Mwanamke wangu ana HIV, wazazi wanataka nimuoe

Mkare_wenu

JF-Expert Member
Mar 11, 2011
1,714
442
Nina na mahusiano na mwanamke mmoja ambaye anaishi mtaa wa jirani ambapo tumedumu kwenye mahusiano kwa takribani mwaka mmoja na nusu, baada ya kuwa nae kwa miezi kadhaa tukatokea kuaminiana na kuanza kusex bila mpira, akawa amepata mimba na nilikuwa nimeplan akishazaa tuanze kuishi pamoja kwavile nilikuwa nampenda na nilihisi ni mtu sahihi anayefaa kuwa mkewangu, na ndugu wengi walikuwa wameshamfahamu.

Bahati mbaya ni kwamba kipindi tunaanza mahusiano hatukuwahi kuzungumza kuhusu kupima HIV, sasa baada ya yeye kupata mimba nilikuwa najua siku akianza kwenda clinic ni lazima ataniambia twende wote, kwa maana sikuhizi ndivyo clinic wanavyotaka, sasa nilianza kupatwa na wasiwasi baada ya kuona mwenzangu hadi mimba inafikia miezi 6 hakuna siku aliyowahi kuniambia habari hiyo na ananiambiaga anaenda clinic, nikahisi kuna kitu ananificha. Kwavile huwa sipendi kukaa na wasiwasi ikabidi siku1 nijitutumue niende kupima mwenyewe kimyakimya bila kumshirikisha, nashukuru Mungu results zikawa Negative, ila bado nilikuwa na wasiwasi naye hivyo ikabidi nijaribu kumdodosa kupitia msg za simu kama ifuatavyo;

Mimi: Clinic sikuhizi hawapimi HIV?
Yeye: Wanapima, mimi walinipima niko fiti

Mimi: Hongera, je hawakukuuliza mwenza maana nnavyojua sikuhizi wanataka muwe wote
Yeye: Kuuliza lazima, tena siku ya kwanza nilipoenda walinifukuza kabisa na kuniambia nije na mwenzangu, Ila nilipoenda siku ya pili na kusema mwenzangu yuko bize sana na kazi hawezi kupata muda wa kuja ndio wakanikubalia wakanipima pekeyangu

Mimi: Kwanini ulilazimika kutunga uongo huo? Je mimi nina ubize wa namna hiyo? Na kwanini hukunipa hata hiyo taarifa ili hata kama nikikataa walau unakuwa umetimiza wajibu wako?
Yeye: Sikutaka kukusumbua tu

Baada ya charts hizo nilikubali kwa shingo upande, ila bado sikumuamini. Siku moja nikamuomba twende tukapime wote, akatoa sababu za kitoto ilimradi tu asiende na kunilaumu ni kwanini simuamini. Hapo akilini ikanijia kabisa kwamba zile hisia zangu zinaweza kuwa sahihi. Nilichofanya ni kugoma kushiriki naye tendo la ndoa hadi atakapokuwa tayari kufanya hivyo. Tukakaa miezi mitatu bila sex hadi alipojifungua. Baada ya kujifungua wazazi walinishauri nianze kuishi naye ili tulee mtoto pamoja, nikawaomba wanipe muda ndani ya miezi miwili nitafanya hivyo.

Siku moja nilikuwa nimelala naye baada ya kujifungua nikambana kisawasawa kwamba ukweli ni upi kwanini hutaki tukapime kama unajiamini uko sawa? Akaniambia ukipima wewe utapata majibu, nikamweleza sisi tumeshakuwa mwili mmoja hivyo ni muhimu kilamtu ajue majibu ya mwenzake na si lazima majibu yafanane. Ukapita ukimya mrefu baada ya muda akaniuliza, je unataka kujua ukweli? Nikamjibu yes, akaniambia 'mimi ni mgonjwa', baada ya kuniambia hivyo sikuonesha kustuka, nikamwabia tu nashukuru kwa kunipa ukweli. Siku hiyohiyo palipokucha kwakuwa ilikuwa imeshapita miezi mitatu nikaenda kucheck tena kwa mara ya pili, namshukuru Mungu kwa 'miujiza' yake nilikutwa negative tena.

NJIAPANDA niliyonayo hapa ni kwamba zile ndoto zangu za kuja kuwa mke wangu ndo zimefail hapa kwakuwa naamini bila sex hakuna ndoa. Je nitawaeleza vipi wazazi wanielewe kuhusu kutomuoa huyu mwanamke wakati niliwaahidi hivyo? Nitumie maneno yepi yatayofanya wazazi kunielewa pasipo kuanika ukweli wa huyu mzazi mwenzangu kuwa mwathirika? Ushauri wenu ni muhimu sana kwa maana muda niliowaahidi wazazi unaelekea kufika kikomo huku hadi sasa sijajua la kuwaambia...
 
USHUHUDA WANGU KUHUSU H.I.V (kwa ufupi):

Hilo suala la mwanamke wangu kusema ana HIV halikunistua/ kunishangaza sana, kwakuwa nilishawahi kukutana na kisa cha namna hiyo kwa mwanamke mwingine miaka kama minne iliyopita, in short yeye nilikuwa nishakuwa naye kwenye mahusiano kama miezi 8 hivi, baada ya 'kuraruana' kavu kwa muda mrefu yeye mwenyewe aliniomba twende tukacheck afya maana tulipanga tutakuja kuoana, tulipima ila majibu yaliyokuja hakuna aliyeamini, yeye alionekana anao mimi nikaonekana sina.

Kesho yake tukaamkia hospital ya serikali, nao wakatupima mara 2 zote majibu yakaonekana hivyohivyo. Kwahiyo plan zetu za kuja kuoana zikafia pale, na mimi nikaja kuchek tena pekeyangu baada ya miezi 3 majibu yakawa hivyohivyo negative, sitaki kuwa kama Deception anayetuaminisha kwamba UKIMWI haupo, mimi nnaamini upo, ila ni Mungu tu ameamua kunifanyia miujiza.
 
USHUHUDA WANGU KUHUSU H.I.V (kwa ufupi):

Hilo suala la mwanamke wangu kusema ana HIV halikunistua/ kunishangaza sana, kwakuwa nilishawahi kukutana na kisa cha namna hiyo kwa mwanamke mwingine miaka kama minne iliyopita, in short yeye nilikuwa nishakuwa naye kwenye mahusiano kama miezi 8 hivi, baada ya 'kuraruana' kavu kwa muda mrefu yeye mwenyewe aliniomba twende tukacheck afya maana tulipanga tutakuja kuoana, tulipima ila majibu yaliyokuja hakuna aliyeamini, yeye alionekana anao mimi nikaonekana sina. Kesho yake tukaamkia hospital ya serikali, nao wakatupima mara 2 zote majibu yakaonekana hivyohivyo. Kwahiyo plan zetu za kuja kuoana zikafia pale, na mimi nikaja kuchek tena pekeyangu baada ya miezi 6 majibu yakawa hivyohivyo negative, sitaki kuwa kama Deception anayetuaminisha kwamba UKIMWI haupo, mimi nnaamini upo, ila ni Mungu tu ameamua kunifanyia miujiza.
Sio muujiza, nasikia mchawi group la damu. Kuna case kama hiyo yako naifahamu
 
Kuishi na mpenzi/mke mwenye ukimwi inataka moyo sana. Kama inatokea akiwa tayari ni mke basi hakuna jinsi bali ni kuendelea kuishi naye. Na namna alivyoupata kaupataje? Kama kapuyanga nje basi hakuna ndoa tena hapo.

Ina maana we Bak ukikutana na situation kama hiyo unapiga chini?
Kwani si kuna njia za kujikinga?
 
Mimi naona Fanya kuufuata moyo wako.
Kama unampenda bado baada ya kukudanganya na kukuibia kipindi chote hicho anajijua sio mzima na akakukubalia na papuchi akakupa akajua kabisa yeye si mzima na alichokuwa anafanya ni kujaribu kukuambukiza na wewe vile hakuwa hata na huruma. Kama bado unampenda oa.
Kama haumpendi wazazi wasikukoseshe amani, ni makosa ya huyo mwanamke, angepaswa akuambie hali yake kabla ili ujue unaendelea kuwa nae au lah.

Aisee UKIMWI ni habari nyingine.
 
Kuishi na mpenzi/mke mwenye ukimwi inataka moyo sana. Kama inatokea akiwa tayari ni mke basi hakuna jinsi bali ni kuendelea kuishi naye. Na namna alivyoupata kaupataje? Kama kapuyanga nje basi hakuna ndoa tena hapo.
Sio kila Ukimwi ulipatikana kwa zinaa. Imagine hakupuyanga...
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
khe khe khe khe Depal unajua hiyo kitu inaweza ikakauka na utelezi wote ukapotea hapo ndiyo unasikia msuguano wa nyama kwa nyama kavu ambao husababisha K kuvimba na hata kuchubuka.😜😜😜

Mnaweza kusex kavu pia lakini kwa kuhakikisha hamna michubuko kutokea.

Unahakikisha tu ameloa mpaka.....
 
khe khe khe khe Depal unajua hiyo kitu inaweza ikakauka na utelezi wote ukapotea hapo ndiyo unasikia msuguano wa nyama kwa nyama kavu ambao husababisha K kuvimba na hata kuchubuka.😜😜😜
Usikamie sana, slowly but sure ukame unatokeaje sasa!! 😆
 
Back
Top Bottom