GE2025 Mwananchi: Kigoma ina wasomi wengi lakini Bodaboda

GE2025 Mwananchi: Kigoma ina wasomi wengi lakini Bodaboda

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

DuaZaMama

JF-Expert Member
Joined
Jun 2, 2025
Posts
1,882
Reaction score
4,129
Madereva bodaboda wanaofanya shughuli zao katika eneo la Ujiji, Kigoma, wamelalamikia changamoto ya mikataba inayowakabili, ikiwemo kulazimika kurejesha Sh10,000 kila siku kwa muda wa miezi 18, hali inayokuwa ngumu zaidi wanapopata ajali na kushindwa kuendelea na kazi.

Wakizungumza na mgombea ubunge jimbo la Kigoma Mjini kupitia ACT Wazalendo, Zitto Kabwe, walimwomba awawezeshe kupata pikipiki zenye mikopo nafuu ili kuinuka kiuchumi.

Akijibu hoja hizo, Zitto ameahidi kushughulikia changamoto hizo pindi atakapochaguliwa, akibainisha kuwa sekta ya bodaboda ni miongoni mwa zinazogusa maisha ya vijana wengi na inahitaji mikakati ya kweli ya kuondoa kero za kimaisha.​
 
Madereva bodaboda wanaofanya shughuli zao katika eneo la Ujiji, Kigoma, wamelalamikia changamoto ya mikataba inayowakabili, ikiwemo kulazimika kurejesha Sh10,000 kila siku kwa muda wa miezi 18, hali inayokuwa ngumu zaidi wanapopata ajali na kushindwa kuendelea na kazi.

Wakizungumza na mgombea ubunge jimbo la Kigoma Mjini kupitia ACT Wazalendo, Zitto Kabwe, walimwomba awawezeshe kupata pikipiki zenye mikopo nafuu ili kuinuka kiuchumi.

Akijibu hoja hizo, Zitto ameahidi kushughulikia changamoto hizo pindi atakapochaguliwa, akibainisha kuwa sekta ya bodaboda ni miongoni mwa zinazogusa maisha ya vijana wengi na inahitaji mikakati ya kweli ya kuondoa kero za kimaisha.​
Aiseee !! halafu watoto wa viongozi wanachezea mabilioni na mamilioni ya pesa Huku watoto wa Maskini waliosoma kwa shida wanaendesha bodaboda.!!
 
Kigoma ina raana ya usaliti usimwamini mtu kutoka kigoma utajuta
 
Back
Top Bottom