mwanachuo
Member
- Jan 15, 2013
- 40
- 38
Naibu Katibu Mkuu Chadema amemshauri Mbunge wa Jimbo la Moshi Mjini Priscus Tarimo asijaribu kutumia kiinua mgongo chake kwenye kampeni za uchaguzi kwani katika kipindi chake chote hakuna alichokifanya zaidi ya kupeleka lami kwa baba yake na kudandia miradi isiyo muhusu ambayo imetekelezwa na serikali kuu huku miradi yake ya Stendi ya mabasi Nganga mfumuni, soko la mbuyuni, manyema na uchafu uliokithiri sambamba na uchakavu wa miundombinu ambayo hata mfuko wa Jimbo ameshindwa kuusimamia kufanya ukarabati.
Ameyasema hayo wakati wa mkutano wa Hadhara wa operation 255 uliofanyika katika viwanja vya manyema mjini Moshi.
Naye Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya kaskazini ndugu Lema amesema Moshi hakuna Mbunge Kuna Boya tu ambalo Kila neno ni ndiyo ndiyo. Hali iliyoamsha kelele na shangwe kwa Wana Moshi waliojaa kwenye mkutano huo.
Nini maoni yako
Ameyasema hayo wakati wa mkutano wa Hadhara wa operation 255 uliofanyika katika viwanja vya manyema mjini Moshi.
Naye Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya kaskazini ndugu Lema amesema Moshi hakuna Mbunge Kuna Boya tu ambalo Kila neno ni ndiyo ndiyo. Hali iliyoamsha kelele na shangwe kwa Wana Moshi waliojaa kwenye mkutano huo.
Nini maoni yako