Mwanaharamu wa Kisiasa (Riwaya)

Mwanaharamu wa Kisiasa (Riwaya)

ILIPOISHIA
“Sasa mtu unakuwa na pesa, halafu unaiua familia yako! Si bora tu ungefanya kitu kingine,” alisema jamaa mwingine kwa majonzi, mpaka muda huo hakukuwa na mtu aliyejua ukweli juu ya kilichokuwa kimetokea.
SONGA NAYO


Chris alikuwa juu ya mti, usiku mzima hakutaka kulala, alikesha akilia tu. Wauaji wale walioliacha gari lao wakalirudia na kuondoka zao pasipo kumpata mtoto huyo aliyevisumbua vichwa vyao.

Kule mtini alipokuwa, Chris alikuwa akilia, bado kichwa chake kiliifikiria familia yake, hakuamini kile alichokiona kwamba wazazi wake waliuawa kwa kupigwa risasi.

Hakulala, ilipofika saa kumi na moja asubuhi akateremka na kuanza kutembea mbugani. Hakuogopa wanyama wakali, wakati mwingine alitamani kuona akiuawa kwani hakujua ni kwa namna gani angeendelea kuishi pasipo kuwa na wazazi wake.

Alimkumbuka dada yake, Tina. Moyo wake ulimuuma mno kila alipomfikiria. Hakuamini kama wangeweza kutendewa unyama mkubwa kiasi kile, aliumia, alilia na kulia lakini hakukuwa na kilichobadilika, ukweli ulibaki palepale kwamba hakuwa na familia, wote waliuawa vibaya ndani ya chumba cha hoteli.

Aliendelea kusonga mbele, alipokuwa akiwaona wanyama wakali kwa mbali, alijificha kichakani, na walipoondoka aliendelea na safari yake. Hakujua alipokuwa akienda, alichokitaka ni kusonga mbele tu.

Alitembea mpaka alipofika sehemu ambayo kwa mbali aliliona basi likija kwa mwendo wa taratibu. Hakutaka kusimama alipokuwa, akaanza kutembea harakaharaka kuelekea kule kulipokuwa na barabara na kusimama.

Alihitaji msaada, hakujua ni kwa namna gani angeweza kutoka salama ndani ya mbuga hiyo. Aliposimama, akapunga mkono kulitaka gari hilo kusimama. Kila mtu aliyemuona Chris pale mbugani alishangaa, hakuamini kama kungekuwa na mtu, tena mtoto kama yeye ambaye angediriki kuwa kwenye mbuga hiyo iliyokuwa na wanyama wakali.

Dereva akasimamisha gari na kondakta kumtaka kuingia ndani haraka sana. Kila mmoja alimshangaa, walimwangalia, waliona akiwa analia tu na walipomuuliza aliwaambia kwamba wazazi wake walimuacha mbugani na hakujua ni mahali gani walipokuwa.

“Ni hatari sana! Hivi wazazi wanawezaje kumuacha mtoto peke yake katika mbuga yenye wanyama wakali kama hawa?” alihoji jamaa mmoja.

“Kuna watu wana roho mbaya sana. Unaweza kukuta mwanaume kagundua huyu mtoto siyo wake, akaamua kumuacha mbugani ili aliwe na wanyama wakali,” alisema dereva huku akiendesha gari hilo kwa mwendo wa 50 ambao walitakiwa kuutumia wawapo mbugani.

Hakukuwa na mtu aliyegundua kwamba mtoto waliyekuwa wamempakia alikuwa Chris, ilikuwa ni asubuhi sana hata matangazo juu ya msako wake hayakuwa yametolewa. Waliendelea na safari mpaka kufanikiwa kutoka salama ndani ya mbuga hiyo.

Safari iliendelea, basi lilipomaliza mbuga hiyo na kuingia katika Jiji la Motown, Chris akateremka huku akiwashukuru watu hao kwa wema mkubwa waliomfanyia kwani hakika kama wasingekuwa wao basi angeweza kufa pale mbugani.

Akaondoka. Hakujua ni mahali gani alipotakiwa kwenda. Hakuwahi kufika Matapatapa, hiyo ilikuwa mara yake ya kwanza, alibaki mjini huku akiwa anazungukazunguka, hakujua ni mahali gani alipotakiwa kwenda.

Ilipofika saa nane mchana huku akiwa mitaani akakutana na kijana mmoja, alikuwa mchafu, macho ya kijanjajanja, alipomuona Chris, hapohapo akamfuata.

“Wewe nani?” aliuliza kijana huyo huku akimwangalia Chris, hakuishia kumwangalia bali akaanza kumzunguka kana kwamba alikuwa akimchunguza.

“Chris…” alijibu huku akitetemeka.

“Mtoto wa kishua?”
“Hapana!”
“Mbona umependeza? Mbona msafi sana? Wewe utakuwa mtoto wa kishua,” alisema kijana huyo huku akiendelea kumwangalia Chris.

Chris hakujibu kitu, kila alipomwangalia kijana yule, kwake alionekana kuwa mtu mwenye roho mbaya kwani kiunoni mwake alikuwa na kisu, alikichomeka na kukifunika na shati lake lililokuwa limechanika, kwa kutumia matundu ya shati, Chris aliweza kukiona.

Kijana huyo hakuzungumza sana, akaondoka mahali hapo. Chris aliendelea kubaki mitaani, hakujua ni mahali gani alitakiwa kwenda kwani kote humo alikuwa mgeni, kila kitu alichokuwa akikiona, kwake kilionekana kuwa kigeni.

Ilipofika saa moja usiku, kijana yule akamrudia tena, akahisi kwamba Chris alikuwa na tatizo kwani kama alivyomkuta mtaani mchana, hata usiku alikuwa hukohuko.

Akazungumza naye na kumtaka kumfuata alipokuwa akienda, safari yao ndogo iliishia katika sehemu moja iliyokuwa na mapipa mengi ambayo ndani yake kulikuwa na takataka zilizokuwa zikiungua moto huku pembeni kuwa na watoto wengine wa mitaani waliokuwa wakiota moto na wengine kujifunika na magunia.

“Hawa ni washikaji zangu,” alisema mtoto huyo aliyejulikana kwa jina la Ndezi.

Hayo ndiyo yalikuwa makazi yake mapya, hakukuwa na sehemu nyingine ya kwenda, alitamani kurudi nchini Tanzania lakini ilishindikana kwani hakuwa na kiasi chochote cha fedha.

Moyo wake uliumia sana, usiku wa siku hiyo hakulala kwa amani, kila wakati alikuwa akishtuka, sauti za wazazi wake wakiomba msamaha zilijirudia kichwani mwake, zilimuumiza sana huku hasira kali ikianza kumpanda dhidi ya rais wa nchi hiyo kwani aliamini kwamba ndiye mtu aliyefanya mipango kuuawa kwa wazazi wake.

“Kuna siku nitamuua kama kulipa kisasi, siwezi kumuacha hivihivi,” alisema Chris huku akiwa na hasira kali, siku hiyo aliendelea kulala usingizi wa mang’amung’amu mpaka asubuhi.

****

Msako wa kimyakimya ulikuwa ukiendelea, maaskari wa mbugani waliendelea kumtafuta Chris pasipo mafanikio yoyote yale. Vichwa vyao viliuma mno, hawakujua mahali alipokuwa kijana huyo kwani kwenye kila basi walilokuwa wakilipekua, waliambulia patupu, hawakujua kama kijana huyo alipita asubuhi sana kuelekea Motown.

Walipoona kwamba mbugani alikosekana, wakahisi kwamba mtoto huyo alikuwa amekimbilia Motown hivyo vijana kutumwa huko na kuambiwa kwamba walitakiwa kufanya kila liwezekanalo kuhakikisha kwamba mtu huyo anapatikana na kuuawa.

Vijana wenye hasira, walioshika maagizo ya rais wakaingia Motown na kuanza kumtafuta Chris, walizunguka sehemu mbalimbali lakini hawakufanikiwa kumuona kitu kilichowafanya kuhisi labda aliliwa na wanyama wakali kule mbugani.

“Hayupo! Tumemkosa, hivi yupo hai kweli?” aliuliza kijana mmoja, alikuwa amechanganyikiwa, hakujua kama kweli walimkosa Chris.

“Haiwezekani tumkose. Kama kweli aliliwa na wanyamapori, basi ilikuwa ni lazima askari wa mbugani wajue hilo, wangeona hata mifupa yake,” alisema kijana mwingine na hivyo kuendelea kumtafuta Chris.

Hawakuchoka, lakini hawakuweza kumpata, walikuwa wakihangaika, siku hiyo ilipita, hawakuwa wamemuona, wakawasiliana na Rais Labad na kumwambia kile kilichokuwa kikiendelea, rais alikasirika, akawaagiza kwamba wafanye kila liwezekanalo kuhakikisha mtu huyo anapatikana kwani waliamini kwamba bado alikuwa nchini Matapatapa.

“Hakikisheni mnampata,” alisema Rais Labad kwa hasira.

“Haina shida mkuu!”
“Nawapeni siku mbili tu! Hakikisheni mnampata, vinginevyo bora niwape kazi watu wengine na nyie niwaue,” alisema Rais Labad kwa hasira.

Vijana zaidi ya hamsini wakaongezeka, wengine wakaambiwa kwamba walitakiwa kwenda kumtafuta katika mbuga ya wanyama ya Kizwalinda lakini wengine walitakiwa kwenda katika Jiji la Motown kuhakikisha wanamtafuta kila kona.

Hilo likafanyika, zaidi ya vijana ishirini wakashushwa katika Jiji la Motown na kuanza kumtafuta. Chris alikuwa mtu muhimu, alivisumbua vichwa vyao, Rais Labad alikuwa na mawazo tele, moyo wake uliuma sana kwani aliamini kwamba kama asingehakikisha mtoto huyo anapatikana basi hapo baadaye maisha yake yangekuwa ya hatari zaidi.

Wakati akiwa na mawazo tele kuhusu Chris, akapigiwa simu na kuambiwa kwamba mtoto huyo alionekana mitaani hapo Motown huku akiwa pamoja na watoto wa mitaani.

“Una uhakika ni yeye?” aliuliza Rais Labad huku akionekana kutokuamini.

“Ni yeye mkuu!”
“Kweli?”
“Ndiyo!”

“Hebu mpigeni picha ya siri mnitumie,” aliagiza.

Vijana hao walimuona Chris akiwa na watoto wengine wa mitaani, walipomwangalia, alionekana kuwa na hofu kubwa, kila wakati alikuwa akiangalia huku na kule na muda mwingi alionekana kuwa na huzuni tele.

Alichokifanya kijana mmoja ni kuchukua simu yake yenye uwezo mkubwa kisha kumpiga picha na kumtumia Rais Labad ambapo baada ya kuiangalia, akagundua kwamba alikuwa Chris.

“Ndiye yeye! Muueni haraka sana,” alisema rais.

“Hapahapa?”
“Hapana! Hapo ni noma! Mtekeni na mkamuulie mafichoni,” alisema Rais Labad na vijana hao kumwambia kwamba jamboo hilo lingefanyika haraka sana na hivyo kumfuata kwa lengo la kumteka.

Je, nini kitaendelea?
Tukutane Alhamisi hapahapa.
Oy mkuu tunaomba basi story zako uwe unaunganisha hapa chini kuliko kufungua thread nyingine
 
MWANAHARAMU WA KISIASA-04

Chris alikuwa mitaani na watoto wenzake, hakuwa na marafiki, mtu ambaye alikuwa naye kila alipokuwa alikuwa Ndezi tu ambaye kila wakati yeye ndiye aliytemwambia twende huku au kule, yeye ndiye aliyemkutanisha na watoto wengine na kumtambulisha.

Maisha hayo yalimuumiza mno, hakuamini kama katika safari ya kuelekea nchini Matapatapa na familia yake angejikuta akiwa mitaani huku akitafuta maisha. Kwa wakati huo, hakukuwa na mtu aliyejua kama Chris alikuwa mitaani, kwa Tanzania, walipata taarifa kwamba Bilionea Massawe aliiua familia yake lakini hawakujua mahali alipokuwa Chris kwa wakati huo.

“Chris! Unapokuwa kwenye tatizo ni lazima upambane kiume,” alisema Ndezi huku akimwangalia Chris.

“Kivipi?”
“Kuna ubabe mkubwa sana huku mtaani. Unaweza kupata pesa halafu kuna wajinga flani wakakufuata na kutaka kuchukua pesa zako, hivyo ni lazima upambane,” alisema Ndezi huku akimwangalia Chris.

“Kwa kupigana?”
“Hapana! Unaweza kupambana kwa kisu au hata bisibisi,” alisema Ndezi maneno yaliyomfanya Chris kushtuka kwani katika maisha yake hakuhisi kama ingetokea siku angeweza kuchukua kisu na kupambana na watu wengine.

Walikuwa wakizunguka huku na kule, walionekana kama watoto wa mitaani lakini kwa Chris alionekana kuwa tofauti na wenzake. Mavazi yake yalikuwa masafi na muda mwingi hakuwa mtu wa kuomba pesa kama ilivyokuwa kwa wenzake.

Saa zilikatika, mpaka vijana wa Rais Labad wanamuona mitaani hakuwa akijua, hakuwafuatilia kwani aliamini kwamba kwa kile kilichotokea mbugani, kisingeweza kuendelea mpaka mitaani.

“Tumfuateni!” alisema kijana mmoja, alikuwa akimwangalia Chris aliyekuwa na Ndezi katika Soko Kuu la Motown ambapo kulikuwa na idadi kubwa ya watu.

“Tusubiri mpaka atoke ndani ya soko!”
“Tunachelewa!”
“Ila tukimfuata, watu wengine watahisi vipi? Tena na hii hali ya watoto kutekwa na kuuawa si ndiyo itatuletea msala?” alihoji jamaa mmoja, alionekana kuwa na wasiwasi mkubwa.

Wenzake hawakutaka kumsikiliza, walijiona wao kuwa sahihi kuliko hata yeye, walichokifanya ni kuteremka kutoka ndani ya gari na kuanza kumfuata Chris aliyeendelea kuwa na Ndezi, walipomfikia, wakamsimamisha.

“Dogo mambo vipi?” aliuliza jamaa mmoja.

Chris hakujibu, alisimama na kuanza kuwaangalia watu hao, hakuwafahamu, alihisi labda wanaweza kuwa wale wanaume waliokuwa hotelini lakini hawakuwa wao, hakujua walihitaji nini, alisimama pamoja na Ndezi huku wakiwaangalia kwa mshtuko.

“Tuna kazi tunataka utusaidie,” alisema jamaa mmoja huku akimwangalia Chris.

“Kazi gani bro?” aliingilia Ndezi.

“Siyo wewe! Tunataka atusaidie huyu.”

“Mimi ndiye meneja wake, bila mimi haendi sehemu,” alisema Ndezi huku akiwaangalia wanaume hao nyusoni mwao.

Alikuwa kijana wa mitaani, mhuni asiyeogopa kitu chochote kile, kwa jinsi mtazamo alioutumia kuwaangalia wanaume hao ulionyesha kabisa kwamba hakuwa mtu wa mchezo hata kidogo.

Walichokifanya ni kuwaambia wawafuate kule walipokuwa wakielekea kwenye gari ambapo ndipo waliposema kwamba kulikuwa na mizigo, walipofika na kuufungua mlango, wakawaingiza wote na kisha kuufunga mlango.

“Tulieni humo ndani,” alisema mwanaume mmoja kwa sauti ya ukali, tena ya kibabe hasa.

Ndezi hakujua ni kitu gani kilikuwa kikiendelea mahali hapo lakini kwa Chris akagundua kwamba inawezekana watu hao walikuwa miongoni mwa wale vijana waliokwenda hotelini mule na kuwaua wazazi wake.

Akaingia na hofu na kuona kwamba huo ndiyo ungekuwa mwisho wake, akaanza kulia. Ndezi alikuwa kimya, aliwaangalia watu hao, waliwaweka nyuma ya gari lile huku huko wakiwa na mwanaume mmoja na wengine wawili wakiwa mbele.

Gari lilikuwa likiondoka kutoka ndani ya soko lile, kutokana na umati mkubwa wa watu, gari liliendeshwa kwa mwendo wa taratibu sana mpaka walipofika nje ya soko lile na ndipo dereva alipoongeza mwendo kuelekea kulipokuwa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Motown.

“Oya! Tunakwenda wapi huku?” aliuliza Ndezi huku akiwaangalia watu hao, hakujua kitu chochote kile, kwake, walionekana kuwa watekaji ambao waliwachukua kwa ajili ya kwenda kuwaua.

“Nyamaza nyambafu we’,” alisema jamaa waliyekuwa naye katika viti vya nyuma.

“Nitanyamazaje na wakati nataka kujua tunakwenda wapi,” alisema Ndezi lakini hata kabla hajakaa vizuri akashtukia akipigwa kibao kimoja cha nguvu shavuni mwake.

“Nimekwambia nyamazaaa…” alisema mwanaume ambaye walikuwa naye nyumba ya gari lile.

Ndezi akanyamaza, moyo wake ukajawa na hasira, hakuamini kama alipigwa kibao kizito namna ile, kwake, ile ilionekana kuwa dharau kubwa, hakuamini kama kungekuwa na mtu ambaye angediriki kumzaba kibao namna ile.

Mwanaume mmoja miongoni mwa wale waliokuwa mbele ya ile gari akampigia simu Rais Labad kwa ajili ya kumpa taarifa kwamba walifanikiwa kumpata Chris na muda huo walikuwa njiani kuelekea sehemu walipotakiwa kumuulia.

“Safi sana, muueni haraka iwezekanavyo halafu mwili wake muuzike porini,” alisikika kwenye simu kwa sauti ambayo watu wote ndani ya lile gari waliisikia.

Ndezi akajiangalia kwenye kiuno chake, kisu chake kilikuwa mahali hapo, alihisi kwamba safari hiyo ilikuwa mbaya na kama asingefanya jambo moja basi wangeweza kupelekwa sehemu na kuuawa.

Alichokifanya kwa haraka sana ni kukitoa kisu chake kisha kumchoma mwanaume walioyekuwa naye nyuma ya gari lile, hakumchoma mara moja, kwa haraka sana akamchoma mara tatu na kisha kuhamia kwa wanaume waliokuwa mbele ya gari.

Alianza na aliyekaa upande wa kushoto, akamchoma mara mbili kisu cha shingo, wakati dereva akigundua hilo na kutaka kumpokonya kisu kile, akashtukia naye akichomwa kisu cha shingo mara mbili tena kwa haraka sana.

Damu zikaanza kumtoka, akahisi kwamba mwili wake ukiishiwa nguvu, mikono yake ikaacha usukani na hapohapo gari likaacha njia na kuanza kuelekea bondeni kwa kasi kubwa.

“Jifunge mkanda,” alisema Ndezi na Chris kufanya hivyo harakaharaka.

Gari likaelekea bongeni ambapo huko likagonga mti mmoja mkubwa, likapinduka na wote wawili kuanza kuugulia maumivu mule garini walipokuwa.

“Chris…Chris….upo hai?” ailuliza Ndezi huku akimwangalia Chris aiyekuwa akitokwa na damu kwenye paji la uso.

“Nipo hai…koh koh koh,” alisema Chris na kukohoa mfululizo.

Hawakutaka kubaki mule, wakaanza kutoka. Ndezi hakutaka kukubali, alihisi kabisa kwamba watu wale walikuwa na pesa mifukoni hivyo akaanza kuwapekua.

Akawakuta na kiasi kikubwa cha fedha, akachukua simu zao na kuondoka katika eneo la tukio haraka sana kwani hawakutaka mtu yeyote awaone mahali hapo.

Wakati wakiwa njiani, ghafla simu moja ikaanza kuita, harakaharaka akaichukua na kuangalia kwenye kioo, jina aliloliona lilisomeka ‘Rais Labad’ akamuonyeshea Chris.

“Huyu amewaua wazazi wangu na dada yangu,” alisema Chris huku akionekana kuwa na hasira kali.

“Kumbe! Sasa wewe mtoto wa mbunge au?” aliuliza Ndezi.

“Pokea kwanza!”

Ndezi akaipokea simu ile na sauti ya Rais Labad ikaanza kusikika kutoka upande wa pili. Kitu cha kwanza kabisa alichouliza kilikuwa ni kazi yake aliyokuwa amewapa, je Chris alikuwa amekwishauawa na mwili wake kuzikwa au bado?

“Bado hajauawa kwa sababu tumewaua wao,” alijibu Ndezi huku akibadilisha sauti yake na kutaka isikike kama mtu mzima.

“Wewe nani?”

“Mshikaji mmoja hivi mtata.”

“Umepata wapi simu hii?”

“Nimewachukulia kisela. Ishu ni kwamba wana wamepata mzinga huku barabarani, kama vipi njooni mchukue miili yao ila kuanzia sasa usipige simu hii kwani ndani ya saa moja itakuwa imeuzwa kwa mtu mwingine kabisa,” alisema Ndezi.

“Wewe ni nani?”

“Daah! Rais unayumba sana! Nimekwambia msela flani hivi mtata lakini hunielewi! Wewe njoo uchukue maiti zako,” alisema Ndezi, hakutaka kuendelea kuongea, hapohapo akakata simu, akaizima, akatoa laini kisha kuiweka mfukoni na kuondoka mahali hapo akiwa na Chris aliyekuwa hoi, na muda wote alionekana kumuogopa Ndezi kwani hakuwahi kumuona mtu aliyekuwa na ushujaa wa kuwaua watu watatu kwa tukio moja kama alivyofanya ndani ya gari lile.

****

Rais Labad alichanganyikiwa, hakujua ni kitu gani alitakiwa kufanya, alipoambiwa kwamba baadhi ya vijana wake walikuwa wameuawa, alihisi moyo wake ukipata hasira kali ambayo hakuwahi kuipata katika maisha yake.

Kitu kilichomkasirisha zaidi kilikuwa ni simu aliyozungumza na mtu asiyemjua. Aliongea kihuni, maneno ya kejeli ambayo yaliufanya mwili wake utetemeke na kijasho chembamba kumtoka.

Hakutaka kukubali, alitaka kumuangamiza Chris kabla ya kuwaambia watu ukweli wa kile kilichokuwa kimetokea, akawapigia simu vijana wake wengine na kuwaambia kilichokuwa kimetokea, na kama ingewezekana basi waondoke kwenda kule kulipotokea ajali hiyo na kuangalia ni kitu gani kilitokea na wafanye juu chini, kama wahanga hawajafa, basi wawaue.

“Sawa mkuu!”

Hakutaka kuishia hapo, alijua kwamba kulikuwa na kazi kubwa kumpata Chris kwani mpaka hapo tu tayari aliona akisumbuka kumpata, akajua kwamba kama kweli gari lilipata ajali, basi inawezekana yule mtu aliyezungumza naye kwenye simu alikuwa rafiki wa Chris au mtu yeyote ambaye alikuwa akijua mahali Chris alipokuwa, hivyo mtu wa kwanza kabisa ilikuwa ni kumtafuta huyo mtu.

Akawapigia simu watu wa mitandao ya simu na kuwaambia kilichokuwa kimetokea, alitaka kujua mahali simu hiyo ilipokuwa, hata kama laini ya simu ingetolewa, aliamini kwamba bado simu hiyo ingeweza kufanya kazi, hivyo alihitaji kujua mahali ilipokuwa.

Hilo halikuwa tatizo, watu wa mitandao wakaingia kwenye kompyuta zao na kuanza kufanya kazi zao. Haikuwa kazi kubwa, kwa kuwa laini ya simu hiyo ilitumika katika simu iliyoibwa, wakaweza kuinasa mpaka mahali ilipokuwa hivyo kumpa taarifa.

“Mkuu! Tumeweza kuinasa simu yenyewe,” alisema kijana mmoja.

“Safi sana! Nitataka kijana mmoja aje, aongozane na vijana wangu mpaka mahali ambapo simu hiyo ilipokuwa,” alisema Rais Labad.

“Hakuna shida!”

Rais hakutulia, muda wote alikuwa akizunguka huku na kule, alichanganyikiwa, mtu aliyekuwa akimuumiza kichwa kwa wakati huo alikuwa Chris ambaye hakujua alikuwa mahali gani.

Alitaka kuficha siri juu ya kila kitu kilichotokea, kitendo cha kijana huyo kutokupatikana kilimaanisha kwamba angekuwa kwenye wakati mgumu sana, alitaka kuona akiuawa haraka iwezekanavyo ili kuifanya ile siri iendelee kuwa siri milele na milele.

Baada ya saa kadhaa vijana watatu wakafika mahali hapo, wakapewa vijana ambao walitakiwa kutangulizana nao kwa ajili ya kuifuatilia simu hiyo kwani ilikuwa ni lazima kumpata mtu aliyekuwa nayo kwa kuhisi kwamba ndiye aliyesababisha ajali au aliliona tukio hilo tangu mwanzo hivyo alikuwa mtu muhimu wa kutoa ushahidi.

Wakaondoka, yeye akabaki ikulu akiendelea kusikilizia kile kilichokuwa kikiendelea. Hakutulia, wakati mwingine hata simu za mawaziri hakuwa akizipokea kwani kile alichokuwa akikisubiria kilikuwa muhimu kuliko simu hizo.

Vijana wale kwa kutumia msaada wa GPRS wakaweza kuinasa simu hiyo. Ilionyesha kwamba ilikuwa katika Mtaa wa Mavizio ambao ulikuwa pembeni kidogo ya Mji wa Motown, mtaa uliokuwa uswahili ambapo kulikuwa na matuki makubwa yaliyokuwa yakitokea kila siku.

“We got him,” (tumemnasa) alisema jamaa mmoja, alikuwa akiwaambia wenzake kumaanisha kwamba GPRS ilisoma mahali alipokuwa mtu huyo.

Wakaanza kumfuatilia, haikuwa kazi nyepesi kwani hapo walipokuwa walitakiwa kuendelea na safari mpaka huko Mavizio kwa ajili ya kuonana na mtu huyo. Huko, walitakiwa kuwa wapole, walijua dhahiri matukio yaliyokuwa yakitokea huko hayakuwa ya kawaida, wanawake walibakwa, watu waliuawa, kulikuwa na matukio mengi yaliyokuwa yakitokea.

Hawakuchukua muda wakafika Mavizio, wakateremka kutoka garini na kuanza kufuatilia simu hiyo ilipokuwa ikionekana kwenye kifaa kidogo walichokuwa nacho. Kulikuwa na ugumu kwani kuifikia ilikuwa ni kupita katika vichochoro vingi, walikutana na wahuni lakini hawakuogopa kwani walikuwa na bastola ambazo zilionekana kama ulinzi kwao.

“Ipo kule mbele, tunaikaribia,” alisema jamaa mmoja wa mtandao wa simu.

Waliendelea kwenda mbele, watu walikuwa wakiwaangalia, kwa jinsi walivyoonekana, hawakuonekana kuwa watu wa kawaida hata kidogo, wengi walihisi kwamba walikuwa polisi waliokuja kumkamata mtu ila hawakutaka tu kuvaa sare. Waliogopwa, kila walipopita, wahuni wengine waliokuwa na bangi mikononi wakaingia ndani kujificha.

“Ni hapo nyuma,” alisema mwanaume mmoja, walikuwa wamekwishafika sehemu husika, kilichobaki ni kwenda mahali hapo kwani walizisikia sauti za watu wakizungumza kuhusu simu, wakajua ndiyo sehemu yenyewe.

****

Ndezi akakata simu, moyo wake ulikuwa kwenye furaha tele kwani alipata simu tatu za bure na hivyo mpango uliokuwepo ulikuwa ni kuziuza na fedha kufanyia mambo yake mengine. Akaondoka na Chris kwenda mitaani kabisa. Muda wote Chris alionekana kuwa na hofu, hakuamini kama yale mauaji makubwa yaliyofanywa yalifanywa na mtu kama Ndezi.

Umri wake na matendo aliyoyafanya vilikuwa vitu viwili tofauti, alionekana kuwa na umri mdogo lakini alikuwa na roho ya chuma, hakukubali kuona akionewa, hakukubali kuona akifanyiwa jambo lolote baya.

Walipoondoka hapo, wakaelekea katika Mtaa wa Mavizio, huko, alitaka kwenda kuziuza simu hizo. Walipofika, akaanza kuzitembeza huku na kule, alikuwa akimuonyeshea kila mtu aliyekuwa akikutana naye.

Zilikuwa simu nzuri, baada ya kuzitembeza kwa dakika kadhaa, akasimamishwa na mwanaume mmoja ambaye naye alizitaka simu hizo kwani kwa muonekano wake zilikuwa nzuri na isingekuwa rahisi kuziacha.

“Kiasi gani?”
“Hii laki mbili na nyingine laki laki,” alisema Ndezi hivyo mwanaume yule kumchukua na kumpeleka sehemu ambayo ilikuwa nzuri kufanya biashara hiyo ya wizi.

“Nakupa laki tatu zote!” alisema mwanaume huyo.

“Umeua bendi mzazi! Niachie jiwe tatu na nusu,” alisema Ndezi.

“Hiyo nyingi sana. Si unajua simu zenyewe za wizi hizi zimejaa magumashi, kama vipi kamatia tatu nisepe,” alisema mwanaume huyo, waliendelea kupatana bei pasipo kujua kwamba moja ya simu zile ilikuwa ikifuatiliwa.

“Tuondoke…” alisema Chris huku akionekana kuwa na hofu, macho yake hayakutulia, yalikuwa yakiangalia huku na kule..

“Subiri kwanza tupige mkwanja halafu tutasepa.”
“Ila nina hofu!”
“Ondoa hofu! Upo na komandoo,” alisema Ndezi huku akiwa na uhakika kwamba kila kitu kilikuwa salama kabisa.

***

Vijana wale walikuwa na uhakika kwamba watu waliokuwa nyuma ya nyumba ile ndiyo ambao walikuwa wakihitajika na Rais Labad hivyo walichokifanya ni kwenda nyuma ya nyumba ile.

Wakawakuta vijana watatu, baada ya vijana hao kuwaona, wakashtuka kwani hawakutegemea kuona wakifuatwa na watu kama hao ambao kwa kuwaangalia tu walionekana kuwa si watu wa utani hata kidogo.

Wakawaweka chini ya ulinzi na kuwapokonya simu, kitu cha kwanza kabisa kilikuwa ni kuwauliza kuhusu simu hiyo, walichowaambia ni kwamba waliinunua kutoka kwa kijana mmoja aliyekuwa na mwenzake.

“Kijana gani?”
“Dogo fulani, alinifuata na kusema kwamba anauza simu, tena alikuwa nazo tatu ambazo zote nilizinunua,” alijitetea kijana huyo.

“Yupo wapi?”
“Sijajua! Ni mtoto wa mitaani, hata nilipoona anauza simu nilijua angeniuzia kwa gharama nafuu, hivyo nikamlalia,” alijitetea kijana huyo.

Kwa kumwangalia tu ilionekana kuwa vigumu kuamini kama yeye ndiye aliyeiiba simu hiyo, alikuwa kijana mtanashati, alivalia shati jeupe na alichomekea.

Hawakuwa wakimuhitaji yeye, waliyekuwa wakimuhitaji alikuwa kijana ambaye aliiba simu hiyo lakini pamoja na hayo, hawakutaka kumuacha, wakamchukua yeye na wenzake na kuondoka nao mahali hapo.

Rais Labada akapewa taarifa juu ya kile kilichokuwa kimetokea, hakuamini kama kweli alishindwa kufanikisha kumpata kijana huyo ambaye aliamini kwamba alikuwa na Chris ambaye alikuwa akimtafuta kwa udi na uvumba.

Akawaambia vijana hao wawapige picha na kuwatumia ili kuona kama walikuwa wao au si wao, alivyotumiwa picha na kuziangalia, hawakuwa wao, hakumuona Chris na hata vijana hao walionekana kuwa wasafi kwani mtu ambaye alipokea simu alikuwa mhuni sana.

“Siyo hao!” alisema Rais Labad.

“Kwa hiyo hawa tuwafanye nini mkuu?”
“Waachieni ila wapokonyeni simu zote.”

Hilo ndilo lililofanyika, halikuhitaji maswali, wakafanya kama walivyoambiwa, wakawapokonya simu na kuwaambia wapotee, wakafanya hivyo.

Mitaani, vijana walikuwa wakihangaika huku na kule, kumpata Chris lilionekana kuwa jambo gumu, kwa kuwa alikuwa na mtandao mkubwa, Rais Labad akapeleka picha za Chris katika vituo vyote vya polisi na kuwaambia kwamba kijana huyo alitakiwa kutafutwa kimyakimya na picha zake zisitoke nje ya vituo hivyo.

“Sawa mkuu!”

Polisi wakaanza kumtafuta Chris mitaani, walikuwa na uhakika kwamba wangeweza kumpata kwani mbali na vituo ishirini vilivyokuwa katika Jiji la Motown, pia kulikuwa na polisi wengi ambapo kwa pamoja waliweka nguvu kwa mtu mmoja tu.

Wakaachana na mambo mengi, wakaacha kuwatafuta wavuta bangi, kipindi hicho ndicho biashara haramu ilipokuwa ikifanyika kwa nguvu zote kwani polisi hawakuwa na mpango wa kuwatafuta watu hao, wao walikuwa wameweka nguvu zao kumtafuta Chris tu.

Kila siku ilikuwa ni lazima kufikisha taarifa kwa mkuu wa kituo juu ya mahali walipofikia ambapo wao walimpigia simu Rais Labad na kumwambia kile kilichotokea.

Rais hakuamini kama kazi ingekuwa ngumu namna ile, aliamini kwamba kumkamata Chris haikuwa kazi kubwa kwa kuwa alikuwa hapohapo Motown, sasa ugumu ulitoka wapi?

Alikasirika! Aliendelea kuwasisitizia watu wake kwamba iwe isiwe ilikuwa ni lazima Chris apatikane kwani alijua hatari iliyokuwa mbele yake kama tu wasingehakikisha mtoto huyo anakamatwa.

Akaagiza ulinzi uongezeke mipakani kwani alijua kwamba kwa namna moja ama nyingine Chris angeweza kuondoka nchini Matapatapa kuelekea Tanzania ambapo huko angeweza kutoa ushahidi juu ya kile kilichokuwa kimetokea.

“Hakikisheni mipaka inaongezwa ulinzi na picha za huyo mtoto zinasambazwa huko mpaka apatinake! Mmenielewa?” alisema Rais Labad.

“Ndiyo mkuu!”

Hilo halikuhitaji kupoteza muda, haraka sana likafanyika, mipakani, picha zikapelekwa, ilikuwa ni lazima wamzuie Chris kama tu angetaka kutoroka nchi hiyo.

Hakutakiwa kufika nchini Tanzania kwa kuamini kwamba kama angefika huko ilikuwa ni lazima kukutana na waandishi wa habari na hiyo kuwaambia kilichokuwa kimetokea nchini Matapatapa.

Akaongeza vijana wake mitaani, polisi wote jicho lao likawa kumtafuta Chris, hawakujua alifanya nini wao walichokuwa wakikifanya ni kumfurahisha rais wao kwani bila kufanya hivyo waliogopa kupoteza kazi zao.

***

Ndezi alikubaliana na mnunuaji na kumuuzia simu zote alizokuwa nazo, akapewa kiasi cha laki tatu na kuondoka zake huku akifurahia, hakutaka kubaki na simu zile kwa kuamini kwamba zilikuuwa tatizo kwani angeweza kutafutwa na kukamatwa kwani simu aliyokuwa amepokea, ilimtisha.

Wakatafuta maji na kunawa, wakatafuta sehemu na kupumzika kwani walijiona kuwa na safari kubwa na bahati kubwa ajali ile haikuwa imewajeruhi kwa kuwa walikuwa katika siti za nyuma.

Hakujua sababu iliyomfanya Rais Labad kuwatuma watu na kuwakamata, aliamini kwamba yeye hakuwa na tatizo lolote bali mtu aliyekuwa na tatizo alikuwa Chris.

Alitaka kujua ukweli juu ya kitu kilichokuwa kikiendelea, alitaka kufahamu sababu iliyomfanya kutafutwa na mtu mzito kama Rais Labad. Akamuuliza lakini Chris hakumwambia ukweli, alimficha, kwa jinsi maongezi yake yalivyokuwa, Ndezi akahisi kwamba kulikuwa na tatizo.

“Niambie ukweli,” alisema Ndezi.

“Huo ndiyo ukweli! Mimi mwenyewe sijui!” alisema Chris.

Ndezi alikasirika sana, hakukuwa na kitu alichokuwa akikichukia kama kudanganywa, alimwambia Chris amwambie ukweli vinginevyo kama alikuwa akimdanganganya na siku moja kuujua ukweli basi kungekuwa na tatizo.

“Ni kwamba anataka kuniua!” alisema Chris.

“Najua! Ila nisichokijua ni kwa nini anataka kukuua,” alisema Ndezi.

“Ni kwa sababu aliwaua wazazi wangu!”
“Wazazi gani?”

“Wale waliouawa jana mbugani!”
“Unamaanisha bilionea Massawe aliyeiua familia yake jana?”
“Ndiyo huyohuyo ila hakuiua familia yake bali iliuawa na watu waliotumwa na rais huyo!” alisema Chris
“Na wewe ndiye huyo mtoto ambaye anatafutwa kila kona?” aliuliza Ndezi.

“Ndiyo!”
“Duuh! Kumbe nipo na brifukesi la pesa halafu sijui. Tufanye mishe tusepe hapa Motown, kushanuka, tusepee zetu Tanzania tukachukue huo mkwanja aliouacha baba yako,” alisema Ndezi huku akionekana kuwa na furaha.

Walikuwa na pesa, kiasi walichokuwa wamekipata waliamini kwamba kingewawezesha kufika nchini Tanzania. Kulikuwa na njia mbili za kufika huko, wangeweza kupitia mpakani auu baharini, walichochagua, kupitia mpakani ilikuwa rahisi zaidi.

“Hapa ni kuvuka boda mwana, hakuna jingine,” alisema Ndezi.

“Sawa.”
Walichokifanya ni kuchukua daladala iliyokuwa ikielekea Mabweni, Kusini mwa Jiji la Motown, kilometa mia nane kutoka hapo mjini. Huko ndipo kulipokuwa na mpaka wa kuingia nchini Tanzania.

Ndani ya daladala waliyochukua, walikuwa kimya. Kila mmoja alikuwa na mawazo yake, kwa Chris alikuwa akifikiria kufika salama nchini Tanzania lakini kwa Ndezi alichokuwa akikifikiria kilikuwa ni pesa tu.

Kitendo cha kuwa karibu na Chris alihisi kwamba yeye ni milionea mkubwa. Hakutaka kumuacha Chris, aliambatana naye na hata kama angepata matatizo pamoja naye, alikuwa radhi lakini mwisho wa siku apate kile alichokuwa akikitaka.

Hawakujua kwamba hata huko mpakani, kulikuwa na polisi waliokuwa wakiwatafuta kwa udi na uvumba.

***

Umati wa Watanzania ulikusanyika katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere kwa ajili ya kuipokea miili ya wanafamilia, Bilionea Massawe ambaye alikufa nchini Matapatapa.

Kila mtu alionekana kuwa na huzuni, wengi walilia, hawakuamini kama kweli bilionea huyo aliiteketeza familia yake kwa kuipiga risasi na kuwamaliza.

Mioyo yao iliuma na wengi kumlaumu kwamba hakutakiwa kufanya kitu kama kile, hata kama alikuwa na mawazo, hasira alitakiwa kuongea na watu wa ushauri na kumwambia nini cha kufanya.

Waandishi wa habari hawakukosa uwanjani hapo, kamera zao zilikuwa mikononi kwa ajili ya kupiga picha kila kitu kilichokuwa kikiendelea mahali hapo.

Ulionekana kuwa msiba mkubwa wa kitaifa kwani bilionea huyo alikuwa mtu wa watu, alipendwa, alikuwa na kampuni nyingi ambazo ziliwaajiri Watanzania wengi.

Viongozi wengi wa kisiasa walikuwa uwanjani hapo, bado hakukuwa na mtu aliyeamini, kila mmoja alikuwa akijiuliza kama iliwezekanaje mwanaume huyo akafanya mauaji hayo katika siku ya matembezi nje ya Tanzania badala ya kuyafanya mauaji hayo hapahapa Tanzania tena nyumbani kwake?

Huzuni ziliendelea kuwatawala, maswali mengi yaliendelea kuwatatiza vichwani mwao. Wengi walitaka kufahamu kuhusu Chris, hakuwa miongoni mwa watu waliouawa, alikuwa wapi na kwa nini hakuuawa? Wengi walitaka kulifahamu hilo.

Saa 4:18 asubuhi ndege iliyobeba miili ya marehemu hao ikaanza kuingia uwanja wa ndege. Vilio vilivyokuwa vikisikika mahali hapo, vikaongezeka zaidi, ndugu wengi walilia kwani hawakuwa wakiamini kama huo ndiyo ungekuwa mwisho wa kuwa na ndugu zao hao.

Ndege ilipotua, majeneza matatu yakatolewa ndani ya ndege na kisha kuanza kusukumwa kwa vyombo vilivyokuwa na mataili kuelekea kule kulipokuwa na umati wa watu.

Waandishi wa habari wakajisogeza kule na kuanza kupiga picha. Kilichokuwa kikiendelea mahali hapo kilimuumiza kila mmoja. Miili hiyo ikachukuliwa na kupelekwa nyumbani kwao.

Huko, umati mkubwa wa watu ulikuwa umekusanyika nyumbani hapo, watu walitaka kuona kitu gani kilikuwa kikiendelea kama kuhuzunika, walihuzunika na kulia sana.

“Jamani! Hivi kweli Massawe ameimaliza familia yake kweli?” aliuliza jamaa mmoja huku akionekana kutokuamini.

“Hata mimi mwenyewe nashangaa….jinsi jamaa alivyokuwa na furaha na familia yake kweli aliwezaje kuiangamiza? Nahisi si kweli, mimi mwenzenu naanza kuhisi kitu,” alisema msichana mmoja, alionekana kuwa na huzuni mno.

“Wewe ni kama mimi! Nahisi kuna mchongo umechezwa,” aliongezea mwanaume mwingine.

Kila mmoja alionekana kuwa na wasiwasi, walimfahamu Massawe, alikuwa miongoni mwa watu waliokuwa wakiipenda mno familia zao, kwenye mitandao ya kijamii na sehemu nyingine aliionyeshea kwamba ilikuwa kila kitu katika maisha yake.’

Kitendo cha taarifa kusema kwamba yeye ndiye aliyeiua familia yake kilimshangaza kila mmoja na kuhisi kwamba kulikuwa na kitu kilichokuwa kimetokea.

“Kuna kitu hapa.”
“Hata mimi nahisi hivyo!”

Hayo ndiyo maneno yaliyokuwa yakisikika msibani hapo, kila mmoja alihisi kwamba kulikuwa na mtu aliyeiangamiza familia hiyo lakini hakukuwa na mtu aliyejua kama familia hiyo iliangamizwa na Rais Labad.

Japokuwa alikuwa na matatizo nchini kwake lakini hakukuwa na mtu aliyefahamu kama watu hao walikuwa kwenye ugomvi mkubwa. Kutokana na kile kilichotokea, kila mmoja akahisi kwamba kulikuwa na bilionea ambaye alikuwa kwenye ugomvi na marehemu na kuamua kumfanyia unyama huo.

Polisi hawakutaka kubaki kimya, kwa kile kilichokuwa kimetokea kilikuwa kikubwa mno, ilikuwa ni lazima wafanye uchunguzi wa ndani kugundua ni kitu gani kilitokea, ni mtu gani alisababisha mauaji yale.

Walijua kwamba kama wangetaka ushirikiano na nchi ya Matapatapa wasingeweza kuupata kwani wao ndiyo waliotangaza kwamba mwanaume huyo aliiangamiza familia yake na mwisho kujimaliza yeye mwenyewe.

“Ni lazima tuliangalie jambo hili kwa undani, ni lazima tujue kila kitu kilichokuwa kimetokea,” alisema Kamanda Mkuu wa Jeshi la Polisi, IGP Mwalami, alikuwa akizungumza na polisi wenzake wa kitengo cha upelelezi.

Waliamua kuweka kikao hicho ambacho kiliwachukua dakika thelathini, mwisho kabisa wakamalizia kwa kumchagua Edson Mwalugonde, kijana machachari aende nchini MAtapatapa, kulekule kwenye Mbuga ya Kizwalinda kwa ajili ya kufanya upelelezi na kugundua ni kitu gani kilikuwa kimetokea mpaka bilionea huyo aiangamize familia yake.

Wakati wakimchagua Edson kwa ajili ya kuchunguza juu ya vifo hivyo, hakuwepo nchini Tanzania, alikuwa nchini Uingereza akifurahia maisha baada ya kukamilisha kazi ya kupeleleza kila kitu kilichotokea katika utekwaji wa watoto wengi nchini Tanzania. Kazi hiyo aliifanya na kuimamilisha, wahusika wakakamatwa, hivyo kuelekea nchini Uingereza kwa ajili ya kupumzika.

Alipopigiwa simu na kupewa taarifa ya kifo cha Bilionea Massawe, alichanganyikiwa, hakuamini kama bilionea huyo aliweza kuimaliza familia yake, kama watu wengine walivyohisi kwamba waliuawa ndivyo alivyohisi hata yeye mwenyewe.

Hakutaka kuendelea kukaa nchini Uingereza, alichokifanya, kwa haraka sana akaondoka kurudi nchini Tanzania, alipofika, akapewa kazi hiyo na kuambiwa kwamba alitakiwa kuelekea huko, katika mbuga hiyo kama mtalii kutoka nchini Nigeria, hilo halikuwa tatizo, akaahidi kufanya kazi hiyo kwa uadilifu mkubwa kabisa.

Kesho yake, saa 6:09 mchana alikuwa ndani ya ndege akielekea nchini Matapatapa. Kichwa chake kiliendelea kumfikiria Bilionea Massawe, alifahamu, mwanaume huyo alikuwa roho nzuri, aliipenda familia yake kuliko kitu chochote kile, kila alipokuwa akitafuta uwezekano wa bilionea huyo kuiteketeza familia yake, kitu hicho hakikuingia kabisa kichwani mwake.

“Hapa kuna kitu! Sidhani kama Bilionea Massawe anaweza kuiteketeza familia yake. Nahisi kuna kitu, na nitakijua tu,” alijisemea huku ndege ikikata mawingu kuelekea nchini Matapatapa.

Haikuchukua saa nyingi, ikafika huko. Akateremka na kukodi gari ambalo lilimpeleka mpaka katika mbuga hiyo. Ilikuwa vigumu kumgundua kama alikuwa Mtanzania, alizungumza Kiingereza kama Mnigeria, aliiga lafudhi hiyo na kila alipokuwa akizungumza, watu wengine hawakuelewa kutokana na Kiingereza chake kuwa na lafudhi ya Lugha ya Yoruba.

“Where are from?” (Umetoka wapi?) aliuliza mhudumu wa mapokezi.,

“Yoruba my friend,” (Yoruba rafiki yangu) alijibu Edson huku akichia tabasamu, kwa jinsi alivyoonekana, alikuwa mcheshi, mpole lakini upande wa pili, huyo jamaa alikuwa hatari hata zaidi ya Mafia.


Je, nini kitaendelea?
Tukutane kesho.
Hapa imekaa poa wadau kwenye kuunganisha au imezingua tena?
 
hapo sasa imekaa poa cyo kama mwanzo kila sehemu na thread yake twangoja sehemu ya5.
 
m
MWANAHARAMU WA KISIASA-04

Chris alikuwa mitaani na watoto wenzake, hakuwa na marafiki, mtu ambaye alikuwa naye kila alipokuwa alikuwa Ndezi tu ambaye kila wakati yeye ndiye aliytemwambia twende huku au kule, yeye ndiye aliyemkutanisha na watoto wengine na kumtambulisha.

Maisha hayo yalimuumiza mno, hakuamini kama katika safari ya kuelekea nchini Matapatapa na familia yake angejikuta akiwa mitaani huku akitafuta maisha. Kwa wakati huo, hakukuwa na mtu aliyejua kama Chris alikuwa mitaani, kwa Tanzania, walipata taarifa kwamba Bilionea Massawe aliiua familia yake lakini hawakujua mahali alipokuwa Chris kwa wakati huo.

“Chris! Unapokuwa kwenye tatizo ni lazima upambane kiume,” alisema Ndezi huku akimwangalia Chris.

“Kivipi?”
“Kuna ubabe mkubwa sana huku mtaani. Unaweza kupata pesa halafu kuna wajinga flani wakakufuata na kutaka kuchukua pesa zako, hivyo ni lazima upambane,” alisema Ndezi huku akimwangalia Chris.

“Kwa kupigana?”
“Hapana! Unaweza kupambana kwa kisu au hata bisibisi,” alisema Ndezi maneno yaliyomfanya Chris kushtuka kwani katika maisha yake hakuhisi kama ingetokea siku angeweza kuchukua kisu na kupambana na watu wengine.

Walikuwa wakizunguka huku na kule, walionekana kama watoto wa mitaani lakini kwa Chris alionekana kuwa tofauti na wenzake. Mavazi yake yalikuwa masafi na muda mwingi hakuwa mtu wa kuomba pesa kama ilivyokuwa kwa wenzake.

Saa zilikatika, mpaka vijana wa Rais Labad wanamuona mitaani hakuwa akijua, hakuwafuatilia kwani aliamini kwamba kwa kile kilichotokea mbugani, kisingeweza kuendelea mpaka mitaani.

“Tumfuateni!” alisema kijana mmoja, alikuwa akimwangalia Chris aliyekuwa na Ndezi katika Soko Kuu la Motown ambapo kulikuwa na idadi kubwa ya watu.

“Tusubiri mpaka atoke ndani ya soko!”
“Tunachelewa!”
“Ila tukimfuata, watu wengine watahisi vipi? Tena na hii hali ya watoto kutekwa na kuuawa si ndiyo itatuletea msala?” alihoji jamaa mmoja, alionekana kuwa na wasiwasi mkubwa.

Wenzake hawakutaka kumsikiliza, walijiona wao kuwa sahihi kuliko hata yeye, walichokifanya ni kuteremka kutoka ndani ya gari na kuanza kumfuata Chris aliyeendelea kuwa na Ndezi, walipomfikia, wakamsimamisha.

“Dogo mambo vipi?” aliuliza jamaa mmoja.

Chris hakujibu, alisimama na kuanza kuwaangalia watu hao, hakuwafahamu, alihisi labda wanaweza kuwa wale wanaume waliokuwa hotelini lakini hawakuwa wao, hakujua walihitaji nini, alisimama pamoja na Ndezi huku wakiwaangalia kwa mshtuko.

“Tuna kazi tunataka utusaidie,” alisema jamaa mmoja huku akimwangalia Chris.

“Kazi gani bro?” aliingilia Ndezi.

“Siyo wewe! Tunataka atusaidie huyu.”

“Mimi ndiye meneja wake, bila mimi haendi sehemu,” alisema Ndezi huku akiwaangalia wanaume hao nyusoni mwao.

Alikuwa kijana wa mitaani, mhuni asiyeogopa kitu chochote kile, kwa jinsi mtazamo alioutumia kuwaangalia wanaume hao ulionyesha kabisa kwamba hakuwa mtu wa mchezo hata kidogo.

Walichokifanya ni kuwaambia wawafuate kule walipokuwa wakielekea kwenye gari ambapo ndipo waliposema kwamba kulikuwa na mizigo, walipofika na kuufungua mlango, wakawaingiza wote na kisha kuufunga mlango.

“Tulieni humo ndani,” alisema mwanaume mmoja kwa sauti ya ukali, tena ya kibabe hasa.

Ndezi hakujua ni kitu gani kilikuwa kikiendelea mahali hapo lakini kwa Chris akagundua kwamba inawezekana watu hao walikuwa miongoni mwa wale vijana waliokwenda hotelini mule na kuwaua wazazi wake.

Akaingia na hofu na kuona kwamba huo ndiyo ungekuwa mwisho wake, akaanza kulia. Ndezi alikuwa kimya, aliwaangalia watu hao, waliwaweka nyuma ya gari lile huku huko wakiwa na mwanaume mmoja na wengine wawili wakiwa mbele.

Gari lilikuwa likiondoka kutoka ndani ya soko lile, kutokana na umati mkubwa wa watu, gari liliendeshwa kwa mwendo wa taratibu sana mpaka walipofika nje ya soko lile na ndipo dereva alipoongeza mwendo kuelekea kulipokuwa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Motown.

“Oya! Tunakwenda wapi huku?” aliuliza Ndezi huku akiwaangalia watu hao, hakujua kitu chochote kile, kwake, walionekana kuwa watekaji ambao waliwachukua kwa ajili ya kwenda kuwaua.

“Nyamaza nyambafu we’,” alisema jamaa waliyekuwa naye katika viti vya nyuma.

“Nitanyamazaje na wakati nataka kujua tunakwenda wapi,” alisema Ndezi lakini hata kabla hajakaa vizuri akashtukia akipigwa kibao kimoja cha nguvu shavuni mwake.

“Nimekwambia nyamazaaa…” alisema mwanaume ambaye walikuwa naye nyumba ya gari lile.

Ndezi akanyamaza, moyo wake ukajawa na hasira, hakuamini kama alipigwa kibao kizito namna ile, kwake, ile ilionekana kuwa dharau kubwa, hakuamini kama kungekuwa na mtu ambaye angediriki kumzaba kibao namna ile.

Mwanaume mmoja miongoni mwa wale waliokuwa mbele ya ile gari akampigia simu Rais Labad kwa ajili ya kumpa taarifa kwamba walifanikiwa kumpata Chris na muda huo walikuwa njiani kuelekea sehemu walipotakiwa kumuulia.

“Safi sana, muueni haraka iwezekanavyo halafu mwili wake muuzike porini,” alisikika kwenye simu kwa sauti ambayo watu wote ndani ya lile gari waliisikia.

Ndezi akajiangalia kwenye kiuno chake, kisu chake kilikuwa mahali hapo, alihisi kwamba safari hiyo ilikuwa mbaya na kama asingefanya jambo moja basi wangeweza kupelekwa sehemu na kuuawa.

Alichokifanya kwa haraka sana ni kukitoa kisu chake kisha kumchoma mwanaume walioyekuwa naye nyuma ya gari lile, hakumchoma mara moja, kwa haraka sana akamchoma mara tatu na kisha kuhamia kwa wanaume waliokuwa mbele ya gari.

Alianza na aliyekaa upande wa kushoto, akamchoma mara mbili kisu cha shingo, wakati dereva akigundua hilo na kutaka kumpokonya kisu kile, akashtukia naye akichomwa kisu cha shingo mara mbili tena kwa haraka sana.

Damu zikaanza kumtoka, akahisi kwamba mwili wake ukiishiwa nguvu, mikono yake ikaacha usukani na hapohapo gari likaacha njia na kuanza kuelekea bondeni kwa kasi kubwa.

“Jifunge mkanda,” alisema Ndezi na Chris kufanya hivyo harakaharaka.

Gari likaelekea bongeni ambapo huko likagonga mti mmoja mkubwa, likapinduka na wote wawili kuanza kuugulia maumivu mule garini walipokuwa.

“Chris…Chris….upo hai?” ailuliza Ndezi huku akimwangalia Chris aiyekuwa akitokwa na damu kwenye paji la uso.

“Nipo hai…koh koh koh,” alisema Chris na kukohoa mfululizo.

Hawakutaka kubaki mule, wakaanza kutoka. Ndezi hakutaka kukubali, alihisi kabisa kwamba watu wale walikuwa na pesa mifukoni hivyo akaanza kuwapekua.

Akawakuta na kiasi kikubwa cha fedha, akachukua simu zao na kuondoka katika eneo la tukio haraka sana kwani hawakutaka mtu yeyote awaone mahali hapo.

Wakati wakiwa njiani, ghafla simu moja ikaanza kuita, harakaharaka akaichukua na kuangalia kwenye kioo, jina aliloliona lilisomeka ‘Rais Labad’ akamuonyeshea Chris.

“Huyu amewaua wazazi wangu na dada yangu,” alisema Chris huku akionekana kuwa na hasira kali.

“Kumbe! Sasa wewe mtoto wa mbunge au?” aliuliza Ndezi.

“Pokea kwanza!”

Ndezi akaipokea simu ile na sauti ya Rais Labad ikaanza kusikika kutoka upande wa pili. Kitu cha kwanza kabisa alichouliza kilikuwa ni kazi yake aliyokuwa amewapa, je Chris alikuwa amekwishauawa na mwili wake kuzikwa au bado?

“Bado hajauawa kwa sababu tumewaua wao,” alijibu Ndezi huku akibadilisha sauti yake na kutaka isikike kama mtu mzima.

“Wewe nani?”

“Mshikaji mmoja hivi mtata.”

“Umepata wapi simu hii?”

“Nimewachukulia kisela. Ishu ni kwamba wana wamepata mzinga huku barabarani, kama vipi njooni mchukue miili yao ila kuanzia sasa usipige simu hii kwani ndani ya saa moja itakuwa imeuzwa kwa mtu mwingine kabisa,” alisema Ndezi.

“Wewe ni nani?”

“Daah! Rais unayumba sana! Nimekwambia msela flani hivi mtata lakini hunielewi! Wewe njoo uchukue maiti zako,” alisema Ndezi, hakutaka kuendelea kuongea, hapohapo akakata simu, akaizima, akatoa laini kisha kuiweka mfukoni na kuondoka mahali hapo akiwa na Chris aliyekuwa hoi, na muda wote alionekana kumuogopa Ndezi kwani hakuwahi kumuona mtu aliyekuwa na ushujaa wa kuwaua watu watatu kwa tukio moja kama alivyofanya ndani ya gari lile.

****

Rais Labad alichanganyikiwa, hakujua ni kitu gani alitakiwa kufanya, alipoambiwa kwamba baadhi ya vijana wake walikuwa wameuawa, alihisi moyo wake ukipata hasira kali ambayo hakuwahi kuipata katika maisha yake.

Kitu kilichomkasirisha zaidi kilikuwa ni simu aliyozungumza na mtu asiyemjua. Aliongea kihuni, maneno ya kejeli ambayo yaliufanya mwili wake utetemeke na kijasho chembamba kumtoka.

Hakutaka kukubali, alitaka kumuangamiza Chris kabla ya kuwaambia watu ukweli wa kile kilichokuwa kimetokea, akawapigia simu vijana wake wengine na kuwaambia kilichokuwa kimetokea, na kama ingewezekana basi waondoke kwenda kule kulipotokea ajali hiyo na kuangalia ni kitu gani kilitokea na wafanye juu chini, kama wahanga hawajafa, basi wawaue.

“Sawa mkuu!”

Hakutaka kuishia hapo, alijua kwamba kulikuwa na kazi kubwa kumpata Chris kwani mpaka hapo tu tayari aliona akisumbuka kumpata, akajua kwamba kama kweli gari lilipata ajali, basi inawezekana yule mtu aliyezungumza naye kwenye simu alikuwa rafiki wa Chris au mtu yeyote ambaye alikuwa akijua mahali Chris alipokuwa, hivyo mtu wa kwanza kabisa ilikuwa ni kumtafuta huyo mtu.

Akawapigia simu watu wa mitandao ya simu na kuwaambia kilichokuwa kimetokea, alitaka kujua mahali simu hiyo ilipokuwa, hata kama laini ya simu ingetolewa, aliamini kwamba bado simu hiyo ingeweza kufanya kazi, hivyo alihitaji kujua mahali ilipokuwa.

Hilo halikuwa tatizo, watu wa mitandao wakaingia kwenye kompyuta zao na kuanza kufanya kazi zao. Haikuwa kazi kubwa, kwa kuwa laini ya simu hiyo ilitumika katika simu iliyoibwa, wakaweza kuinasa mpaka mahali ilipokuwa hivyo kumpa taarifa.

“Mkuu! Tumeweza kuinasa simu yenyewe,” alisema kijana mmoja.

“Safi sana! Nitataka kijana mmoja aje, aongozane na vijana wangu mpaka mahali ambapo simu hiyo ilipokuwa,” alisema Rais Labad.

“Hakuna shida!”

Rais hakutulia, muda wote alikuwa akizunguka huku na kule, alichanganyikiwa, mtu aliyekuwa akimuumiza kichwa kwa wakati huo alikuwa Chris ambaye hakujua alikuwa mahali gani.

Alitaka kuficha siri juu ya kila kitu kilichotokea, kitendo cha kijana huyo kutokupatikana kilimaanisha kwamba angekuwa kwenye wakati mgumu sana, alitaka kuona akiuawa haraka iwezekanavyo ili kuifanya ile siri iendelee kuwa siri milele na milele.

Baada ya saa kadhaa vijana watatu wakafika mahali hapo, wakapewa vijana ambao walitakiwa kutangulizana nao kwa ajili ya kuifuatilia simu hiyo kwani ilikuwa ni lazima kumpata mtu aliyekuwa nayo kwa kuhisi kwamba ndiye aliyesababisha ajali au aliliona tukio hilo tangu mwanzo hivyo alikuwa mtu muhimu wa kutoa ushahidi.

Wakaondoka, yeye akabaki ikulu akiendelea kusikilizia kile kilichokuwa kikiendelea. Hakutulia, wakati mwingine hata simu za mawaziri hakuwa akizipokea kwani kile alichokuwa akikisubiria kilikuwa muhimu kuliko simu hizo.

Vijana wale kwa kutumia msaada wa GPRS wakaweza kuinasa simu hiyo. Ilionyesha kwamba ilikuwa katika Mtaa wa Mavizio ambao ulikuwa pembeni kidogo ya Mji wa Motown, mtaa uliokuwa uswahili ambapo kulikuwa na matuki makubwa yaliyokuwa yakitokea kila siku.

“We got him,” (tumemnasa) alisema jamaa mmoja, alikuwa akiwaambia wenzake kumaanisha kwamba GPRS ilisoma mahali alipokuwa mtu huyo.

Wakaanza kumfuatilia, haikuwa kazi nyepesi kwani hapo walipokuwa walitakiwa kuendelea na safari mpaka huko Mavizio kwa ajili ya kuonana na mtu huyo. Huko, walitakiwa kuwa wapole, walijua dhahiri matukio yaliyokuwa yakitokea huko hayakuwa ya kawaida, wanawake walibakwa, watu waliuawa, kulikuwa na matukio mengi yaliyokuwa yakitokea.

Hawakuchukua muda wakafika Mavizio, wakateremka kutoka garini na kuanza kufuatilia simu hiyo ilipokuwa ikionekana kwenye kifaa kidogo walichokuwa nacho. Kulikuwa na ugumu kwani kuifikia ilikuwa ni kupita katika vichochoro vingi, walikutana na wahuni lakini hawakuogopa kwani walikuwa na bastola ambazo zilionekana kama ulinzi kwao.

“Ipo kule mbele, tunaikaribia,” alisema jamaa mmoja wa mtandao wa simu.

Waliendelea kwenda mbele, watu walikuwa wakiwaangalia, kwa jinsi walivyoonekana, hawakuonekana kuwa watu wa kawaida hata kidogo, wengi walihisi kwamba walikuwa polisi waliokuja kumkamata mtu ila hawakutaka tu kuvaa sare. Waliogopwa, kila walipopita, wahuni wengine waliokuwa na bangi mikononi wakaingia ndani kujificha.

“Ni hapo nyuma,” alisema mwanaume mmoja, walikuwa wamekwishafika sehemu husika, kilichobaki ni kwenda mahali hapo kwani walizisikia sauti za watu wakizungumza kuhusu simu, wakajua ndiyo sehemu yenyewe.

****

Ndezi akakata simu, moyo wake ulikuwa kwenye furaha tele kwani alipata simu tatu za bure na hivyo mpango uliokuwepo ulikuwa ni kuziuza na fedha kufanyia mambo yake mengine. Akaondoka na Chris kwenda mitaani kabisa. Muda wote Chris alionekana kuwa na hofu, hakuamini kama yale mauaji makubwa yaliyofanywa yalifanywa na mtu kama Ndezi.

Umri wake na matendo aliyoyafanya vilikuwa vitu viwili tofauti, alionekana kuwa na umri mdogo lakini alikuwa na roho ya chuma, hakukubali kuona akionewa, hakukubali kuona akifanyiwa jambo lolote baya.

Walipoondoka hapo, wakaelekea katika Mtaa wa Mavizio, huko, alitaka kwenda kuziuza simu hizo. Walipofika, akaanza kuzitembeza huku na kule, alikuwa akimuonyeshea kila mtu aliyekuwa akikutana naye.

Zilikuwa simu nzuri, baada ya kuzitembeza kwa dakika kadhaa, akasimamishwa na mwanaume mmoja ambaye naye alizitaka simu hizo kwani kwa muonekano wake zilikuwa nzuri na isingekuwa rahisi kuziacha.

“Kiasi gani?”
“Hii laki mbili na nyingine laki laki,” alisema Ndezi hivyo mwanaume yule kumchukua na kumpeleka sehemu ambayo ilikuwa nzuri kufanya biashara hiyo ya wizi.

“Nakupa laki tatu zote!” alisema mwanaume huyo.

“Umeua bendi mzazi! Niachie jiwe tatu na nusu,” alisema Ndezi.

“Hiyo nyingi sana. Si unajua simu zenyewe za wizi hizi zimejaa magumashi, kama vipi kamatia tatu nisepe,” alisema mwanaume huyo, waliendelea kupatana bei pasipo kujua kwamba moja ya simu zile ilikuwa ikifuatiliwa.

“Tuondoke…” alisema Chris huku akionekana kuwa na hofu, macho yake hayakutulia, yalikuwa yakiangalia huku na kule..

“Subiri kwanza tupige mkwanja halafu tutasepa.”
“Ila nina hofu!”
“Ondoa hofu! Upo na komandoo,” alisema Ndezi huku akiwa na uhakika kwamba kila kitu kilikuwa salama kabisa.

***

Vijana wale walikuwa na uhakika kwamba watu waliokuwa nyuma ya nyumba ile ndiyo ambao walikuwa wakihitajika na Rais Labad hivyo walichokifanya ni kwenda nyuma ya nyumba ile.

Wakawakuta vijana watatu, baada ya vijana hao kuwaona, wakashtuka kwani hawakutegemea kuona wakifuatwa na watu kama hao ambao kwa kuwaangalia tu walionekana kuwa si watu wa utani hata kidogo.

Wakawaweka chini ya ulinzi na kuwapokonya simu, kitu cha kwanza kabisa kilikuwa ni kuwauliza kuhusu simu hiyo, walichowaambia ni kwamba waliinunua kutoka kwa kijana mmoja aliyekuwa na mwenzake.

“Kijana gani?”
“Dogo fulani, alinifuata na kusema kwamba anauza simu, tena alikuwa nazo tatu ambazo zote nilizinunua,” alijitetea kijana huyo.

“Yupo wapi?”
“Sijajua! Ni mtoto wa mitaani, hata nilipoona anauza simu nilijua angeniuzia kwa gharama nafuu, hivyo nikamlalia,” alijitetea kijana huyo.

Kwa kumwangalia tu ilionekana kuwa vigumu kuamini kama yeye ndiye aliyeiiba simu hiyo, alikuwa kijana mtanashati, alivalia shati jeupe na alichomekea.

Hawakuwa wakimuhitaji yeye, waliyekuwa wakimuhitaji alikuwa kijana ambaye aliiba simu hiyo lakini pamoja na hayo, hawakutaka kumuacha, wakamchukua yeye na wenzake na kuondoka nao mahali hapo.

Rais Labada akapewa taarifa juu ya kile kilichokuwa kimetokea, hakuamini kama kweli alishindwa kufanikisha kumpata kijana huyo ambaye aliamini kwamba alikuwa na Chris ambaye alikuwa akimtafuta kwa udi na uvumba.

Akawaambia vijana hao wawapige picha na kuwatumia ili kuona kama walikuwa wao au si wao, alivyotumiwa picha na kuziangalia, hawakuwa wao, hakumuona Chris na hata vijana hao walionekana kuwa wasafi kwani mtu ambaye alipokea simu alikuwa mhuni sana.

“Siyo hao!” alisema Rais Labad.

“Kwa hiyo hawa tuwafanye nini mkuu?”
“Waachieni ila wapokonyeni simu zote.”

Hilo ndilo lililofanyika, halikuhitaji maswali, wakafanya kama walivyoambiwa, wakawapokonya simu na kuwaambia wapotee, wakafanya hivyo.

Mitaani, vijana walikuwa wakihangaika huku na kule, kumpata Chris lilionekana kuwa jambo gumu, kwa kuwa alikuwa na mtandao mkubwa, Rais Labad akapeleka picha za Chris katika vituo vyote vya polisi na kuwaambia kwamba kijana huyo alitakiwa kutafutwa kimyakimya na picha zake zisitoke nje ya vituo hivyo.

“Sawa mkuu!”

Polisi wakaanza kumtafuta Chris mitaani, walikuwa na uhakika kwamba wangeweza kumpata kwani mbali na vituo ishirini vilivyokuwa katika Jiji la Motown, pia kulikuwa na polisi wengi ambapo kwa pamoja waliweka nguvu kwa mtu mmoja tu.

Wakaachana na mambo mengi, wakaacha kuwatafuta wavuta bangi, kipindi hicho ndicho biashara haramu ilipokuwa ikifanyika kwa nguvu zote kwani polisi hawakuwa na mpango wa kuwatafuta watu hao, wao walikuwa wameweka nguvu zao kumtafuta Chris tu.

Kila siku ilikuwa ni lazima kufikisha taarifa kwa mkuu wa kituo juu ya mahali walipofikia ambapo wao walimpigia simu Rais Labad na kumwambia kile kilichotokea.

Rais hakuamini kama kazi ingekuwa ngumu namna ile, aliamini kwamba kumkamata Chris haikuwa kazi kubwa kwa kuwa alikuwa hapohapo Motown, sasa ugumu ulitoka wapi?

Alikasirika! Aliendelea kuwasisitizia watu wake kwamba iwe isiwe ilikuwa ni lazima Chris apatikane kwani alijua hatari iliyokuwa mbele yake kama tu wasingehakikisha mtoto huyo anakamatwa.

Akaagiza ulinzi uongezeke mipakani kwani alijua kwamba kwa namna moja ama nyingine Chris angeweza kuondoka nchini Matapatapa kuelekea Tanzania ambapo huko angeweza kutoa ushahidi juu ya kile kilichokuwa kimetokea.

“Hakikisheni mipaka inaongezwa ulinzi na picha za huyo mtoto zinasambazwa huko mpaka apatinake! Mmenielewa?” alisema Rais Labad.

“Ndiyo mkuu!”

Hilo halikuhitaji kupoteza muda, haraka sana likafanyika, mipakani, picha zikapelekwa, ilikuwa ni lazima wamzuie Chris kama tu angetaka kutoroka nchi hiyo.

Hakutakiwa kufika nchini Tanzania kwa kuamini kwamba kama angefika huko ilikuwa ni lazima kukutana na waandishi wa habari na hiyo kuwaambia kilichokuwa kimetokea nchini Matapatapa.

Akaongeza vijana wake mitaani, polisi wote jicho lao likawa kumtafuta Chris, hawakujua alifanya nini wao walichokuwa wakikifanya ni kumfurahisha rais wao kwani bila kufanya hivyo waliogopa kupoteza kazi zao.

***

Ndezi alikubaliana na mnunuaji na kumuuzia simu zote alizokuwa nazo, akapewa kiasi cha laki tatu na kuondoka zake huku akifurahia, hakutaka kubaki na simu zile kwa kuamini kwamba zilikuuwa tatizo kwani angeweza kutafutwa na kukamatwa kwani simu aliyokuwa amepokea, ilimtisha.

Wakatafuta maji na kunawa, wakatafuta sehemu na kupumzika kwani walijiona kuwa na safari kubwa na bahati kubwa ajali ile haikuwa imewajeruhi kwa kuwa walikuwa katika siti za nyuma.

Hakujua sababu iliyomfanya Rais Labad kuwatuma watu na kuwakamata, aliamini kwamba yeye hakuwa na tatizo lolote bali mtu aliyekuwa na tatizo alikuwa Chris.

Alitaka kujua ukweli juu ya kitu kilichokuwa kikiendelea, alitaka kufahamu sababu iliyomfanya kutafutwa na mtu mzito kama Rais Labad. Akamuuliza lakini Chris hakumwambia ukweli, alimficha, kwa jinsi maongezi yake yalivyokuwa, Ndezi akahisi kwamba kulikuwa na tatizo.

“Niambie ukweli,” alisema Ndezi.

“Huo ndiyo ukweli! Mimi mwenyewe sijui!” alisema Chris.

Ndezi alikasirika sana, hakukuwa na kitu alichokuwa akikichukia kama kudanganywa, alimwambia Chris amwambie ukweli vinginevyo kama alikuwa akimdanganganya na siku moja kuujua ukweli basi kungekuwa na tatizo.

“Ni kwamba anataka kuniua!” alisema Chris.

“Najua! Ila nisichokijua ni kwa nini anataka kukuua,” alisema Ndezi.

“Ni kwa sababu aliwaua wazazi wangu!”
“Wazazi gani?”

“Wale waliouawa jana mbugani!”
“Unamaanisha bilionea Massawe aliyeiua familia yake jana?”
“Ndiyo huyohuyo ila hakuiua familia yake bali iliuawa na watu waliotumwa na rais huyo!” alisema Chris
“Na wewe ndiye huyo mtoto ambaye anatafutwa kila kona?” aliuliza Ndezi.

“Ndiyo!”
“Duuh! Kumbe nipo na brifukesi la pesa halafu sijui. Tufanye mishe tusepe hapa Motown, kushanuka, tusepee zetu Tanzania tukachukue huo mkwanja aliouacha baba yako,” alisema Ndezi huku akionekana kuwa na furaha.

Walikuwa na pesa, kiasi walichokuwa wamekipata waliamini kwamba kingewawezesha kufika nchini Tanzania. Kulikuwa na njia mbili za kufika huko, wangeweza kupitia mpakani auu baharini, walichochagua, kupitia mpakani ilikuwa rahisi zaidi.

“Hapa ni kuvuka boda mwana, hakuna jingine,” alisema Ndezi.

“Sawa.”
Walichokifanya ni kuchukua daladala iliyokuwa ikielekea Mabweni, Kusini mwa Jiji la Motown, kilometa mia nane kutoka hapo mjini. Huko ndipo kulipokuwa na mpaka wa kuingia nchini Tanzania.

Ndani ya daladala waliyochukua, walikuwa kimya. Kila mmoja alikuwa na mawazo yake, kwa Chris alikuwa akifikiria kufika salama nchini Tanzania lakini kwa Ndezi alichokuwa akikifikiria kilikuwa ni pesa tu.

Kitendo cha kuwa karibu na Chris alihisi kwamba yeye ni milionea mkubwa. Hakutaka kumuacha Chris, aliambatana naye na hata kama angepata matatizo pamoja naye, alikuwa radhi lakini mwisho wa siku apate kile alichokuwa akikitaka.

Hawakujua kwamba hata huko mpakani, kulikuwa na polisi waliokuwa wakiwatafuta kwa udi na uvumba.

***

Umati wa Watanzania ulikusanyika katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere kwa ajili ya kuipokea miili ya wanafamilia, Bilionea Massawe ambaye alikufa nchini Matapatapa.

Kila mtu alionekana kuwa na huzuni, wengi walilia, hawakuamini kama kweli bilionea huyo aliiteketeza familia yake kwa kuipiga risasi na kuwamaliza.

Mioyo yao iliuma na wengi kumlaumu kwamba hakutakiwa kufanya kitu kama kile, hata kama alikuwa na mawazo, hasira alitakiwa kuongea na watu wa ushauri na kumwambia nini cha kufanya.

Waandishi wa habari hawakukosa uwanjani hapo, kamera zao zilikuwa mikononi kwa ajili ya kupiga picha kila kitu kilichokuwa kikiendelea mahali hapo.

Ulionekana kuwa msiba mkubwa wa kitaifa kwani bilionea huyo alikuwa mtu wa watu, alipendwa, alikuwa na kampuni nyingi ambazo ziliwaajiri Watanzania wengi.

Viongozi wengi wa kisiasa walikuwa uwanjani hapo, bado hakukuwa na mtu aliyeamini, kila mmoja alikuwa akijiuliza kama iliwezekanaje mwanaume huyo akafanya mauaji hayo katika siku ya matembezi nje ya Tanzania badala ya kuyafanya mauaji hayo hapahapa Tanzania tena nyumbani kwake?

Huzuni ziliendelea kuwatawala, maswali mengi yaliendelea kuwatatiza vichwani mwao. Wengi walitaka kufahamu kuhusu Chris, hakuwa miongoni mwa watu waliouawa, alikuwa wapi na kwa nini hakuuawa? Wengi walitaka kulifahamu hilo.

Saa 4:18 asubuhi ndege iliyobeba miili ya marehemu hao ikaanza kuingia uwanja wa ndege. Vilio vilivyokuwa vikisikika mahali hapo, vikaongezeka zaidi, ndugu wengi walilia kwani hawakuwa wakiamini kama huo ndiyo ungekuwa mwisho wa kuwa na ndugu zao hao.

Ndege ilipotua, majeneza matatu yakatolewa ndani ya ndege na kisha kuanza kusukumwa kwa vyombo vilivyokuwa na mataili kuelekea kule kulipokuwa na umati wa watu.

Waandishi wa habari wakajisogeza kule na kuanza kupiga picha. Kilichokuwa kikiendelea mahali hapo kilimuumiza kila mmoja. Miili hiyo ikachukuliwa na kupelekwa nyumbani kwao.

Huko, umati mkubwa wa watu ulikuwa umekusanyika nyumbani hapo, watu walitaka kuona kitu gani kilikuwa kikiendelea kama kuhuzunika, walihuzunika na kulia sana.

“Jamani! Hivi kweli Massawe ameimaliza familia yake kweli?” aliuliza jamaa mmoja huku akionekana kutokuamini.

“Hata mimi mwenyewe nashangaa….jinsi jamaa alivyokuwa na furaha na familia yake kweli aliwezaje kuiangamiza? Nahisi si kweli, mimi mwenzenu naanza kuhisi kitu,” alisema msichana mmoja, alionekana kuwa na huzuni mno.

“Wewe ni kama mimi! Nahisi kuna mchongo umechezwa,” aliongezea mwanaume mwingine.

Kila mmoja alionekana kuwa na wasiwasi, walimfahamu Massawe, alikuwa miongoni mwa watu waliokuwa wakiipenda mno familia zao, kwenye mitandao ya kijamii na sehemu nyingine aliionyeshea kwamba ilikuwa kila kitu katika maisha yake.’

Kitendo cha taarifa kusema kwamba yeye ndiye aliyeiua familia yake kilimshangaza kila mmoja na kuhisi kwamba kulikuwa na kitu kilichokuwa kimetokea.

“Kuna kitu hapa.”
“Hata mimi nahisi hivyo!”

Hayo ndiyo maneno yaliyokuwa yakisikika msibani hapo, kila mmoja alihisi kwamba kulikuwa na mtu aliyeiangamiza familia hiyo lakini hakukuwa na mtu aliyejua kama familia hiyo iliangamizwa na Rais Labad.

Japokuwa alikuwa na matatizo nchini kwake lakini hakukuwa na mtu aliyefahamu kama watu hao walikuwa kwenye ugomvi mkubwa. Kutokana na kile kilichotokea, kila mmoja akahisi kwamba kulikuwa na bilionea ambaye alikuwa kwenye ugomvi na marehemu na kuamua kumfanyia unyama huo.

Polisi hawakutaka kubaki kimya, kwa kile kilichokuwa kimetokea kilikuwa kikubwa mno, ilikuwa ni lazima wafanye uchunguzi wa ndani kugundua ni kitu gani kilitokea, ni mtu gani alisababisha mauaji yale.

Walijua kwamba kama wangetaka ushirikiano na nchi ya Matapatapa wasingeweza kuupata kwani wao ndiyo waliotangaza kwamba mwanaume huyo aliiangamiza familia yake na mwisho kujimaliza yeye mwenyewe.

“Ni lazima tuliangalie jambo hili kwa undani, ni lazima tujue kila kitu kilichokuwa kimetokea,” alisema Kamanda Mkuu wa Jeshi la Polisi, IGP Mwalami, alikuwa akizungumza na polisi wenzake wa kitengo cha upelelezi.

Waliamua kuweka kikao hicho ambacho kiliwachukua dakika thelathini, mwisho kabisa wakamalizia kwa kumchagua Edson Mwalugonde, kijana machachari aende nchini MAtapatapa, kulekule kwenye Mbuga ya Kizwalinda kwa ajili ya kufanya upelelezi na kugundua ni kitu gani kilikuwa kimetokea mpaka bilionea huyo aiangamize familia yake.

Wakati wakimchagua Edson kwa ajili ya kuchunguza juu ya vifo hivyo, hakuwepo nchini Tanzania, alikuwa nchini Uingereza akifurahia maisha baada ya kukamilisha kazi ya kupeleleza kila kitu kilichotokea katika utekwaji wa watoto wengi nchini Tanzania. Kazi hiyo aliifanya na kuimamilisha, wahusika wakakamatwa, hivyo kuelekea nchini Uingereza kwa ajili ya kupumzika.

Alipopigiwa simu na kupewa taarifa ya kifo cha Bilionea Massawe, alichanganyikiwa, hakuamini kama bilionea huyo aliweza kuimaliza familia yake, kama watu wengine walivyohisi kwamba waliuawa ndivyo alivyohisi hata yeye mwenyewe.

Hakutaka kuendelea kukaa nchini Uingereza, alichokifanya, kwa haraka sana akaondoka kurudi nchini Tanzania, alipofika, akapewa kazi hiyo na kuambiwa kwamba alitakiwa kuelekea huko, katika mbuga hiyo kama mtalii kutoka nchini Nigeria, hilo halikuwa tatizo, akaahidi kufanya kazi hiyo kwa uadilifu mkubwa kabisa.

Kesho yake, saa 6:09 mchana alikuwa ndani ya ndege akielekea nchini Matapatapa. Kichwa chake kiliendelea kumfikiria Bilionea Massawe, alifahamu, mwanaume huyo alikuwa roho nzuri, aliipenda familia yake kuliko kitu chochote kile, kila alipokuwa akitafuta uwezekano wa bilionea huyo kuiteketeza familia yake, kitu hicho hakikuingia kabisa kichwani mwake.

“Hapa kuna kitu! Sidhani kama Bilionea Massawe anaweza kuiteketeza familia yake. Nahisi kuna kitu, na nitakijua tu,” alijisemea huku ndege ikikata mawingu kuelekea nchini Matapatapa.

Haikuchukua saa nyingi, ikafika huko. Akateremka na kukodi gari ambalo lilimpeleka mpaka katika mbuga hiyo. Ilikuwa vigumu kumgundua kama alikuwa Mtanzania, alizungumza Kiingereza kama Mnigeria, aliiga lafudhi hiyo na kila alipokuwa akizungumza, watu wengine hawakuelewa kutokana na Kiingereza chake kuwa na lafudhi ya Lugha ya Yoruba.

“Where are from?” (Umetoka wapi?) aliuliza mhudumu wa mapokezi.,

“Yoruba my friend,” (Yoruba rafiki yangu) alijibu Edson huku akichia tabasamu, kwa jinsi alivyoonekana, alikuwa mcheshi, mpole lakini upande wa pili, huyo jamaa alikuwa hatari hata zaidi ya Mafia.


Je, nini kitaendelea?
Tukutane kesho.
Hapa imekaa poa wadau kwenye kuunganisha au imezingua tena?
mpaka lini kaka? Tusimulizie sehemu zingine
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom