NIMPENDENANI
JF-Expert Member
- Nov 2, 2014
- 6,114
- 5,397
Habari wana MMU,
Kuna jambo linanitatiza,Jana amekuja wifi yangu mke wa kaka na kilio nikajua amefiwa kumuliza haya kumezidi nini? Anasema anataka kuachwa amesha choka na kuona SMS kwenye simu ya mumewe za mapenzi na hivi karibuni aliona msg na picha za mtoto kwenye simu ya mumewe akafatilia mpaka akajua kama mumewe ana mtoto mwengine.
Sasa amehama nyumba na anataka talaka yake, hapo alipo yeye ni mkubwa kuliko bro, ameolewa mwanzo ana watoto wawili na akazaa watatu na bro. Nilichomwambia astahimili alee watoto wake. Hakuna ndoa yenye raha moja kwa moja leo tamu kesho chungu
Na istoshe watoto wake anasomeshewa, maisha sio mabaya anayoishi tatizo la mumewe ajitahidi kumuomba mwenyezi mungu atatulia, anasema moyo wake hauchukui tena anataka talaka yake na watoto wake wawili kawachukua lakini mmoja karudi anasema anataka kuishi na ndugu zake.
Nimemwambia wifi anipe muda bro amesafiri akirejea nitaongea nae lakini ameshikilia talaka. Bro amesema talaka sio tatizo atampa aseme jengine. Lakini waungwana mie sitaki waachane sababu watoto watapata tabu, mama wa wifi nae nimeongea nae kanichamba utadhani mie ndio nilomuoa mwanawe sasa hapa nimebakia njia ya panda hata lakumwambia akanielewa sinaaaa.
Naomba mnisaidie mawazo ili hawa watoto waishi na wazazi wao kwa salama na amani.
Kuna jambo linanitatiza,Jana amekuja wifi yangu mke wa kaka na kilio nikajua amefiwa kumuliza haya kumezidi nini? Anasema anataka kuachwa amesha choka na kuona SMS kwenye simu ya mumewe za mapenzi na hivi karibuni aliona msg na picha za mtoto kwenye simu ya mumewe akafatilia mpaka akajua kama mumewe ana mtoto mwengine.
Sasa amehama nyumba na anataka talaka yake, hapo alipo yeye ni mkubwa kuliko bro, ameolewa mwanzo ana watoto wawili na akazaa watatu na bro. Nilichomwambia astahimili alee watoto wake. Hakuna ndoa yenye raha moja kwa moja leo tamu kesho chungu
Na istoshe watoto wake anasomeshewa, maisha sio mabaya anayoishi tatizo la mumewe ajitahidi kumuomba mwenyezi mungu atatulia, anasema moyo wake hauchukui tena anataka talaka yake na watoto wake wawili kawachukua lakini mmoja karudi anasema anataka kuishi na ndugu zake.
Nimemwambia wifi anipe muda bro amesafiri akirejea nitaongea nae lakini ameshikilia talaka. Bro amesema talaka sio tatizo atampa aseme jengine. Lakini waungwana mie sitaki waachane sababu watoto watapata tabu, mama wa wifi nae nimeongea nae kanichamba utadhani mie ndio nilomuoa mwanawe sasa hapa nimebakia njia ya panda hata lakumwambia akanielewa sinaaaa.
Naomba mnisaidie mawazo ili hawa watoto waishi na wazazi wao kwa salama na amani.