Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,276
Samuel Mugarula, Mwanafunzi wa chuo kikuu cha Makerere nchini Uganda amevumbua njia ya kutengeneza mabomu ya kutoa machozi (Tear Gas) ambayo hutumika na vikosi vya polisi mara nyingi kuzima maandamano.
Mugarula 23, ambaye anayetarajiwa kuhitimu mwakani shahada ya kemia na utafiti wa mimea, alianza kutengeneza bomu la kutoa moshi wa machozi (Tear Gas) baada ya hapo Mugarula alifanya utafiti zaidi kutengeneza vilipuzi vingine, mfano bomu la moshi mkali na vibomu vidogo vidogo vya moto
"Imenichukua miaka mawili, nilianza mwaka 2014, na bomu la kutoa moshi wa machozi na nilipotoka na mafanikio ulikuwa ni mshangao mkubwa nilikuwa na furaha sana ndio maana niliendelea kufanya utafiti katika milipuko mingine"alisema
Mugarula anasema baadhi ya vifaa anavyotumia kutengeneza vilipuzi hivyo ni vifaa vya kawaida vinavyotumika majumbani, mfano sukari, hamira ya kuumua mikate, na vikorombozo vingine na sukari yenye sumu kali inayotengezwa maabara ambayo haitumiki majumbani.
Vikosi vya usalama nchini Uganda vimetaka kumkamata Mwanafunzi huyo anayemaliza kusoma mwaka huu kwa hofu ya kuhatalisha usalama wa Taifa.
Mugarula ana hofu kuwa huenda makundi ya kigaidi wakataka katumia ubunifu wake ndio maana aliweza kuwaandikia barua Waziri mkuu wa Uganda Dk. Ruhakana Rugunda, Waziri wa Elimu Janet Museveni na Mkuu wa polisi wa Uganda Jenerali Kale Kayihura akiwafamisha msimamo wake kutaka kushirikiana kwa pamoja na serikali ya Uganda katika utafiti wake
Mugarula kwa sasa habari zake zimefika kwa Rais wa Uganda na amealikwa rasmi kukutana na Rais Yoweri Kaguta Museveni
Chanzo : BBC
"Imenichukua miaka mawili, nilianza mwaka 2014, na bomu la kutoa moshi wa machozi na nilipotoka na mafanikio ulikuwa ni mshangao mkubwa nilikuwa na furaha sana ndio maana niliendelea kufanya utafiti katika milipuko mingine"alisema
Mugarula anasema baadhi ya vifaa anavyotumia kutengeneza vilipuzi hivyo ni vifaa vya kawaida vinavyotumika majumbani, mfano sukari, hamira ya kuumua mikate, na vikorombozo vingine na sukari yenye sumu kali inayotengezwa maabara ambayo haitumiki majumbani.
Vikosi vya usalama nchini Uganda vimetaka kumkamata Mwanafunzi huyo anayemaliza kusoma mwaka huu kwa hofu ya kuhatalisha usalama wa Taifa.
Mugarula ana hofu kuwa huenda makundi ya kigaidi wakataka katumia ubunifu wake ndio maana aliweza kuwaandikia barua Waziri mkuu wa Uganda Dk. Ruhakana Rugunda, Waziri wa Elimu Janet Museveni na Mkuu wa polisi wa Uganda Jenerali Kale Kayihura akiwafamisha msimamo wake kutaka kushirikiana kwa pamoja na serikali ya Uganda katika utafiti wake
Mugarula kwa sasa habari zake zimefika kwa Rais wa Uganda na amealikwa rasmi kukutana na Rais Yoweri Kaguta Museveni
Chanzo : BBC