Mwanamke, ilinde ndoa yako! Kupinduana kupo sana tu...

Mtambuzi

Platinum Member
Oct 29, 2008
8,806
15,379
Unapoishi nyumbani na ndugu yako, jamaa yako au hata mtumishi wa kike, ni vizuri ukajitahidi kulinda ndoa yako. Kumbuka kwamba, wanaume hawajali hisia, hujali zaidi mwili. Kama ukimwachia ndugu yako, jamaa au rafiki yako kumzoea sana mumeo, jua tu kwamba, inawezekana unajitengenezea maumivu makubwa sana hapo baadae.

Tafiti zinathibitisha sana kwamba, mwanaume anapohisi kuwa mwanamke fulani anamwonesha kwamba, yeye ni mwanaume kweli kweli, anapoonesha kwamba, anatambua uwepo wake na mchango wake katika familia, mwanaume huanza kumpenda, bila kujali sura au hadhi.

Kama ndugu yako ni mjuaji wa mambo haya, anaweza kumwonesha mumeo kwamba, anaamini kuwa ni mwanaume kwelikweli. Hii hufanyika kwa kumsifu, kutopingana naye, kumpongeza mara kwa mara na kumwonesha kwamba anaamini katika yeye.

Hata wale watumishi wa ndani, wanaochukuliwa na wanaume za watu hawafanyi hivyo kwa sababu, ati hao watumishi ni wazuri sana wa sura au wanajua sana mapenzi, hapana.

Wanaume huwachukua kwa sababu, wake au wapenzi wa wanaume hao wameshindwa wajibu wao, wameshindwa kujua kwamba wanaume hutazama uhusiano kwa jicho tofauti.

Lakini, iwe ndugu au jamaa zenu na hata watumishi majumbani mwenu, bado na wao ni binadamu, wana udhaifu. Kwa udhaifu wao, pamoja na udhaifu wa wanaume au wapenzi wenu, wanaweza kuwasaliti. Kwa hiyo ni juu yenu kulinda ndoa zenu, ili udhaifu huo usiwe chanzo kwa kuvunjika kwa matumaini na matarajio yenu ya kujenga familia.

Kuna mambo mawili makubwa hapa, kwanza inawezwekana mmejiachia wazi sana kama wanawake na kusahau kuwa wanaume huvutiwa na mambo gani.
Kwa hali hiyo, mnawaacha wale walio karibu nao kuwafanyia yale wanayohitaji na kuchukua nafasi zenu.

Lakini pili, ni udhaifu wa kibinadamu na zaidi kwa wanaume, linapokuja suala la mwili. Kwa udhaifu huo, inabidi muwasaidie kuwalinda wasishawishiwe kirahisi. Lakini, ndugu zenu wa kike au watumishi mnaoishi nao, inabidi muwakague vizuri na kuacha kuwamini kupita kiasi kwa waume au wapenzi wenu.

Ni hatari sana kwa mwanamke kwa mfano, kumwambia au kumruhusu mumewe aende sehemu za starehe na rafiki yake wa kike au na ndugu yake wa kike, ati kwa sababu anamwamini rafiki huyo au mumewe. Kumbuka, suala hapa sio kuaminika au kutoaminika, bali ukweli wa kimaumbile pia. Mwanamke, chunga ndoa yako, ilinde sana, kwani sio dhambi.
 
Kama utakuwa humwamini mme wako kiasi hicho, yeye kwa nini akuamini? Mtaishi kwa kutoaminiana katika ndoa mpaka lini???
 
Hii thread ni kwa ajili ya wanawake kwa ajili ya kuchunga waume zao? Not the other way around? Au the other way around hakunaga shida? Anyway, just passing!
 
Bullshit!
Why is always a woman's responsibility kichunga ndoa? Why not man's, after all nani alimchumbia mwenzie, akabother kujipendekeza, kutoa mahali, kugharamia a very expensive wedding etc! Whose loss will be if ndoa ikivunjika? A man will have to incur the same shit allover again plus taking care of the children!
 
Asante kwa hii post, nimeipenda nikaicut na kuipaste ili nimtumie wife, lakini nikasita nisije kumletea problem tx wetu, asante ujumbe umenifikia.
 
Tafiti zinathibitisha sana kwamba, mwanaume anapohisi kuwa mwanamke fulani anamwonesha kwamba, yeye ni mwanaume kweli kweli, anapoonesha kwamba, anatambua uwepo wake na mchango wake katika familia, mwanaume huanza kumpenda, bila kujali sura au hadhi.

.

Hio paragraph nilo bakisha ndio hua natoa basis kua mwanamke anaweza kabisa mbadilisha mwanaume aelekee ndani ya nyumba (thou not always) for at the end of the day waume zetu wanataka uwaoneshe na wajue una m-appreciate, unajali uwepo wake, unajali mahitaji yake na kwamba wamthamini... End result ni kua anaweza ndio asikupende.... lakini hatasikia neno lolote baya juu yako, au kutoa maamuzi yoyote mabaya juu yako maaana yule mwelewa anajua kabisa kua hio amani anapata hapo sio guranteed toka kwa wanawake wooote...
 
Hio paragraph nilo bakisha ndio hua natoa basis kua mwanamke anaweza kabisa mbadilisha mwanaume aelekee ndani ya nyumba (thou not always) for at the end of the day waume zetu wanataka uwaoneshe na wajue una m-appreciate, unajali uwepo wake, unajali mahitaji yake na kwamba wamthamini... End result ni kua anaweza ndio asikupende.... lakini hatasikia neno lolote baya juu yako, au kutoa maamuzi yoyote mabaya juu yako maaana yule mwelewa anajua kabisa kua hio amani anapata hapo sio guranteed toka kwa wanawake wooote...
Hakuna kitu ambacho wanaume wengi kinawakera kama akiwa anajali na kutekeleza wajibu wake kama mume/bf lakini bado kunakuwa na lack of appreciation! Hapo mwanaume anavunjika sana moyo na inakuwa rahisi sana kuishia kwengine
 
Unapoishi nyumbani na ndugu yako, jamaa yako au hata mtumishi wa kike, ni vizuri ukajitahidi kulinda ndoa yako. Kumbuka kwamba, wanaume hawajali hisia, hujali zaidi mwili. Kama ukimwachia ndugu yako, jamaa au rafiki yako kumzoea sana mumeo, jua tu kwamba, inawezekana unajitengenezea maumivu makubwa sana hapo baadae.

Tafiti zinathibitisha sana kwamba, mwanaume anapohisi kuwa mwanamke fulani anamwonesha kwamba, yeye ni mwanaume kweli kweli, anapoonesha kwamba, anatambua uwepo wake na mchango wake katika familia, mwanaume huanza kumpenda, bila kujali sura au hadhi.

Kama ndugu yako ni mjuaji wa mambo haya, anaweza kumwonesha mumeo kwamba, anaamini kuwa ni mwanaume kwelikweli. Hii hufanyika kwa kumsifu, kutopingana naye, kumpongeza mara kwa mara na kumwonesha kwamba anaamini katika yeye.

Hata wale watumishi wa ndani, wanaochukuliwa na wanaume za watu hawafanyi hivyo kwa sababu, ati hao watumishi ni wazuri sana wa sura au wanajua sana mapenzi, hapana.

Wanaume huwachukua kwa sababu, wake au wapenzi wa wanaume hao wameshindwa wajibu wao, wameshindwa kujua kwamba wanaume hutazama uhusiano kwa jicho tofauti.

Lakini, iwe ndugu au jamaa zenu na hata watumishi majumbani mwenu, bado na wao ni binadamu, wana udhaifu. Kwa udhaifu wao, pamoja na udhaifu wa wanaume au wapenzi wenu, wanaweza kuwasaliti. Kwa hiyo ni juu yenu kulinda ndoa zenu, ili udhaifu huo usiwe chanzo kwa kuvunjika kwa matumaini na matarajio yenu ya kujenga familia.

Kuna mambo mawili makubwa hapa, kwanza inawezwekana mmejiachia wazi sana kama wanawake na kusahau kuwa wanaume huvutiwa na mambo gani.
Kwa hali hiyo, mnawaacha wale walio karibu nao kuwafanyia yale wanayohitaji na kuchukua nafasi zenu.

Lakini pili, ni udhaifu wa kibinadamu na zaidi kwa wanaume, linapokuja suala la mwili. Kwa udhaifu huo, inabidi muwasaidie kuwalinda wasishawishiwe kirahisi. Lakini, ndugu zenu wa kike au watumishi mnaoishi nao, inabidi muwakague vizuri na kuacha kuwamini kupita kiasi kwa waume au wapenzi wenu.

Ni hatari sana kwa mwanamke kwa mfano, kumwambia au kumruhusu mumewe aende sehemu za starehe na rafiki yake wa kike au na ndugu yake wa kike, ati kwa sababu anamwamini rafiki huyo au mumewe. Kumbuka, suala hapa sio kuaminika au kutoaminika, bali ukweli wa kimaumbile pia. Mwanamke, chunga ndoa yako, ilinde sana, kwani sio dhambi.

Mkuu naona hapa hii story inafanana sana na ile drama ya governor Arnold Schazneggerkuishia kuwa na affair na kumzalisha yule house maid wake na ndoa kuvunjika
 
Hakuna kitu ambacho wanaume wengi kinawakera kama akiwa anajali na kutekeleza wajibu wake kama mume/bf lakini bado kunakuwa na lack of appreciation! Hapo mwanaume anavunjika sana moyo na inakuwa rahisi sana kuishia kwengine


Na vice versa Sherrif... hata wanawake tunajisikia hivo pia.. thou tunajikaza in most cases... Sema maamuzi ya mwisho ndio tumetofautiana... mwingine anaachia ngazi mapema.. wengine unashindwa for unaua dhahiri waweza ruka mkojo na ukakanyaga kinyesi.. you try your best... ikishindikana then unasepa... thou it is the worst option ever katika relationships...
 
Mapenzi ya dhati yameenda wapi siku hizi? Kama kweli unampenda mwenzio na yeye anakupenda, je ni kwa nini kuwe na lapses kama hizo eti oooh sijui mume katembea na house maid, ama mke kakumbushia old flame?
Inasikitisha sana morals hakuna kabisa siku hizi hata kwa waliofunga pingu za maisha!
 
Hio paragraph nilo bakisha ndio hua natoa basis kua mwanamke anaweza kabisa mbadilisha mwanaume aelekee ndani ya nyumba (thou not always) for at the end of the day waume zetu wanataka uwaoneshe na wajue una m-appreciate, unajali uwepo wake, unajali mahitaji yake na kwamba wamthamini... End result ni kua anaweza ndio asikupende.... lakini hatasikia neno lolote baya juu yako, au kutoa maamuzi yoyote mabaya juu yako maaana yule mwelewa anajua kabisa kua hio amani anapata hapo sio guranteed toka kwa wanawake wooote...
kweli kabisa Adi, mana tukishaona tunathaminiwa basi hata rungu linapunguza fujo, linakua linataka mtu maalum tu na kwa muda maalum.
 
wanawake wa kizazi mbona mna wakati mgumu? Hata kuilinda ndoa ni jukumu lenu, siku c nyingi nyie ndo mtakua vichwa vya familia!
 
Mapenzi ya dhati yameenda wapi siku hizi? Kama kweli unampenda mwenzio na yeye anakupenda, je ni kwa nini kuwe na lapses kama hizo eti oooh sijui mume katembea na house maid, ama mke kakumbushia old flame?
Inasikitisha sana morals hakuna kabisa siku hizi hata kwa waliofunga pingu za maisha!

Sherrif, mapenzi ya dhati yapo, tena sana, lakini kuna wakati wanandoa au wapenzi hujisahau na kuwaachia watu wngine majukumu ambayo yalitakiwa yafanywe na wao, na si kwa wanawake tu hata wanaume pia. kunakuwa na kujisahau kwingi na ndio maana ndoa ikivunjika, husemwa kwamba wote mmechangia, ina maana kuna mmoja wa wandoa aliuona udhaifu kwa mwenzie na kuamua kuufumbia macho au kulalamika kwa ndugu, jamaa au marafki zake. hiyo haisaidii, sana sana inachangia kuipeleka ndoa shimoni.
 
Life is not about finding the right person, but creating the right relationship, it's not how we care in the beginning, but how much we care till the very end.
 
umejitahidi kumpotray mwanaume ni kiumbe dhaifu,ukweli ni kwamba mwanaume ni mwenye nguvu zaidi na ana uwezo sana wa kucontrol hisia zake....we both men and women have equal rensponsibilities kufanya kila jitihada ndoa zetu zidumu sio jukumu la mwanamke pekee kama unavyotaka kutuaminisha hapa.
 
umejitahidi kumpotray mwanaume ni kiumbe dhaifu,ukweli ni kwamba mwanaume ni mwenye nguvu zaidi na ana uwezo sana wa kucontrol hisia zake....we both men and women have equal rensponsibilities kufanya kila jitihada ndoa zetu zidumu sio jukumu la mwanamke pekee kama unavyotaka kutuaminisha hapa.

Ann Marie, Siwezi kukubishia kwa sababu huo ndio mtazamo wako.......lakini kama wewe ni msomaji mzuri wa mada za mahusiano zinazowekwa humu utagundua kuwa kuna malalamiko mengi ya wanawake juu ya kusalitiwa kwa ndoa au mahusiano yao. Nimezungumzia hisia kwa sababu hisia za wanawake na za wanaume katika swala zima la mapenzi zinatofautiana. Kama si mila na desturi zetu ambazo zinamsisitiza mwanamke kuwa yeye ndiye anayewajibika kulinda ndoa kwa kiasi kikubwa swala la kukithiri kwa talaka au kutengana lingekuwepo tangu kale. lakini wazazi wetu waliliona swala la talaka kama udhaifu kwa mwanamke na sio kwa mwanaume. muingiliano wa tamaduni umesababisha kwa kiasi kikubwa kuongezeka kwa swala zima la talaka. hiyo ni kutokana na mabadiliko ya kiuchumi. kile tulichokuwa tukiita mke ni mama wa nyumbani hakipo tena, mke ni lazima achangie pato la familia, na ndio maana kuna mahitaji ya kuwa na mfanyakazi wa nyumbani tunaita House Girl au ndugu wa kike ambaye anaweza kuchukuliwa kwa ajili ya kusaidia kazi za nyumbani... Tatizo huja wapi......? Rejea makala yangu ukisoma between line utanielewa.........
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom