Sky Eclat
JF-Expert Member
- Oct 17, 2012
- 57,595
- 215,272
Bwana mmoja mfanyabiashara aliishi na mke wake kwa muda wa mwaka mmoja bila kufanikiwa kupata mtoto, kwa kuwa jamaa ana uwezo kidogo na yeye ndiye jicho la familia, mama mkwe na mawifi wakaanza vi maneno. Yule bwana alimpenda sana mke wake, wala hakutaka kusikiliza maneno ya ndugu, mke wake alikuwa kabisa yeye hana tatizo ila aligundua jamaa amebeba joka la kibisa.
Mke alimuomba mume wake amletee kijana mtoto wa ndugu ili apate kijana wa kumtuma, na mume wake akisafiri pia asiwe mpweke, kwa sababu jamaa alikuwa anasafiri sana kwa shughuli za biashara.
Yule bwana alikwenda kijijini kwao akaomba kijana mmoja ambae amemaliza darasa la 12 (form IV), kwa ahadi kuwa atamuendeleza na mafunzo ya VETA. Kijana alipofika nyumbani mama alikuwa anamlia timing mume wake, akitoka tu anagawa mechi kwa kijana, hakukua na mapenzi tena alimtisha yule kijana "ukimwambia mtu mambo haya utarudi kwenu".
Haikuchukua hata miezi miwili baada ya kijana kufika mama akainua mimba, mume alifurahi sana, mtoto alizaliwa. Walipofika watoto watatu, kijana alishamaliza mafunzo yake, alipata kibarua na alitafuta chumba chake akaanza maisha yake. Mama alimwambia biashara kati yao imekwisha.
Biashara za baba mwenye nyumba zilianza kwenda vibaya, na aliona huko waendako sio kuzuri, aliamua akatafute maisha Marekani. Baada ya kuwasili kule wenyeji wake walimshauri kuomba ukimbizi.
Alipofanikiwa aliwaambia watu wa uhamiaji ana mke na watoto watatu bongo. Ikabidi mama apeleke watoto ubalozi wa Marekani kwa DNA samples.
DNA zilirudi yule baba siye baba wa watoto, wanasayansi wakamuuliza hawa watoto uliwazaa na mke wako? Akajibu ndio basi wakawapa visa mama na watoto wake. Walipofika kule mama aliombwa awaeleze wanasayansi sayansi alotumia. Mama alitiririka yote! Mume alibaki ametoa macho.
Mwisho wa yote mume akasema hawa watoto tangu wanazaliwa niliwapenda kama wa kwangu na hata kuja kwangu huku ni kuwatafutia wao maisha, hawa ni watoto wangu.
Mke alimuomba mume wake amletee kijana mtoto wa ndugu ili apate kijana wa kumtuma, na mume wake akisafiri pia asiwe mpweke, kwa sababu jamaa alikuwa anasafiri sana kwa shughuli za biashara.
Yule bwana alikwenda kijijini kwao akaomba kijana mmoja ambae amemaliza darasa la 12 (form IV), kwa ahadi kuwa atamuendeleza na mafunzo ya VETA. Kijana alipofika nyumbani mama alikuwa anamlia timing mume wake, akitoka tu anagawa mechi kwa kijana, hakukua na mapenzi tena alimtisha yule kijana "ukimwambia mtu mambo haya utarudi kwenu".
Haikuchukua hata miezi miwili baada ya kijana kufika mama akainua mimba, mume alifurahi sana, mtoto alizaliwa. Walipofika watoto watatu, kijana alishamaliza mafunzo yake, alipata kibarua na alitafuta chumba chake akaanza maisha yake. Mama alimwambia biashara kati yao imekwisha.
Biashara za baba mwenye nyumba zilianza kwenda vibaya, na aliona huko waendako sio kuzuri, aliamua akatafute maisha Marekani. Baada ya kuwasili kule wenyeji wake walimshauri kuomba ukimbizi.
Alipofanikiwa aliwaambia watu wa uhamiaji ana mke na watoto watatu bongo. Ikabidi mama apeleke watoto ubalozi wa Marekani kwa DNA samples.
DNA zilirudi yule baba siye baba wa watoto, wanasayansi wakamuuliza hawa watoto uliwazaa na mke wako? Akajibu ndio basi wakawapa visa mama na watoto wake. Walipofika kule mama aliombwa awaeleze wanasayansi sayansi alotumia. Mama alitiririka yote! Mume alibaki ametoa macho.
Mwisho wa yote mume akasema hawa watoto tangu wanazaliwa niliwapenda kama wa kwangu na hata kuja kwangu huku ni kuwatafutia wao maisha, hawa ni watoto wangu.