Mwalimu wa Hesabu Form 4 Kibosho Girls Atafelisha Watoto Mwaka huu 2014

j2chenga

JF-Expert Member
Dec 21, 2012
201
61
Ndugu wana jamvi,

Mimi kama mzazi mwenye mtoto anayesoma Shule ya Sekondari ya wasichana Kibosho, nina wasiwasi sana na ufaulu wa watoto kwa somo la hesabu kidato cha nne mwaka huu 2014. Matokeo ya watoto waliopo kidato cha nne mwaka huu yamekuwa hayaridhishi kwa kipindi cha miaka mitatu mfululizo na pre mock ya mwaka huu watoto wamepata hadi asilimia 12%!

Mkuu wa shule haonyeshi kustushwa na matokeo haya lakini nina wasiwasi kwa mara ya kwanza shule ya wasichana ya Kibosho itatoa division 4 na 0 wengi kwa sababu ya somo la hesabu kuwa tatizo. Mkuu wa shule malengo yake ni kufuta division 3 ili ibaki 1 na 2. Hilo litawezekanaje wakati watoto walipata hadi asilimia 6%? kwa somo la hesabu kwa mtihani wa mwisho wa mwaka 2013?

Kwa utamaduni wa Kibosho, mwalimu wa hesabu huanza na watoto kidato cha kwanza na kwenda nao hadi kidato cha nne. Kulingana na matokeo ambayo tumeyashuhudia tangu mwaka jana (2013), mwalimu huyu wa hesabu anawapeleka watoto korongoni. Angalia matokeo haya ya mwaka jana (form 3) ambao sasa wapo kidato cha nne:A=0, B=8, C=24, D=36 na F=83. Haya matokeo ni mabaya mno kwa shule kama Kibosho. Hapa huwezi kusema watoto hawa wote ni wajinga kuliko mwalimu wao. Mwalimu ana tatizo. Mtoto anapata 6 au 12 hesabu wakati masomo mengine anapata A. Huyu mtoto huwezi kusema kwamba hana uwezo. Inawezekana anakatishwa tamaa na ufundishaji,

Japo kuwa muda umekwenda, kwa hawa waliopo kidato cha nne wakijiandaa na mitihani yao ya mwisho, naamini nafasi bado ipo ya hali hii kuangaliwa kwa makini angalau kunusuru aibu hii inayoenda kuonekana. Mwaka jana kwenye kikao cha wazazi Msimbazi Centre wazazi waliliongelea hili kwa uchungu lakini bado linanendelea kuonekana.

Kwakuwa hili suala ni la muhimu sana mjadala uendelee na uwafikie viongozi mbalimbali kama mwenyekiti wa bodi ya shule ili naye ahoji hili kwa undani zaidi na kumbana Mkuu wa shule. Naomba tuache mambo ya kejeli na mzaha kwenye hili suala.
 
sielewagi kwann wazazi wanalalamikaga saaana juu ya waalimu..................
ivi kazi ya kumsomesha mtoto ni ya mwl peke yake?? je wewe mzazi mwaka juzi umeona hali mbaya ukauchuna kisa sio wako, mwaka jana hivyo hivyo sasa leo ndo unaamka kisa wako ni mhanga??

kama alifelisha waliopita acha na wako afeli manake hakuna tofauti kati ya waliofeli mbeleni na huyu wakwako atakayefeli sasa.
 
Hivi mkuu wa Shule ni Sister nani....??? Alikuwaga Sister Edmundina....

Aisee...ni tatizo kubwa...Ni vuzuri ukawasaliana na mkuu wa shule ukaongea nae...

Kibosho Girls ni shule nzuri sana....Mdogo wangu alimaliza hapo mwaka 2007 akatoka na Div I.10 (Alipata Phy A, Chem A , Bios A na Math A)....Advance akapiga St. Mary Gorett akatoka na Div I. 9 (PCM)

Anamalizia Degree yake ya Computer Engineering mwaka huu....
 
Inaonekana wewe ni mwalimu katika hiyo shule kwani maelezo yako yamekaaaa kichonganishi, hata Kama kuna ukweli ila umewakilisha mada yako kwa chukii na uchonganishi, inawezekana una bifu huyo ticha au unamchongeaa ili afikuzwe kazi, fanya yako ndugu fitina hazina tija!
 
Katika mafunzo ualimu huwa hakuna somo linaloitwa 'kufaulisha mtoto'. Aidha ktk vipengele vya upimaji kwa walimu tarajali huwa hakuna kipengele kinachoitwa "uwezo wa kufaulisha mtoto". Hivyo siyo kazi ya MWL kufaulisha mtoto, hakusomea hicho kitu.
 
Hivi mkuu wa Shule ni Sister nani....??? Alikuwaga Sister Edmundina....

Aisee...ni tatizo kubwa...Ni vuzuri ukawasaliana na mkuu wa shule ukaongea nae...

Kibosho Girls ni shule nzuri sana....Mdogo wangu alimaliza hapo mwaka 2007 akatoka na Div I.10 (Alipata Phy A, Chem A , Bios A na Math A)....Advance akapiga St. Mary Gorett akatoka na Div I. 9.....

Anamalizia Degree yake ya Computer Engineering mwaka huu....

Habari za siku mme mwenza, mzima mke wetu Madam B?

Mkuu umefanya masifa kama ya kina Rweyemamu ndio hawachelewagi kushusha CV!!
 
Last edited by a moderator:
sielewagi kwann wazazi wanalalamikaga saaana juu ya waalimu..................
ivi kazi ya kumsomesha mtoto ni ya mwl peke yake?? je wewe mzazi mwaka juzi umeona hali mbaya ukauchuna kisa sio wako, mwaka jana hivyo hivyo sasa leo ndo unaamka kisa wako ni mhanga??

kama alifelisha waliopita acha na wako afeli manake hakuna tofauti kati ya waliofeli mbeleni na huyu wakwako atakayefeli sasa.

umemjibu ipasavyo, hata mimi nilitaka kumjibu hivihivi.!
 
Hivi mkuu wa Shule ni Sister nani....??? Alikuwaga Sister Edmundina....

Aisee...ni tatizo kubwa...Ni vuzuri ukawasaliana na mkuu wa shule ukaongea nae...

Kibosho Girls ni shule nzuri sana....Mdogo wangu alimaliza hapo mwaka 2007 akatoka na Div I.10 (Alipata Phy A, Chem A , Bios A na Math A)....Advance akapiga St. Mary Gorett akatoka na Div I. 9.....

Anamalizia Degree yake ya Computer Engineering mwaka huu....

na wewe ulipata ngapi?
 
usiogope sana, unaweza kuta mwalimu ana utaratibu wa kutunga mtihani mgumu, personally nlipataga A ya necta mathematics ila pepa za ndani zilikuwaga tight mbaya, unaweza pata 34 ukawa wa 13 kati ya watu 78, ila mwisho wa siku 42 students tulipata A, hakukuwa na F hata moja.

Kuna walimu pepa zao za math hazisoviki, ila yote hiyo ni kumjenga mwanafunzi awe na uwezo wa kupambana na mtihani wa aina yeyote ile.
 
Habari za siku mme mwenza, mzima mke wetu Madam B?

Mkuu umefanya masifa kama ya kina Rweyemamu ndio hawachelewagi kushusha CV!!

Dahhh....Mkuu ni longi sanaaa!!! Hivi upo..?? Dahh....

Unajua mleta mada inaonekana anataka kuichafua hii shule sasa bila kuweka record sawa atakatisha watu tamaa...

Mkuu mm nipo bana...nafurahi kukuona tena..
 
Last edited by a moderator:
Dahhh....Mkuu ni longi sanaaa!!! Hivi upo..?? Dahh....

Unajua mleta mada inaonekana anataka kuichafua hii shule sasa bila kuweka record sawa atakatisha watu tamaa...

Mkuu mm nipo bana...nafurahi kukuona tena..

Nipo mkuu,kuna mambo yaliniweka bize mno nikawa humu naingia kwa machale.

Nimeingia CC leo nikakutana na sura mpya kibao nikapita kimya kimya, maana babu Asprin na chairman wa milele (kama Mugabe) Baba V hawachelewi kukutia adabu mule usipowapa heshima..

Ila I am back again mkuu.
 
Last edited by a moderator:
sielewagi kwann wazazi wanalalamikaga saaana juu ya waalimu..................
ivi kazi ya kumsomesha mtoto ni ya mwl peke yake?? je wewe mzazi mwaka juzi umeona hali mbaya ukauchuna kisa sio wako, mwaka jana hivyo hivyo sasa leo ndo unaamka kisa wako ni mhanga??

kama alifelisha waliopita acha na wako afeli manake hakuna tofauti kati ya waliofeli mbeleni na huyu wakwako atakayefeli sasa.
Nashangaa...wanalaumu walim wakat watoto wao walishajua kilicho ndani ya surual? Watoto wa karne hii ni majanga msilaumu waalim was watu. Mzazi mwenyewe ukute umeshindwa kumsema mwanao mwalim ndo ataweza?
 
Inaonekana wewe ni mwalimu katika hiyo shule kwani maelezo yako yamekaaaa kichonganishi, hata Kama kuna ukweli ila umewakilisha mada yako kwa chukii na uchonganishi, inawezekana una bifu huyo ticha au unamchongeaa ili afikuzwe kazi, fanya yako ndugu fitina hazina tija!
Mwambie majungu so mtaji
 
Nashangaa...wanalaumu walim wakat watoto wao walishajua kilicho ndani ya surual? Watoto wa karne hii ni majanga msilaumu waalim was watu. Mzazi mwenyewe ukute umeshindwa kumsema mwanao mwalim ndo ataweza?

nimekuwa kwenye hii industry for a while sasa nimezoea kuona wazazi wakilaumu waalim ilihali wao wenyewe hawatake minitiative zozote kuhakikisha kwamba watoto wao wanaongeza bidii katika elimu. mzazi huyu analalamika utakuta kila siku anaimba wimbo wa mwl wa hesabu ni mbaya sana tena anauimba na mtoto unategemea mtt asemeje ama afanyeje??

sikumbuki siku mzazi wangu aliawah kumnanga mwl mbele yangu, lkn wazazi wa kileo eti ndo kuwapenda watoto wao kila kukicha ni kuwateta waalimu wa watoto wao hadi watoto wanajenga jeuri kwa waalimu unategemea nini??
 
nimekuwa kwenye hii industry for a while sasa nimezoea kuona wazazi wakilaumu waalim ilihali wao wenyewe hawatake minitiative zozote kuhakikisha kwamba watoto wao wanaongeza bidii katika elimu. mzazi huyu analalamika utakuta kila siku anaimba wimbo wa mwl wa hesabu ni mbaya sana tena anauimba na mtoto unategemea mtt asemeje ama afanyeje??

sikumbuki siku mzazi wangu aliawah kumnanga mwl mbele yangu, lkn wazazi wa kileo eti ndo kuwapenda watoto wao kila kukicha ni kuwateta waalimu wa watoto wao hadi watoto wanajenga jeuri kwa waalimu unategemea nini??

gfsonwin siku hizi mwalimu haruhusiwi kumgombeza mtoto ukifanya hivyo moto wake kutoka kwa mzazi utajuta kibarua chako, mwalimu na mwanafunzi wanaishi kama washkaji...yakija kutokea ya kufeli eti mzazi anakimbilia JF kulalamika. mzazi kama huyu kuna nati imelegea kichwani si bure. wawaache waalim wa watu wapumue
 
Last edited by a moderator:
Sio kwamba watoto wenu wameconcetrate zaidi fesibuku na c kwny masomo?hesabu somo gumu bana bila juhudi binafsi za mwanafunZi kufeli muhimu!!msilaumu walimu bure
 
Hivi mkuu wa Shule ni Sister nani....??? Alikuwaga Sister Edmundina....

Aisee...ni tatizo kubwa...Ni vuzuri ukawasaliana na mkuu wa shule ukaongea nae...

Kibosho Girls ni shule nzuri sana....Mdogo wangu alimaliza hapo mwaka 2007 akatoka na Div I.10 (Alipata Phy A, Chem A , Bios A na Math A)....Advance akapiga St. Mary Gorett akatoka na Div I. 9 (PCM)

Anamalizia Degree yake ya Computer Engineering mwaka huu....

Tendo muongo mdogo wako si yupo maeda bar akiwa kama muosha vyombo
 
Back
Top Bottom