LILENDI
JF-Expert Member
- Oct 27, 2013
- 1,400
- 496
Mwalimu mmoja wa darasa la tatu alitoa maelekezo darasani:
MWALIMU: Haya watoto wazuri, kila mmoja wenu achukue kalamu na karatasi kisha achore picha ya gari linalotembea, sawa?
WANAFUNZI: Sawa, mwalimu.
Baada ya muda mfupi mwalimu akawa anapita kila dawati kuangalia picha zilizochorwa. alipofika mwishoni mwa darasa akastaajabu alichokiona kwa mwanafunzi mmoja:
MWALIMU: (kwa ukali kidogo) Wewe... mbona umechora mawingu tu hapo kwenye karatasi?
MWANAFUNZI: Mwalimu, nilichora picha ya gari linalotembea hapa lakini limeshapita. unachokiona ni vumbi!
MWALIMU: Haya watoto wazuri, kila mmoja wenu achukue kalamu na karatasi kisha achore picha ya gari linalotembea, sawa?
WANAFUNZI: Sawa, mwalimu.
Baada ya muda mfupi mwalimu akawa anapita kila dawati kuangalia picha zilizochorwa. alipofika mwishoni mwa darasa akastaajabu alichokiona kwa mwanafunzi mmoja:
MWALIMU: (kwa ukali kidogo) Wewe... mbona umechora mawingu tu hapo kwenye karatasi?
MWANAFUNZI: Mwalimu, nilichora picha ya gari linalotembea hapa lakini limeshapita. unachokiona ni vumbi!