Interlacustrine R
JF-Expert Member
- Jan 22, 2022
- 5,971
- 12,301
Ndivyo hivyo sasa jinsi ilivyokuwa na hadi sasa hakuna anachoisaidia familia yake zaidi ya kuwapatia 250, 000/= kwa kila mwisho wa mwezi.Hakyamama Mungu ananiona,hunichukulii mume kifala hivyo,heheee labda km Mungu hayupo!
Yaani huo mpambano wake Mungu ndo anajua!
Km anausikiaga ule mstari wa" usimuache mwanamke mchawi aishi "unavyofanya kazi basi ataelewa
Sbb kiukweli hapo nguvu za giza tu zimetumika,hakuna mwanaume Kwenye akili timamu anaweza fanya hivyo!
Pia inshu kama hiyo imemtokea Binamu yake na Mke wangu, kapurulwa weee na Mchepuko kwa zaidi ya miaka mi5 baada ya kibarua kuota nyasi na kufulia mithili ya fukara na kupigwa chini na Mchepuko wake, ndipo sasa hivi kaanza upya kumsumbua Mkewe wa ndoa kumwomba msamaha warudiane kuishi pamoja ilihali tayari Mkewe alisharudi kwa wazazi wake na watoto wanasomeshwa na kulelewa na Babu na Bibi zao(wazazi wa Mke wa ndoa).
Tena anawasumbua hadi wakwe zake wamwombee msamaha kwa Mkewe wa ndoa ilihali Mama Mkwe kakaza kabisa hataki kusikia huo upumbavu.
Mkasa mwingine, ni kuhusu Best Man wangu yani kiujumla nina shuhuda nyingi sana za matatizo ya Me sababu ya michepuko.