Mwalimu akutwa kichakani akiwa amefariki

real G

JF-Expert Member
Feb 7, 2013
5,227
5,287
Mwalimu wa shule ya msingi Lupapila iliyopo kata ya Subira Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma Christopher Ndimbo (29) amekutwa amefariki baada ya kukatwakatwa sehemu mbalimbali za mwili wake na kitu chenye ncha kali

Kamanda wa polisi mkoa wa Ruvuma Zuberi Mwombeji alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema mwalimu huyo aliuawa na watu wasiojulikana na pia walichukua pikipiki yake.
Kwa mujibu wa kamanda huyo, mwalimu huyo aliuawa Juni 14 mwaka huu na mwili wake uliokotwa kichakani na majeraha hayo.

Kamanda ameongezea Mwalimu huyo mara ya mwisho mwalimu huyo alionekana maeneo ya Uhuru Pub uwanja wa Maji akisubiria abiria na baada ya kumpata mteja aliondoka na kuelekea kusikojulikana.
 
serikali inalipa mishahara isiyokidhi mahitaji hadi walimu wanakuwa madereva boda boda.

angekuwa analipwa vizuri baada ya kazi angekuwa kwake amelala
 
1. Ni mwalimu
2. Ni bodaboda

Tatizo ni hiyo mishahara midogo wanayolipwa na serikali.. ona sasa wameshamkill.

RIP mwalimu
Mkuu tatizo ni mshahara mdogo au ni kutaka kujiongezea kipato? Kama ni mshahara basi wabunge wasingekuwa wanafanya biashara. Mshahara siku zote hautoshi.




R. I. P mwalimu.
 
Daaaah watu wamekosa ubinadamu siku hizi, malezi ya wazazi yamekua hovyo siku hizi, yani pikipiki isiyozidi mil.2 mtu anatoa uhai wa mtu??!!!!!!!!!!! R.I.P kwa mwalimu mjasiriamali
 
Ningekuwa na uwezo, hawa wanaopatikana na hatia ya kuua, wangekuwa wananyongwa au kupingwa risasi hadharani, so sad. Mtu anajiongezea kipato kulingana na mshahara kuwa mdogo, mtu mwingine kwa sababu za tamaa anakatisha uhai wake. Kweli inauma
 
serikali inalipa mishahara isiyokidhi mahitaji hadi walimu wanakuwa madereva boda boda.

angekuwa analipwa vizuri baada ya kazi angekuwa kwake amelala
Unaongelea huyo anayelipwa mshahara mdogo? ... je asiyekuwa na kazi je! Kuendesha daladala / bodaboda ni njia ya kujiongezea kipato. Wapo watumishi wengine wa serikali wanafuga, wanalima n.k
 
Back
Top Bottom