Ndugu yangu Kibo 10 na kubaliana nawewe kwamba Mawaziri wengi ni wakaidi na hawapendi Ushauri wa Kisheria hasa kwenye Mawizara kwani wamekuwa wakiona ushauri huo mara nyingi umekuwa ukienda kinyume na Matarajio yao. Lakini vile vile kuna jambo kubwa la kikatiba limetokea hapa ambalo tuliangalie wote kwa makini;
1: " Hawa Mawakili wa Serikali waliokuwa katika operesheni hiyo,DPP(MKURUGENZI WA MASHTAKA) ATATAKIWA KUTOA MAELEZO,HAO MAWAKILI WAKE WALIKWENDA HUKO KWA MISINGI GANI PAMOJA NA MAHAKIMU WALIOKUWA HUKO:Natumaini watatueleza na kufafanua yafuatayo:
1. Nani alikuwa akiwalipa posho kwa kipindi chote walichokuwa huko?
2.Je kuna mashtaka yeyote waliyo yafungua kama sehemu ya kuwako kwao katika Taskforce hiyo?
3.Je katika uendeshaji wao au uwepo wao katika Kamati kumeathiri vipi Misingi ya Haki asilia " PRINCIPLE OF NATURAL JUSTICE, Kwamba;Mtu asiwe Hakimu,Mpelelezi na Mwendesha mashtaka yeye mwenyewe KATIKA SHAURI HILOHILO na pia mtu hawezi kuwa Hakimu katika Jmabo linalo Muhusu kitaalamu wanazungumza kama
"NEMO JUDES IN CAUSA SUE "
4. Je hao Mahakimu waliteuliwa kuingia katika Kamati hizo kwa misingi gani? Jaji Mkuu aliidhinisha?je walikuwa wanakazi gani haswa katika Kikosi kazi hicho?
Msingi wa Pili ni Hoja ya Mheshimiwa Jaji Mstaafu ,Thomas Mihayo kwamba itumike sheria ya Kutafiti sababu ya Vifo. na dhani hapa anazungumzia The Inquest Act Sura ya 21 iliyorejewa mwaka 2002 ....Kimsingi sheria hii ipo na ninzuri kabisa na hata ingetumika kutafuta sababu na wahusika wa vifo kama vilivyotokea Morogopro,Soweto Arusha na Nyololo Iringa ingekuwa Rahisi sana na Sijui kwanini wanasheria na wadau wa Haki za Binadamu hawapendi kuitumia labda wana wasiwasi na uwezo wa Mahakimu.
Na Uzuri wa Sheria hii ni kwamba anybody can move the Corona`s Court " Ili kuchunguza Kifo chochote chenye Utata.Hii ni kwa mujibu wa
kifungu cha 12(1) ambacho kinaeleza kwamba
When any body is found ,or a person has died,in circumstances which make the holding of an inquest necessary or desirable,the person finding the body or becoming aware of the death shall as soon as practicable inform the Coroner,or a police officer or any appropriate authority and upon receiving that information the police officer or the appropriate authority shall notify a coroner having jurisdiction to hold an inquest.
Katika mazingira yanayozunguka Tukio hili , Tume ya Kimahakama siyo chaguo sahihi wala Inquest Act haita toa suluhisho sahihi la tatizo hili kwani hapa tayari Mahakama Imeguswa na lazima Mahakimu walioingia huko waliteuliwa kwa mujibu wa taratibu za Kiutawala za Mahakama kwahiyo Mahakama tayari inakuwa "subjudice" Mahakama nayo ni mtuhumiwa tayari wa vitendo hivyo.
Iwapo ningeulizwa ushauri basi kwa maoni yangu ningependekeza iundwe Tume huru na Rais nje ya mfumo wa sasa wa vyombo vya utawala itakayoundwa na Majaji wastaafu na ikiwezekana Majaji wawili kutoka Nje ya Tanzania katiaka nchi mojawapo mwanachama wa Jumuiya ya Madola ili waweze kuchunguza na watoe maoni yao iwapo kunawatu wanatakiwa kuchukuliwa hatua zaidi za kisheria mbali na hatua za kiutawala kama kufukuzwa kazi au kujiuzuru.