Mtu kwao anatunzwa, hata kama hana dini,
Mtu kwao anatunzwa,ili apate thamani,
Mtu kwao anatunzwa, mfanowe halingani,
Nyerere kweli mwalimu, kwa mengi alotufunza
Uongozi msimamo, bila kutaka makuu,
Uongozi ni masomo, uwezo uwe wa juu,,
Uongozi mitizamo, yenye tija na nafuu,
Nyerere kweli mwalimu, kwa mengi alotufunza
Tanzania uliyounda,haikujari ni nani,
Wote uliwapenda, kama watoto nyumbani,
Sheria hukuzipinda, ili tukujue nani,
Nyerere kweli mwalimu, kwa mengi alotufunza
Nchi ulivyoipenda, tena na kuithamini,
Nchi yako ukalinda, kwa akili na makini,
Pamoja na kukuwinda, ila ulijiamini,
Nyerere kweli mwalimu, kwa mengi alotufunza
Leo tunakukumbuka, kama shujaa makini
Toka umetuondoka, mambo hayawezekani,
Kama ungeliamka, usingeweza amini,
Nyerere kweli mwalimu, kwa mengi alotufunza
Leo tumekusaliti, kama hatuwa wako,
Toka upate mauti, ni kama haukuwako,
Tumeuza hata miti, ya pale shambani kwako,
Nyerere kweli mwalimu, kwa mengi alotufunza
Ulale pema peponi, mwalimu shujaa wetu,
Tuliopo humu ndani, twakumbuka enzi zetu,
Ujamaa vijijini, kauli na mbiu yetu,
Nyerere kweli mwalimu, kwa mengi alotufunza
We must never cease from exploring. At the end of all exploring, will be to arrive at where we began and know the place for the first time