi Dar es Salaam, na kufikia uamuzi wa kumpokea Lowassa.
Atatangazwa rasmi kesho Jumanne, Bahari Beach Hotel Dar es Salaam kwa tukio ambalo litarushwa live na ITV, saa 10 jioni. Mamia ya watanzania watashuhudia kupitia kwenye tv zao.
Lowassa alikuwa miongoni mwa wanaCCM 38, waliyotia nia kugombea urais wa Tanzania kwa mwenvuli wa chama hicho. Alikatwa katika hatua ya awali na Kamati ya Maadili ya CCM.
Aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar na kutimuliwa baada ya Bunge la Katiba, Othman Masoud ametajwa kuwa Mgombea Mwenza wa Edward Lowassa.
Mwanasheria huyo aliyebobea ndani ya taaluma hiyo, kesho atachukua kadi ya CHADEMA na kuwa mwanachama kamili ili kuweza kukidhi taratibu, kanuni na sharia za Tanzania za mfumo wa vyama vingi na za uchaguzi.
Aidha, kuna tetesi kuwa Othman Masoud, anaandaliwa kuwa mgombea urais kwa mwaka 2020 ama kwa nafasi ya Muungano au Zanzibar.
Othman Masoud ni Mwanasheria wa Kwanza kujitokeza wazi wazi kuitetea Zanzibar, bila kutanguliza maslahi yake. Othman Masoud kwa sasa si mwanachama wa chama chochote cha siasa..