Baada ya kumpenda yule dada alieniacha baada kwenda kusoma mwanza Hakika niliteseka sana,Jinamizi la huyu mwanadada lilinitesa saana kiasi kwamba nikitizama nje darasani kipindi hiko nilikuwa kama namuona!
Ubaya zaidi ni kwamba ukiwa katika mapenzi mazito na mtu hata kama hakupendi huezi amini kama hakupendi kweli!
kweli mwanadada uliniacha katika kipindi kigumu katika maisha yangu...ukanifanya Nisipende tena wala kumuamini Mwanamke....Nikaangua katika Janga la UplayBoy!
Nilikuwa na imani ipo siku nitampata ambaye tutapendana...ikachuku muda sikupenda mwanamke ata we mzuri kiasi gani...nikabakia kuplay tu!
Lakini Mungu si Athumani...Amenipatia mwanadada! Mzuri ambaye automaticaly tumeendana ghafla japo mwanzoni nilimtongoza kimasihara tu...Ghafla siku Nenda rudi nikaangukia katika wimbi la Mahaba na huyu Mwnadada..! Hakika sikuamini!
Imefikia mtoto wa kikee ananiletea msosi Gheto...ananipikiaa mimi..Hajisikii na title ya kwao kwamba ni mtoto wa Kishuaa!, tukiwa kitandani hanibanii..ananipa ninavyotakaa!
Nakushukuru sana Mwenyezi Mungu pamoja na wewe Mwanadada, Hakika kwa Mapenzi yako umeniaminisha na Kubadili Mtizamo wangu kuhusu wanawake!...umeniaminisha kwamba Good women still exists...umeniamisha kwamba wanawake wenye mapenzi ya dhati bado wapo saana....labda huenda wanaume hatuwaoni!
Najua Hauwezi ona nachokiandika hapa ila mimi nimekupa moyo wangu na sio unafiki! Mwishowe Mwenyezi Mungu akipenda utakuwa Mama wa Watoto wangu!...Mapenzi yake Mwenyezi Mungu Yatimizwe!