Mwanamke baada ya kuzaa nae watoto anakua ndugu yako au wale watoto ndio ndugu zako???...

mojoki

JF-Expert Member
Oct 21, 2010
1,314
290
... kuna mwanamke mmoja nilikua naongea nae tena ye ni mke wa mtu (ni kawaida yangu kuwa na mazoea na wake za watu japo kwa nia njema)...and katika stori stori za hapa na pale nikamwambia, 'me i think unapofunga ndoa na mwanamke kisha mkazaa watoto, basi mnakua ndugu kabisa, kwa maana ya kwamba uwepo wa watoto wale umechangiwa nanyi wawili (under assumption kwamba hao watoto ni wa ndani ya ndoa), na wao kwa kuwepo kwao kwafanya nyinyi kuwa zaidi ya mke na mume...

Kwamba hata kama mtakoseana vp lakini kuna undugu kati yenu ambao umesababishwa na uwepo wa wale watoto...

Well ye alinijibu kwamba 'wacha kujidanganya wale watoto ndo ndugu zako yule mwanamke sio ndugu yako hata siku moja...'nikajiuliza ye ana mume na ana watoto watatu how come anasema hivi (tena ukizingatia anaupinga upande wake)...

Sikutaka kubishana coz kwanza sijaoa sina mke wala uzoefu na hayo mambo...halafu pia nikasema yawezekana mawazo yangu ya ki bilogoia haya apply kwenye real life...lakini hata hivyo sikuridhika na majibu yake kutokana na uhusiano wa moja kwa moja ninaouona baada ya mke na mume kupata watoto...

Sasa enyi wana JF mliooa, mlioolewa na hata mabachelor kama mimi mnaweza liongelea vp hili suala...

Naombeni tafadhali mtatue utata...
 
anasababu yake ya kusema hivo, mi najua kama mume wako ni ndugu yako sababu unamwita baba yeke baba, na ndugu zake shemeji, na huo ni undugu tayari. ukija kuongeza na vya watoto ndio kabisaaa, maana hata mkiachana (God forbid) wakwe zago bado ni ndugu, na watoto watatembelea kote.
Mi naona wewe ndio ulisema sawa, ila kuna exception, kama huyo mama.
 
Hivi undugu sio lazima muwe mmechangia damu kwa namna fulani? Mtu na kaka yake, mtu na shangazi, baba mdogo, kaka, dada, mtoto etc, mi nadhani mkiona mnakuwa karibu na mkizaa mnakuwa karibu zaidi, ni bora kusema mnakuwa mwili mmoja ( Kama isemavyo biblia) ila bado haitoshi kusema mmekuwa ndugu, huyo mama alikuwa sawa
 
Duuh kweli kuna utata hapa, ila ni kweli kusema mnakuwa ndugu. Lakn likija swala lakuachana tena duuh undugu haupo tena.
 
Hivi undugu sio lazima muwe mmechangia damu kwa namna fulani? Mtu na kaka yake, mtu na shangazi, baba mdogo, kaka, dada, mtoto etc, mi nadhani mkiona mnakuwa karibu na mkizaa mnakuwa karibu zaidi, ni bora kusema mnakuwa mwili mmoja ( Kama isemavyo biblia) ila bado haitoshi kusema mmekuwa ndugu, huyo mama alikuwa sawa

sasa hapo nimkubamba mkuu tukienda kihesabu zaidi kama mtoto wako ni ndugu yako kwa vile mmechangia damu na pia huyo huyo mtoto ni ndugu wa mkeo kwa vile amechangia nae damu then wewe na mkeo ni ndugu...i.e. Kama A=B na B=C then bila shaka wala doubt A=C
 
Duuh kweli kuna utata hapa, ila ni kweli kusema mnakuwa ndugu. Lakn likija swala lakuachana tena duuh undugu haupo tena.

kwani undugu huwa unavunjika mkuu?...undugu upo pale pale either mmeachana au mmechuniana
 
Hivi undugu sio lazima muwe mmechangia damu kwa namna fulani? Mtu na kaka yake, mtu na shangazi, baba mdogo, kaka, dada, mtoto etc, mi nadhani mkiona mnakuwa karibu na mkizaa mnakuwa karibu zaidi, ni bora kusema mnakuwa mwili mmoja ( Kama isemavyo biblia) ila bado haitoshi kusema mmekuwa ndugu, huyo mama alikuwa sawa
Ni ndugu yako bwana! Au unaogopa ukisema ni ndugu atakunyima?
 
Back
Top Bottom