Ethel Chisono Edwards, anayefahamika mtandaoni kama One Boss Lady, amehukumiwa na mahakama ya Lusaka baada ya kukiri kosa la kuchapisha maneno ya kumdhalilisha Rais Hakainde Hichilema. Hukumu yake imekuja licha ya hatua ya rais huyo mwaka 2021 kufuta sheria ya makosa ya kumkashifu rais — mabadiliko yaliyopongezwa na Wazambia wengi kama maendeleo katika kukuza uhuru wa kiraia
Edwards amehukumiwa chini ya Sheria za Usalama wa Mtandao na Makosa ya Mtandao, ambazo zilianza kutumika baada ya kufutwa kwa adhabu ya kumkashifu rais. Kesi hiyo imeibua mjadala mkali miongoni mwa vijana na watumiaji wa mitandao, ambao wanaona kuwa sheria hizo mpya zinakinzana na haki za kikatiba za kujieleza
Edwards amehukumiwa chini ya Sheria za Usalama wa Mtandao na Makosa ya Mtandao, ambazo zilianza kutumika baada ya kufutwa kwa adhabu ya kumkashifu rais. Kesi hiyo imeibua mjadala mkali miongoni mwa vijana na watumiaji wa mitandao, ambao wanaona kuwa sheria hizo mpya zinakinzana na haki za kikatiba za kujieleza