Mwanamke Hata Umpe Mwanaume Kila Kitu

Mwanamke Hata Umpe Mwanaume Kila Kitu

Companero

Platinum Member
Joined
Jul 12, 2008
Posts
5,609
Reaction score
1,734
Hata umpende vipi. Na hata umsifie sana. Tena hata umpikie vyakula vitamu na vinono. Au umnunulie zawadi nzuri nzuri. Vile vile umsaidie kimaisha na kimawazo. Umuimbie nyimbo tamu pia. Siri zako zote za moyoni hali kadhalika umweleze. Walio wako nao wamkubali.

Ila ukimnyima kitu kimoja tu. Yaani kimoja tu atanyong'onyea wee. Kama samaki nje ya maji atatapatapa. Mwanawane hatatulia mpaka apate hicho ulichomnyima. Popote pale atakitafuta - huku, pale na kule. Lo akishakipata rijali atatulia tuli kama maji kwenye mtungi.
 
teh! ni hiki ninachofikiria mie au akili yangu inanidanganya!!!!!!
eti ni nini hicho?
 
Kuna mchezo mpya wa kuruka ukuta
 
Hata umpende vipi. Na hata umsifie sana. Tena hata umpikie vyakula vitamu na vinono. Au umnunulie zawadi nzuri nzuri. Vile vile umsaidie kimaisha na kimawazo. Umuimbie nyimbo tamu pia. Siri zako zote za moyoni hali kadhalika umweleze. Walio wako nao wamkubali.

Ila ukimnyima kitu kimoja tu. Yaani kimoja tu atanyong'onyea wee. Kama samaki nje ya maji atatapatapa. Mwanawane hatatulia mpaka apate hicho ulichomnyima. Popote pale atakitafuta - huku, pale na kule. Lo akishakipata rijali atatulia tuli kama maji kwenye mtungi.
Nawe pia utakuwa na matatizo!!! kwa nn umpe kila kitu........... kasoro hicho tu!!?
 
Napita, salamu kwenu nyote

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Companero nasubiri jibu ili nikampe hicho kilichobaki sio uchungulie hapo chini unanichelewesha!!!!
 
Last edited by a moderator:
Mh! Dada mbona unaongea mambo nusu nusu? Sidhani kama kuna ukweli katika hoja yako, unless hicho unacho mnyima sasa mlikubaliana before, wakati mpo kwenye meza ya duara mkipitia terms na conditions!
 
Back
Top Bottom