Mwakyembe kadhalilishwa?

Hivi jf hakuna members ambao siyo ccm au ukawa? kwa nini mtu akitoa mtazamo wake mnambatiza ufipa au lumumba? we should be fair guys, it is not right to judge someone because of his/her concepts
So r u saying u listen to liberals while there is only Republicans and democrats ....stop wasting our time sometimes
 
. Ingefaha sana kumwita Mwakyembe na kumwambia aje kutengua katazo lake mwenyewe, kuliko ile njia iliyotumika kumwadhibu.

Huwezi kuamua jambo kubwa vile na tena kuweka mpaka tarehe ya kuanza kutumika bila kushauriana na wengine. Kwani Wizara yake ndo inatoa vyeti? Kwa kuwa hakuconsult, ilistahili apigwe za uso na yeye bila kumconsult. Kastahili treament aliyopata.
 
Mwakyembe alikosea,ilitakiwa uamuzi aupitishie kwa Makonda ndio atangaze,nakuhakikishia nchi nzima ingekuwa heka heka vyeti vya kuzaliwa!
 
Nilicheka peke yangu eti huenda hata mwakyembe mwenyewe huenda hana cheti cha kuzaliwa
 
PM wanna be ni mzigo, Kaiingiza Tanesco mkenge mkubwa, Cheti cha ndoa na kuzaliwa vina uhusiano gani? Kama proof of age, mashahidi wawili wanatosha kuthibitisha umri. Ikibainika kwamba wahusika wali Makonda, waachiwe kama bashite
 
Na yeye alitamka bila kufikilia, yaani uzuie watu wasioane kisa vyeti toka RITA?
 
Tatizo la Mwakembe ni kukubaki kila kazi anayopewa hata kama anajua fika kazi ile haiwezi, sasa anayekupa kazi atakuchukuliaje.
 
Kule serikali imembwaga Mwakyembe.
Huku Mawakili wasomi wamemtupilia mbali..!
 
Kwanza Mh Magufuli kamuheshimu,Mwakyembe alikuwa ni wakutimuliwa kabisa,waziri gani ana lewa madaraka mpaka ana wapiga watu marufuku kuharisha wanapokuwa safari,kwani binadamu amekuwa fungo ambaye ana bana makalio yake na mkia mpaka akajisaidie mahali alipojiwekea kujisaidia wakati kuna sehemu zingine ambazo ana weza akajisitii na kujisaidia.
 
kama tulivyosema sisi kina gogo la shamba kwamba,miaka hii mitano itakwisha kwa kusikia mambo mengi ya ajabu hasa kutoka kwa watu tuliokuwa tunawategemea kutuletea maendeleo
 
Dr.Mwakyembe ujuzi wa sheria anao vizuri tu lakini sijui vitu gani vinampeleka nje ya ulingo,Tulianzia huko nyuma kwenye sakata la Richmond,yeye kama mwenyekiti wa tume ya Bunge,wapo watu wanasema tume yake haikumtendea Lowassa haki,hakuna ushahidi wa ufisadi bali zilikuwa ngonjera, fitina na majungu kumuondoa Lowassa.
Sasa kaja na mpya anataka kufuta TLS kana kwamba yeye ni mwanasheria "wakuja"wakati TLS ni mama mzazi wake wala si mama mlezi.
Kama haitoshi tamko lake la sharti la kufunga ndoa linazidi kumpeleka kwenye kamba huku bosi wake super heavy weight boxing champion Magu akimshindilia magumi ya upper cut,na lo leo amelamba, mchanga,kuzinduka katoto kadogo kameukwaa uraisi wa TLS Tindu Lissu.
 
Hajadhalilishwa ila tumejithibitishia kuwa "hajapona". Ni vema akarudia kuvaa soksi mkononi tu!
 
Siyo kweli kaka, kama Mwakyembe alikosea bado kiongozi mkuu kama baba na mlezi alitakiwa amwite na kumwambia akafute mwenyewe kauli yake kuliko kutumia medias kumponda na kumuhoji kama yeye ana cheti cha kuzaliwa.
Mimi niliposoma utenguzi wa amri ya mwakinyeembe, swali la kwanza lililonijia akilini ni je kama amri hii ingekuwa imetolewa na Bashite kama alivyozoea kwa wananchi wa Dar anaowaita wananchi wake, mukulu angechukua hatua kama hii?
 
Huwezi kuamua jambo kubwa vile na tena kuweka mpaka tarehe ya kuanza kutumika bila kushauriana na wengine. Kwani Wizara yake ndo inatoa vyeti? Kwa kuwa hakuconsult, ilistahili apigwe za uso na yeye bila kumconsult. Kastahili treament aliyopata.
Dawa ya moto ni___________________
 
sababu za mh raisi kupiga marufuku alichokiagiz waziri ziko wazi huitaji kuwa na PHD kuzielewa.kudhalilika ama kutodhalilika atapima mhusika.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…