Mwanahalisi lashinda kesi.

Mwanahalisi lashinda kesi.

mwanahalisi huru? naaamini kuna mambo kedekede walikuwa wanayakusanya na kuyatafiti wakati limefungiwa hivyo naamini mengi tuyatarajie, karibu mwanahalisi uraiani

Halijafunguliwa bado,lakini limeshinda kesi ambayo kuna njemba moja inaishi.........ililishitaki.kwenye hiyo kesi Bwana niliwahi kumshuhudia mmoja wa watoa Ushahidi anaitwa Ndimara Tegambwage wakati anatoa ushahidi mbele ya mahakama,huyu ni mwandishi mkongwe na Mwanaharakati,jamaa ni hatari kweli anajieleza,alijieleza mbele ya hakimu mpaka akasema kwamba mahakama imepata darasa.
 
Mkuu,tulia sehemu moja usichezecheze,funguka.
 
msinishambulie jamani, nimeisikia kwa kifupi kwenye kipindi cha uchambuzi wa magazeti leo asubuhi, ni gazeti la tanzania daima limeandika habari hii. You can go for it!

kwanza jielezee jinsia yako
mbona una mambo ya kitoto kweny mambo nyeti hv.?!
Kama unawashwa c uende jukwaa la utan au umbea ukakunwe huko
 
Gazeti la mwanahalisi limeshinda kesi yake na mlalamikaji ameamriwa na mahakama kulipa gharama za kesi.
Chanzo: Tanzania Daima toleo la leo.

Kesi gani tena? kwani liliifikisha serikali mahakamani?
 
Msinishambulie jamani, nimeisikia kwa kifupi kwenye kipindi cha uchambuzi wa magazeti leo asubuhi, ni gazeti la Tanzania Daima limeandika habari hii. You can go for it!

Ingekuwa vizuri Mkuu anjnr kama ungelitafuta hilo gazeti ili kupata details na kuzimwaga hapa.. Unajua members wengi hawana access za kupata hayo magazeti..
 
Kesi ya kukashifu,iliyokuwa ikilikabili gazeti la mwanahalisi imetupipiliwa mbali na mdai ametakiwa kulipa gharama za kesi.

Hakimu mkkazi wa wa mahakama ya kisutu jijini Dar es salaam,Warilwande lema ,katika hukumu yake juzi jumatano amesema ili maneno yawe,au yaonekane kuwa ya kashfa,sharti yawe ama si ya kweli au yawe ya uongo.

Amesema kwa mujibu wa ushahidi uliotolewa mahakama haikuona chochote kile kilichodhibitisha madai ya kashfa.

Juma Jaffari Nyaingesha,mwenyekiti wa serikali ya mtaa Msewe jijini Dar es salaam ndiye alishitaki gazeti la mwanahalisi akidai kuwa kwa habari na makala zilizochapishwa katika matoleo yake matano alikashifiwa na kuvunjiwa heshima mbele ya jamii.


Mdai alishitaki muhariri wa gazeti Jabir Idrissa,mshahuri wa gazeti Ndimara Tegambwage,kampuni ya uchapishaji ya printech na kampuni nyingine ya uchapishaji ,Tanzania Standard printers limited.

Nyaingeshi alidai kuwa matoleo matano ya mwanahalisi yalikuwa na taarifa zilizomkashifu na kumuondolea hadhi mbele ya jamii,aliyataja matoleo hayo kuywa ni 10,12,24,31 oktoba 2007 na 14 okotba 2008.

Katika matoleo hayo kulikuwa na habari na makala juu ya madai ya kuwapo vitendo vya uhalifu msewe,ukosefu wa amani na matumizi mabaya ya madaraka ambavyo Nyaingesha alidai vilikuwa vinaelekezwa kwake.

Katika hukuku yake Hakmu Lema alisema kwanza mdai hakuleta hata shaihidi mmoja kudhibitisha madai yake na kwamba yeye mwenyewe hakudhibitisha kuwa amekashifiwa

Mwanahalisi ilikuwa ikitetewa na wakili maarufu Mabere Marando

SOURCE NIPASHE 8/2/2013 UKURASA WA 8
 
Kusemasema sana sio dili.TUmepewa chanzo,tukifuatilie tujue kw kina.Daima ucpuuze tetesi,zibebe zifanyie kazi kama una nia,kama huna nia TULIA.
 
Ninaamini Utarudi tu!

A1-MWANAHALISI-GAZETI+LA+MWANAHALISI-SAED+KUBENEA-TANZANIA+NEWSPAPERS-MAGAZETI+YA+TANZANIA-HABARI+ZA+TANZANIA-TANZANIA+NEWS-PRESS.JPG
 
mbona unakuwa kama hafisa masoko wa tazania daima...
so taarifa yako inatufanya tulitafute mtanzania daima
 
Habari hii hapa


MwanaHALISI lashinda kesi

na Mwandishi wetu

KESI ya kukashifu, iliyokuwa ikilikabili
gazeti la MwanaHALISI, imetupiliwa
mbali na mdai ametakiwa kulipa
gharama zote za kesi. Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama ya
Kisutu jijini Dar es Salaam, Warialwande
Lema, katika hukumu yake Jumatano,
alisema ili maneno yawe, au yaonekane
kuwa ya kashfa, sharti yawe ama si ya
kweli au yawe ya uongo. Alisema kwa mujibu wa ushahidi
uliotolewa mahakama haikuona chochote
kile kilichothibitisha madai ya kashfa. Juma Jaffari Nyaigesha, Mwenyekiti wa
Serikali ya Mtaa wa Msewe, jijini Dar es
Salaam ndiye alilishtaki gazeti akidai
kuwa kwa habari na makala
zilizochapishwa katika matoleo yake
matano, alikashifiwa na kuvunjiwa heshima mbele ya jamii. Mdai alimshtaki mhariri wa gazeti, Jabir
Idrisa, mshauri wa gazeti, Ndimara
Tegambwage, Stella Kajuna – mkazi wa
Msewe, mhariri mkuu, kampuni
inayochapisha gazeti, Hali Halisi
Publishers Limited, kampuni ya uchapaji ya Printech na kampuni nyingine ya
uchapaji, Tanzania Standard Printers
Limited. Nyaigesha alidai kuwa matoleo matano
ya MwanaHALISI yalikuwa na taarifa
zilizomkashifu na kumwondolea hadhi
mbele ya jamii. Aliyataja matoleo hayo kuwa yale ya 10,
12, 24, 31 Oktoba 2007 na 14 Oktoba
2008. Katika matoleo hayo kulikuwa na habari
na makala juu ya madai ya kuwepo
vitendo vya uhalifu Msewe, ukosefu wa
amani na matumizi mabaya ya madaraka
ambavyo Nyaigesha alidai vilikuwa
vinaelekezwa kwake. Katika hukumu yake, hakimu Lema
alisema kwanza mdai hakuleta hata
shahidi mmoja kuthibitisha madai yake
na kwamba yeye mwenyewe hakuweza
kuthibitisha kuwa amekashifiwa. Hata takwimu za kura za uchaguzi
alizopeleka mahakamani, zilionyesha
kuwa hata baada ya kuandika yaliyokuwa
yakitokea Msewe, katika uchaguzi
uliofuata alipata kura nyingi, jambo
ambalo lilikinzana na madai ya kukashfiwa. Hakimu alisema Jaffari ni kiongozi na
kile walichofanya waandishi kilikuwa ni
mjalizo halali na wa haki juu ya kiongozi
na uongozi wa umma na siyo kashfa. Alisema ameridhika na ushahidi
uliotolewa na walalamikiwa, ushahidi wa
maandishi kutoka kwenye kata na hata
kauli ya mdai kuwa mmoja wa
walalamikiwa alipigwa na kwamba yote
hayo yalidhihirisha umuhimu wa kilichoandikwa. MwanaHALISI ilikuwa ikitetewa na wakili
maarufu, Mabere Marando, wakati
Tanzania Standard Printers Ltd,
iliwakilishwa na wakili Audax
Kahendaguza Vedasto wote wa Dar es
Salaam. Kuhusu wachapaji wa gazeti, hakimu
alisema hawakuwa na hatia kwa kuwa
hawakutenda kashfa yoyote, kwa vile
hakuna kashfa iliyothibitishwa. Aidha hakimu alikubaliana na hoja
kwamba mchapaji anayefanya kazi
aliyopewa na kuirejesha kwa mhusika,
hawezi kuwa ametenda kashfa. Alipoulizwa Mkurugenzi Mtendaji wa
HaliHalisi Publishers, Saeed Kubenea, juu
ya hatua anayojiandaa kuchukua, alisema
hajakaa na wakili wake kupanga hatua
inayofuata.
 
Mwanaharisi na Raia Mwema wako jirani mita kumi nambili Mkanusha habari Salvatory Rweyemamu, sasa kaa chonjo tupate habari za ukweli kutoka viwandani Kinondoni - Mwinjuma
 
Ni kweli hukumu ilitolewa jumatano wiki hii.hongera Mwanahalisi,ngoja tusubiri na JK alifungulie kwa sababu alilisema sana huko Ethiopia,ingawa alidanganya na inavyoonekana alipotoshwa na wapambe wake.na hicho ndio kigezo tosha kabisa kwamba atatoa amri ya kuliachia.

Mara nyingi nimesikia jk kadanganywa na walio chini yake.JK hana ufahamu wowote ule,?Anasubiri tu kudanganywa kila mara? Nisadieni kwa hili.
 
Back
Top Bottom