Mwana CCM jitafakari

Mwana CCM jitafakari

Criss

JF-Expert Member
Joined
Mar 19, 2011
Posts
1,944
Reaction score
3,090
Yawezekana wewe ni mstaafu , uliyewahi kulitumikia Taifa kwa moyo wako wote.

Yawezekana bado upo kwenye madaraka na bado unazitii order zote nakukiombea mema chama chako kiendelee kutawala.

Yawezekana wewe ni mwanachama wa kawaida unaeshiriki kupambana kuwabagaza wapinzani kwa uwezo wako wote .

Yawezekana wewe na wale waliyoupande wapili kunakipindi mliwahi kuwa upande mmoja aidha ndani au nje ya mfumo uliyomo wewe kwa sasa .

Kwa upole kabisa nakuuliza .

Wewe mwanaccm mwenzangu kwenye hili sakata la #Polepole unefanikiwa kujifunza nini?

Yawezekana ukasema kaponzwa na kamdomo kake , siyo?

Unaamini wewe siku zote utaweza kuishi kwenye uelekeo wautakao?

Unaamini ndugu na watoto wako wataweza kuishi kwenye uelekeo wautakao?

Jiulize , ikiwa adhabu za kila atakae kengeuka iwe ni hii iliyomkuta Polepole ,wewe umejiandaaje?

Hebu fumba macho kisha jiulize ,Unautazama uelekeo wa Taifa lako kwa sura gani?

Bilashaka unaiona picture ya Taifa la mazombie ,au wewe unaonaje? Litakuwa Taifa la watu wasiyo na uwezo wakuchalange chochote , yeah ,ndiyo , maana atakaechalange atatoka wapi? Hadithi za waliyochalange zitakuwa zimejazwa vichwani mwao , majina ya kina Polepole ,Soka ,Mdude ,Mawazo ,Sativa ,Ben Saa nane na wengine wengi yatatumika kama fimbo za kuwaangamiza kiroho .

Lakini tujiulize , kwanini hatuna upendo na Taifa letu?

CCM ni chama cha siasa tukipendacho kweli kweli lakini kama kweli tunakipenda ,kwanini tusiwasihi viongozi wetu wakashiriki uwepo wa katiba ambayo haitatuelekeza kubaya ili hata tutakapostaafu bado tuendelee kuwa salama ?

Kwanini tusiwaombe viongozi wetu wakatengeneza mazingira yanayotambua haki na kumthamni kila Mtanzania bila upendeleo?

Ikiwa vyote ni upuuzi , hivi tunamjua aliye nyuma yetu?

Tumejiandaa vyakutosha kuja kuinywa dawa tunayoshiriki kuikoroga?

Muwe na wakati mwema .
 
Mazingira yanapumbaza sana , ipo siku tutasema free Mzee mkubwa yule ambae sasa ndiyo ring leader hapo ndipo tutakapojua kumbe kweli Dunia haina mwenyewe hii
 
Mimi nina kadi ya ccm! Ila siungi mkono Wahuni wachache kujimilikisha chama na nchi. Hili jambo halikibaliki hata kidogo. Hii nchi ni mali ya wananchi wote! Na siyo mali ya Wahuni wachache.

##Kataa Wahuni, okoa Taifa##
 
Mimi sio mwanaccm na sijawahi kuipenda ccm japo familia ninayotoka mzazi wangu mmoja ambaye kwa sasa ni marehemu alikuwa ni nwanaccm kindaki ndaki kiasi cha kutaka na mimi niwe mwana ccm..!!

Naamini kabisa kwa hii ccm ya sasa hivi asingethubutu hata kuvaa kanga ya chama wala kuudhuria mkutano wowote wa ccm, maana matukio yanayofanywa na ccm hii ya Samia ni aibu kwa mtu yeyote mwenye ubinadamu...!!

Kuhusu hili tukio la Polepole, naona comments nyingi za wanaccm wakioneshwa kufurahishwa nalo... tafsiri yake ni kwamba hawajajifunza chochote.

Ni wazi kabisa sasa hivi sifa kuu ya kuwa mwanaccm ni lazima roho ya ubinadamu ikitoke, na kisha uvae roho ya kishetani na unafiki. Na uwe tayari kumuua mtu yeyote anayeenda kinyume na matakwa ya malaika mkuu.

Nina uhakika zaidi ya 98% ya wanaccm wa sasa na hasa UVCCM hawajui hata misingi ya hiki chama tangu kuanzishwa kwake ni ipi.

Mara kadhaa nimeona UVCCM wanamtukana Mwalimu Nyerere tena kwa sababu za kipuuzi sana, na kuna wengine wanasema hivi vyama vya upinzani havitakiwi kuwepo... sasa hao ni watu kweli?

Hiki chama kimeshakuwa laana kwenye taifa letu.
 
Back
Top Bottom