Mwana wa Osama bin Laden asakwa na Marekani

Mtoto wa Osam Bin Laden, Hamza Bin Laden ajiunga na Al Qaeda-BBC SWAHILI
Sasa anatakiwa yeye ndio awe mstari wa mbele. ajifunge bomu kwanza, asiwe kama chadema ya mbowe ambaye yeye hutuma tu wafuasi waandamane halafu yeye anakaa chumbani ana angalia TV.
 
Sasa anatakiwa yeye ndio awe mstari wa mbele. ajifunge bomu kwanza, asiwe kama chadema ya mbowe ambaye yeye hutuma tu wafuasi waandamane halafu yeye anakaa chumbani ana angalia TV.
Hahahahaaaaaaaaaa wanasema Jambazi kuu hufa mwishoni
 
View attachment 454966
Mwana wa Osama bin Laden aorodheshwa na Marekani miongoni mwa magaidi wanaosakwa na Marekani

Marekani imesema kuwa imemuorodhesha mwana wa mwisho wa Osama Bin Laden, Hamza, katika orodha ya magaidi wanaosakwa na taifa hilo.

Wizara ya mambo ya nje ya Marekani imesema kuwa Hamza Bin Laden ameanza kushiriki katika maswala ya kundi la al Qaeda, kundi la jihad lililofadhiliwa na babake.

Amesema kuwa atalipiza kisasi mauaji ya babake yaliotekelezwa na kikosi maalum cha Marekani kwa kutekeleza mashambulizi dhidi ya Wamarekani.
Sasa atapigwa marufuku kwa kufanya biashara na raia wa Marekani huku mali yake ikipigwa tanji.

Mamake Hamza ni Khairiah Sabar, mmoja wa wake za Osama aliyekamatwa wakati wa shambulio la wanajeshi wa Marekani kwenye maficho ya Osama mjini Abbotabad nchini Pakistan mwaka 2011.

Mkuu wa kitengo cha usalama cha kundi la al-Qaeda Ibrahim al-Banna pia ameongezwa katika orodha hiyo .

Marekani imetoa kitita cha dola milioni 5 kwa mtu yeyote atakayemkamata al-Banna.

Hamza bin Laden alitambuliwa kuwa mmoja wa viongozi wa al-Qaeda mwaka 2015 na baadaye akaapa kulipiza kisasi mauaji ya babake mwezi Julai mwaka uliopita.

View attachment 454965
Hamza bin Laden, kulia, alipokuwa bado mdogo kwenye kanda ya video iliyopigwa mwaka 2001

Katika ujumbe wa sauti wa dakika 21 wenye kichwa "We Are All Osama," (Sote ni Osama), na uliochapishwa katika mitandao, aliapa lazima angelipiza kisasi mauaji ya babake mwaka 2011 nchini Pakistan.
''Tutaendelea kuwasaka na kuwapiga popote pale mtakapokuwa mumejificha ati nyuma ya pazia za usalama kwa maovu munayoyaendeleza ,Palestina, Afghanistan, Syria, Iraq, Yemen, Somalia na kote kwenye ardhi ya waislamu mnayokalia,'' shirika la habari la Reuters lilimnukuu.

''Na kwa wale wanaodhania kuwa tutakuwa tukilipiza kisasi mauaji ya Osma ole wenu, kwanini sisi tutakuwa tukilinda dinia ya kiislamu'' alisema Hamza.

Hamza, kulingana na wachanganuzi, alitambulishwa na kiongozi wa kidini wa kundi la al-Qaeda Ayman al-Zawahiri katika ujumbe huo uliolenga kuwavutia vijana ambao kwa sasa wamejiunga kwa wingi na kundi la Islamic state.

Hamza sasa anaungana na nduguye wa kambo, Saad, kuwa miongoni mwa watu wa jamii ya Osama walioorodheshwa kuwa magaidi.




Wanaoamini hizi habari ni kama hawa waliokubali kugeuzwa sakafu

b35e1b8c90aa5543dc18de9941c954de.jpg
 
Back
Top Bottom