ecolizer baba
Member
- Sep 29, 2010
- 88
- 310
Imekuwa fasheni siku hizi kwa watu mbalimbali kuwabeza wabunge wa Bunge hili la Kumi linaloendelea na mkutano wake wa nne, mjini Dodoma. Fasheni hiyo ilianza taratibu wiki kadhaa zilizopita wakati Spika, Anne Makinda aliposema kwamba heshima ya Bunge ilikuwa imeanza kupotea kutokana na mijadala mikali aliyosema ilikuwa inaligeuza Bunge kuwa kama Kariakoo.
Baada ya kauli hiyo ya Spika, watu kadhaa, wakiwamo baadhi ya wabunge wa chama tawala na viongozi wengine ambao ni wafuasi wa chama hicho walitoa kauli mbalimbali na kunukuliwa na vyombo vya habari wakirudia kauli ya Spika kwamba mijadala na minyukano mikali ya hoja inayoendelea bungeni imepoteza hadhi ya Bunge na kuharibu taswira ya chombo hicho cha kutunga sheria.
Lakini kwa upande mwingine, wabunge na wafuasi wa vyama vya upinzani walipinga msimamo wa Spika na baadhi ya wafuasi wa chama chake na kusema kwamba, hali hiyo ni kielelezo kizuri cha kushamiri kwa demokrasia ya vyama vingi katika nchi yetu na kuimarika kwa uhuru wa wabunge kutoa mawazo yao pasipo kufungwa midomo kinyume na ilivyokuwa wakati wa Bunge la chama kimoja.
Hata hivyo, pamoja na ufafanuzi huo, kejeli zimeendelea kuelekezwa kwa wabunge wa Kambi ya Upinzani, hasa wa Chadema na NCCR na baadhi ya wabunge wa chama tawala ambao wakati mwingine wamekuwa wakiikosoa Serikali bungeni, kwamba wabunge hao wanafanya mambo ya kitoto ambayo hawakutumwa na wananchi.
Sisi tunadhani kwamba madai ya kupungua kwa nidhamu ya wabunge na hadhi ya Bunge siyo ya kweli. Tunadhani madai hayo yanatolewa na watu wanaoshindwa kuimudu kasi ya Bunge la Kumi ambalo lina wabunge wengi vijana na wasomi ambao wanahoji mambo ya msingi ambayo huko nyuma yalikuwa yanafichwa chini ya zulia kwa lengo la kutetea serikali iliyo madarakani badala ya kuisimamia na kuiwajibisha pale ilipokosea.
Inawezekana kwamba upo udhaifu wa hapa na pale kwa baadhi ya wabunge kuvunja kanuni hii au ile kwa makusudi au vinginevyo. Tunachopinga hapa ni madai ya jumlajumla yanayoelekezwa kwa wabunge, hasa wa Kambi ya Upinzani kwamba wanapotoa hoja au kuuliza maswali magumu yanayoibana Serikali wanalidhalilisha Bunge. Mfano ni pale wabunge wanapokatazwa kumuuliza Waziri Mkuu maswali ya hapo kwa hapo ambayo siyo ya kisera, eti kwa sababu maswali hayo yanahitaji muda mrefu wa kufanyiwa utafiti.
Kwa hiyo, lazima tukiri kwamba wengi wa wabunge wa Kambi ya Upinzani katika Bunge hili la Kumi ni wabunge makini, ingawa Bunge la Tisa lililokuwa chini ya Spika Samwel Sitta ndilo lilikuwa anzilishi la mijadala mikali kutokana na kiongozi huyo kusimamia vyema kanuni za Bunge na kutoa haki sawa kwa wabunge wote bila upendeleo . Yaliyompata Spika Sitta sasa ni historia, lakini ni vyema tu tukasema kwamba kiongozi huyo alirudisha imani ya wananchi kwa Bunge.
Tunachokiona katika Bunge la Kumi ni juhudi za makusudi au vinginevyo za uongozi wa Bunge kupunguza kasi ya uhuru wa wabunge wa kuhoji na kuiwajibisha Serikali. Kambi ya Upinzani katika Bunge hili imeimarika maradufu na wabunge wake vijana wameonekana kujizatiti kwa kusoma na kuzielewa Kanuni za Bunge na kutoa hoja za msingi ambazo mara nyingi zinapingwa na kuzimwa na wabunge wa upande wa pili kwa kutumia wingi wao bungeni.
Hali hiyo imeleta hofu kwa sababu wananchi sasa wanaiona mijadala hiyo katika luninga na wanafuatilia na kuguswa sana na mijadala hiyo yenye msisimko mkubwa. Hili ni Bunge la hoja, siyo la staha au la kuendeleza dhana ya kulindana. Ni Bunge lenye vijana wenye uwezo wa kuchambua miswada inayoletwa bungeni. Ni kwa sababu hiyo wananchi wamefurahia hali hiyo ambapo Bunge siyo tena mhuri wa kupitisha mambo ya Serikali pasipo kuhoji. Ndiyo maana tunasema hili ndilo Bunge ambalo wananchi wanalitaka.
Baada ya kauli hiyo ya Spika, watu kadhaa, wakiwamo baadhi ya wabunge wa chama tawala na viongozi wengine ambao ni wafuasi wa chama hicho walitoa kauli mbalimbali na kunukuliwa na vyombo vya habari wakirudia kauli ya Spika kwamba mijadala na minyukano mikali ya hoja inayoendelea bungeni imepoteza hadhi ya Bunge na kuharibu taswira ya chombo hicho cha kutunga sheria.
Lakini kwa upande mwingine, wabunge na wafuasi wa vyama vya upinzani walipinga msimamo wa Spika na baadhi ya wafuasi wa chama chake na kusema kwamba, hali hiyo ni kielelezo kizuri cha kushamiri kwa demokrasia ya vyama vingi katika nchi yetu na kuimarika kwa uhuru wa wabunge kutoa mawazo yao pasipo kufungwa midomo kinyume na ilivyokuwa wakati wa Bunge la chama kimoja.
Hata hivyo, pamoja na ufafanuzi huo, kejeli zimeendelea kuelekezwa kwa wabunge wa Kambi ya Upinzani, hasa wa Chadema na NCCR na baadhi ya wabunge wa chama tawala ambao wakati mwingine wamekuwa wakiikosoa Serikali bungeni, kwamba wabunge hao wanafanya mambo ya kitoto ambayo hawakutumwa na wananchi.
Sisi tunadhani kwamba madai ya kupungua kwa nidhamu ya wabunge na hadhi ya Bunge siyo ya kweli. Tunadhani madai hayo yanatolewa na watu wanaoshindwa kuimudu kasi ya Bunge la Kumi ambalo lina wabunge wengi vijana na wasomi ambao wanahoji mambo ya msingi ambayo huko nyuma yalikuwa yanafichwa chini ya zulia kwa lengo la kutetea serikali iliyo madarakani badala ya kuisimamia na kuiwajibisha pale ilipokosea.
Inawezekana kwamba upo udhaifu wa hapa na pale kwa baadhi ya wabunge kuvunja kanuni hii au ile kwa makusudi au vinginevyo. Tunachopinga hapa ni madai ya jumlajumla yanayoelekezwa kwa wabunge, hasa wa Kambi ya Upinzani kwamba wanapotoa hoja au kuuliza maswali magumu yanayoibana Serikali wanalidhalilisha Bunge. Mfano ni pale wabunge wanapokatazwa kumuuliza Waziri Mkuu maswali ya hapo kwa hapo ambayo siyo ya kisera, eti kwa sababu maswali hayo yanahitaji muda mrefu wa kufanyiwa utafiti.
Kwa hiyo, lazima tukiri kwamba wengi wa wabunge wa Kambi ya Upinzani katika Bunge hili la Kumi ni wabunge makini, ingawa Bunge la Tisa lililokuwa chini ya Spika Samwel Sitta ndilo lilikuwa anzilishi la mijadala mikali kutokana na kiongozi huyo kusimamia vyema kanuni za Bunge na kutoa haki sawa kwa wabunge wote bila upendeleo . Yaliyompata Spika Sitta sasa ni historia, lakini ni vyema tu tukasema kwamba kiongozi huyo alirudisha imani ya wananchi kwa Bunge.
Tunachokiona katika Bunge la Kumi ni juhudi za makusudi au vinginevyo za uongozi wa Bunge kupunguza kasi ya uhuru wa wabunge wa kuhoji na kuiwajibisha Serikali. Kambi ya Upinzani katika Bunge hili imeimarika maradufu na wabunge wake vijana wameonekana kujizatiti kwa kusoma na kuzielewa Kanuni za Bunge na kutoa hoja za msingi ambazo mara nyingi zinapingwa na kuzimwa na wabunge wa upande wa pili kwa kutumia wingi wao bungeni.
Hali hiyo imeleta hofu kwa sababu wananchi sasa wanaiona mijadala hiyo katika luninga na wanafuatilia na kuguswa sana na mijadala hiyo yenye msisimko mkubwa. Hili ni Bunge la hoja, siyo la staha au la kuendeleza dhana ya kulindana. Ni Bunge lenye vijana wenye uwezo wa kuchambua miswada inayoletwa bungeni. Ni kwa sababu hiyo wananchi wamefurahia hali hiyo ambapo Bunge siyo tena mhuri wa kupitisha mambo ya Serikali pasipo kuhoji. Ndiyo maana tunasema hili ndilo Bunge ambalo wananchi wanalitaka.