WASOMI WASEMA: Dk. Mwakyembe ni mpotoshaji
MWANDISHI WETU
Mbunge wa Jimbo la Kyela kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Dk. Harrison Mwakyembe, ametajwa kuwa ni miongoni mwa watu wapotoshaji nchini huku akijificha kwa kofia ya kubobea katika taaluma ya sheria.
Hali hiyo imebainishwa na watu mbalimbali hivi karibuni kufuatia kitendo chake cha kusalimu amri na kuhojiwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupamba na Rushwa nchini (TAKUKURU) kutokana na kashfa ya kupokea posho mara mbili kwa kazi moja.
Dk. Mwakyembe pamoja na baadhi ya wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania , akiwemo Mbunge wa Kishapu, mkoani Shinyanga, Fred Mpendazoe ambaye naye awali aligoma kuhojiwa, hatimaye alikubali kuhojiwa na taasisi hiyo nyeti ya serikali.
Baadhi ya wasomi ambao waliongea na mwandishi wetu kwa masharti ya kutotajwa majina yao gazetini walisema kuwa kusalimu amri kwa Dk. Mwakyembe na mwenzake na hatimaye kuhojiwa na Takukuru kumechukuliwa na baadhi ya watu kuwa ni hatua ya kiume na kukomaa kisiasa kwa wabunge hao ambayo ilikuwa ikitarajiwa na wengi nchini.
Hata hivyo, baadhi yao wamemtaja msomi huyo wa sheria kuwa ni mpotoshaji kwani ameshindwa kuwa na msimamo katika mambo yake.
Awali alisema kuwa hawezi kuhojiwa kwa sakata la kupokea posho mara mbili kwa kazi moja kwa kuwa ana kinga ya kisheria, baadaye aliambiwa kuwa asipokubali angekamatwa na kuhojiwa kwa nguvu anabadilika na kukubali, hii ina maana gani kama si upotoshaji, alihoji mwanafunzi wa udaktari Chuo Kikuu cha Tiba cha Muhimbili, jijini Dar es Salaam.
Alisema kuwa kujua sheria haina maana kuwa hawezi kufanya uhalifu, hivyo inavyoonekana ni kuwa alikuwa akifanya makusudi kuchukua posho mara mbili huku akijua kuwa kufanya hivyo ni kosa kisheria.
Hata hivyo, daktari huyo mwanafunzi alisema kuwa kila shughuli anayofanya Dk. Mwakyembe anakuwa na lengo fulani, kwani sakata la Kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Richmond ambayo yeye alikuwa mwenyekiti wa kamati ya kuchunguza mkataba wake, anaona kama inampa kinga asisemwe.
Hata hivyo, mwalimu mmoja wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) cha jijini Dar es Salaam alisema kuwa, kukataa kuhojiwa kwa Dk. Mwakyembe kumemuondolea heshima yake mbele ya umma.
Kama kuna rushwa mahakamani na polisi, basi wanaofanya makosa wakatae kukamatwa na polisi na wakatae kuhukumiwa na majaji? alihoji msomi huyo na kuongeza kuwa huu ni upotoshaji mkubwa.
Hata hivyo, baadhi ya watu wanashangaa kwanini alikubali kuhojiwa.
Ni kweli kuwa Dk. Mwakyembe angeendelea kugoma kuhojiwa, mwisho wa siku angejikuta akivunjiwa heshima yake kwa kuhojiwa kwa nguvu na hatimaye kupelekwa mahakamani kwa kukataa amri halali ya taasisi hiyo iliyopewa meno na Bunge lenyewe, alisema mmoja wa watu waliohojiwa na mwandishi wetu.
Akaongeza: Baada ya hapo ndipo ushujaa wake ungemtokea puani kwani aibu ya kuhojiwa isingelingana na aibu ya kupelekwa mahakamani na kuhukumiwa kwa kukaidi amri ya halali ya serikali, kosa ambalo mwenyewe analitambua kisheria.
Hata hivyo, kukubali kuhojiwa kwa Dk. Mwakyembe ambaye aliapa kuwa asingehojiwa kamwe huku akidai kuwa kufanya hivyo ni kuwadhililisha wabunge, kumemwaibisha na heshima yake kuporomoka.
Heshima yake imeshuka kwa vile anafahamika na mara kwa mara amekuwa akijitangaza kuwa ni mtu wa kanuni, hivyo swali hapa ni vipi alisimamia hoja ambayo asingeweza kuiendeleza.
Wachunguzi wa mambo ya kisiasa wanasema kwamba, Dk. Mwakyembe ni mwanasheria, tena aliyebobea katika nyanja hiyo, hivyo anategemewa kuwa kila anachokisema anakuwa ameshakitafakari mara kadhaa kwa kuangalia madhara na athari zake mbele ya umma.
Aidha, wamesema kauli ya mbunge huyo kuwa hawezi kuhojiwa kwa kuwa kufanya hivyo ni kukiuka sheria bila shaka ameitoa kwenye vitabu, kwa maana hiyo inaonekana kuwa vitabu vyake vya sheria alivyovisoma vilimdanganya au alikosea kuvisoma na kumwelekeza kuwa hapaswi kuhojiwa.
Mbunge huyo wa Kyela, aliwahi kusema kuwa kuwahoji wabunge maana yake ni kukiuka sheria inayohusu kinga, madaraka na haki ya wabunge, bila shaka hoja hiyo ameijenga kupitia mtazamo wa kisheria zaidi.
Si hivyo tu, Dk. Mwakyembe alidai kuwa taratibu hazikufuatwa kwani aliitwa kutaka kuhojiwa kwa simu badala ya wito maalum wa barua.
Dk. Mwakyembe hakuishia hapo, alizidi kusema kuwa hatua hiyo ilichukuliwa kwa nia ya kufunika kashfa ya mkataba tata wa Kampuni ya kufua umeme ya Richmond .
Kimsingi ni kuwa, wito ni wito tu, uitwe kwa kukonywezwa, kuitwa kwa barua, kwa mdomo, kwa simu au kupitia barua pepe, unabaki kuwa wito, kwani kinachotazamwa hapa ni taarifa ya kukutaka ufike sehemu fulani.
Hata hivyo, hatua ya kutakiwa kuhojiwa na kashfa ya mkataba wa Kampuni ya Richmond , ni mambo mawili tofauti ambayo kimsingi yasingestahili kuwekwa pamoja kama alivyojaribu kufanya Dk. Mwakyembe.
Hatimaye, sheria imechukua mkondo wake, Dk. Mwakyembe kahojiwa, japo kwa shingo upande, lakini kuhojiwa ni kuhojiwa tu. Ingekuwa ni jambo la aibu kwa serikali kushindwa kumchukulia hatua mvunjifu wa sheria.
Hata hivyo, kitendo cha Dk. Mwakyembe kugeuka jiwe na kukubali kuhojiwa, kinaweza kuwashangaza wengi waliomuona mbunge huyo ni shujaa kutokana na hoja zake za kupinga asihojiwe huku akisema kuwa hatua hiyo ilikuwa na ajenda ya siri.
Baada ya kuhojiwa sasa Dk. Mwakyembe ameibuka kwenye gazeti moja la Kiingereza na kutangaza kuwa alikubali kuhojiwa baada ya TAKUKURU kubadilisha taratibu za mahojiano ambayo awali yalikuwa yakienda kinyume na Katiba na Sheria za nchi.
Wakati Dk. Mwakyembe anasema hivyo, Mpendazoe yeye akasema kuwa hayakuwa mahojiano, bali yalikuwa mazungumzo tu. Ni mazungumzo gani hayo na TAKUKURU?
Hayo ni mambo ya kushangaza ambayo hayapaswi kujirudia kwa wabunge wetu, kwani wanapaswa kuwa mfano wa tabia na mwenendo mzuri unaozingatia weledi na si kukurupuka na kutoa matamshi mazito na yenye utata ambayo baadaye wanakuja kuyajutia.
Hili la matamshi mazuri yenye kufurahisha watu linamkumba pia Spika wa Bunge Samwel Sitta, ambaye aliwahi kujitokeza na kuwakingia kifua wabunge kuwa kuwahoji ni kuwadhalilisha, wakati yeye ndiye aliyetaka waheshimiwa hao wahojiwe.
Hii ina maana kuwa Spika Sitta hakuwa mkweli, aliwahadaa wabunge huku akijua kuwa yeye ndiye aliwasha moto huo bungeni baada ya kutakiwa kufanya hivyo na viongozi wa serikali.
Tuhuma za wabunge kuwa wanapokea posho mara mbili kwa kazi moja zilifikishwa TAKUKURU na ofisi ya Bunge la Jamhuri ya Tanzania Aprili 26, mwaka huu.
Kufuatia hali hiyo, Waziri Mkuu Mizengo Pinda alikaririwa akisema kuwa wabunge wanapaswa kuhojiwa kwani agizo hilo linatoka katika Ofisi ya Rais na si kwingineko.
Hata hivyo, kila jambo halikosi mtibuaji, kwani suala hilo lilikuja kutibuliwa na Spika mwenyewe aliposema kuwa watu wanawaonea wivu wabunge ambapo aliwataka wajiandae kuingia katika ulingo wa siasa na kugombea ubunge mwakani.
Hata hivyo, Spika Sitta alisema kuwa wabunge wataendelea kupokea fedha hizo mara mbili kwa kuwa ni takrima.
Wabunge waliokwishahojiwa na kamati hiyo hadi sasa ni pamoja na James Lembeli (Kahama), Chrisant Mzindakaya (Kwela), Fred Mpendazoe (Kishapu), Aloyce Kimaro (Vunjo) na Anthony Diallo (Ilemela).
Hakuna sababu hata moja ya Watanzania kujichanganya kwani TAKUKURU imekusudia kutekeleza wajibu wake na hakuna aliye juu ya sheria.
Hata hivyo, sheria na kanuni za malipo ya posho zinasema mtumishi, mtu au asasi haiwezi kulipwa zaidi ya mara moja kwa ajili ya kazi hiyo hiyo.
Sasa hawa wabunge wanalipwa posho za kujikimu (subsistence allowance) na Ofisi za Bunge, lakini wakienda kwenye taasisi au mashirika ya umma au serikali za mitaa wanalipwa tena posho za kujikimu kwa shughuli hiyo hiyo ambayo Bunge imeshawalipa.
Inaelezwa kwamba, wabunge wanapotembelea asasi, taasisi na mashirika ya umma anapaswa kupewa chakula, maji ya kunywa, vinywaji baridi au baada ya kikao kufanyiwa hafla.
Mchambuzi mmoja wa masuala ya kisiasa nchini aliwahi kusema kuwa Watanzania kila tunapotaka kufanya suala la maendeleo, huwa kuna urasimu unatokea, hivyo hadi unapokamilisha taratibu zake kunakuwa hakuna maana tena.
Dk. Mwakyembe alikataa kuhojiwa na TAKUKURU kama baadhi ya wabuge wengine walivyohojiwa na taasisi hiyo kwa madai kuwa hizo ni mbinu za kutaka kuwaziba midomo wabunge.
Katika mahojiano yake na vyombo vya habari hivi karibuni Dk. Mwakyembe alikaririwa akisema kuwa, TAKUKURU inawapigia simu wabunge mmoja mmoja na kuwahoji kwa takriban zaidi ya saa tatu.
Alisema kuwa hilo ni kosa na ni kinyume cha sheria kwani mahojiano hayo hayawekwi kwenye maandishi.
CHANZO: TAIFA Tanzania, Desemba 18, 2009
Nimeinasa kwenye mtandao wa kwanzajamii.com
MWANDISHI WETU
Mbunge wa Jimbo la Kyela kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Dk. Harrison Mwakyembe, ametajwa kuwa ni miongoni mwa watu wapotoshaji nchini huku akijificha kwa kofia ya kubobea katika taaluma ya sheria.
Hali hiyo imebainishwa na watu mbalimbali hivi karibuni kufuatia kitendo chake cha kusalimu amri na kuhojiwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupamba na Rushwa nchini (TAKUKURU) kutokana na kashfa ya kupokea posho mara mbili kwa kazi moja.
Dk. Mwakyembe pamoja na baadhi ya wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania , akiwemo Mbunge wa Kishapu, mkoani Shinyanga, Fred Mpendazoe ambaye naye awali aligoma kuhojiwa, hatimaye alikubali kuhojiwa na taasisi hiyo nyeti ya serikali.
Baadhi ya wasomi ambao waliongea na mwandishi wetu kwa masharti ya kutotajwa majina yao gazetini walisema kuwa kusalimu amri kwa Dk. Mwakyembe na mwenzake na hatimaye kuhojiwa na Takukuru kumechukuliwa na baadhi ya watu kuwa ni hatua ya kiume na kukomaa kisiasa kwa wabunge hao ambayo ilikuwa ikitarajiwa na wengi nchini.
Hata hivyo, baadhi yao wamemtaja msomi huyo wa sheria kuwa ni mpotoshaji kwani ameshindwa kuwa na msimamo katika mambo yake.
Awali alisema kuwa hawezi kuhojiwa kwa sakata la kupokea posho mara mbili kwa kazi moja kwa kuwa ana kinga ya kisheria, baadaye aliambiwa kuwa asipokubali angekamatwa na kuhojiwa kwa nguvu anabadilika na kukubali, hii ina maana gani kama si upotoshaji, alihoji mwanafunzi wa udaktari Chuo Kikuu cha Tiba cha Muhimbili, jijini Dar es Salaam.
Alisema kuwa kujua sheria haina maana kuwa hawezi kufanya uhalifu, hivyo inavyoonekana ni kuwa alikuwa akifanya makusudi kuchukua posho mara mbili huku akijua kuwa kufanya hivyo ni kosa kisheria.
Hata hivyo, daktari huyo mwanafunzi alisema kuwa kila shughuli anayofanya Dk. Mwakyembe anakuwa na lengo fulani, kwani sakata la Kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Richmond ambayo yeye alikuwa mwenyekiti wa kamati ya kuchunguza mkataba wake, anaona kama inampa kinga asisemwe.
Hata hivyo, mwalimu mmoja wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) cha jijini Dar es Salaam alisema kuwa, kukataa kuhojiwa kwa Dk. Mwakyembe kumemuondolea heshima yake mbele ya umma.
Kama kuna rushwa mahakamani na polisi, basi wanaofanya makosa wakatae kukamatwa na polisi na wakatae kuhukumiwa na majaji? alihoji msomi huyo na kuongeza kuwa huu ni upotoshaji mkubwa.
Hata hivyo, baadhi ya watu wanashangaa kwanini alikubali kuhojiwa.
Ni kweli kuwa Dk. Mwakyembe angeendelea kugoma kuhojiwa, mwisho wa siku angejikuta akivunjiwa heshima yake kwa kuhojiwa kwa nguvu na hatimaye kupelekwa mahakamani kwa kukataa amri halali ya taasisi hiyo iliyopewa meno na Bunge lenyewe, alisema mmoja wa watu waliohojiwa na mwandishi wetu.
Akaongeza: Baada ya hapo ndipo ushujaa wake ungemtokea puani kwani aibu ya kuhojiwa isingelingana na aibu ya kupelekwa mahakamani na kuhukumiwa kwa kukaidi amri ya halali ya serikali, kosa ambalo mwenyewe analitambua kisheria.
Hata hivyo, kukubali kuhojiwa kwa Dk. Mwakyembe ambaye aliapa kuwa asingehojiwa kamwe huku akidai kuwa kufanya hivyo ni kuwadhililisha wabunge, kumemwaibisha na heshima yake kuporomoka.
Heshima yake imeshuka kwa vile anafahamika na mara kwa mara amekuwa akijitangaza kuwa ni mtu wa kanuni, hivyo swali hapa ni vipi alisimamia hoja ambayo asingeweza kuiendeleza.
Wachunguzi wa mambo ya kisiasa wanasema kwamba, Dk. Mwakyembe ni mwanasheria, tena aliyebobea katika nyanja hiyo, hivyo anategemewa kuwa kila anachokisema anakuwa ameshakitafakari mara kadhaa kwa kuangalia madhara na athari zake mbele ya umma.
Aidha, wamesema kauli ya mbunge huyo kuwa hawezi kuhojiwa kwa kuwa kufanya hivyo ni kukiuka sheria bila shaka ameitoa kwenye vitabu, kwa maana hiyo inaonekana kuwa vitabu vyake vya sheria alivyovisoma vilimdanganya au alikosea kuvisoma na kumwelekeza kuwa hapaswi kuhojiwa.
Mbunge huyo wa Kyela, aliwahi kusema kuwa kuwahoji wabunge maana yake ni kukiuka sheria inayohusu kinga, madaraka na haki ya wabunge, bila shaka hoja hiyo ameijenga kupitia mtazamo wa kisheria zaidi.
Si hivyo tu, Dk. Mwakyembe alidai kuwa taratibu hazikufuatwa kwani aliitwa kutaka kuhojiwa kwa simu badala ya wito maalum wa barua.
Dk. Mwakyembe hakuishia hapo, alizidi kusema kuwa hatua hiyo ilichukuliwa kwa nia ya kufunika kashfa ya mkataba tata wa Kampuni ya kufua umeme ya Richmond .
Kimsingi ni kuwa, wito ni wito tu, uitwe kwa kukonywezwa, kuitwa kwa barua, kwa mdomo, kwa simu au kupitia barua pepe, unabaki kuwa wito, kwani kinachotazamwa hapa ni taarifa ya kukutaka ufike sehemu fulani.
Hata hivyo, hatua ya kutakiwa kuhojiwa na kashfa ya mkataba wa Kampuni ya Richmond , ni mambo mawili tofauti ambayo kimsingi yasingestahili kuwekwa pamoja kama alivyojaribu kufanya Dk. Mwakyembe.
Hatimaye, sheria imechukua mkondo wake, Dk. Mwakyembe kahojiwa, japo kwa shingo upande, lakini kuhojiwa ni kuhojiwa tu. Ingekuwa ni jambo la aibu kwa serikali kushindwa kumchukulia hatua mvunjifu wa sheria.
Hata hivyo, kitendo cha Dk. Mwakyembe kugeuka jiwe na kukubali kuhojiwa, kinaweza kuwashangaza wengi waliomuona mbunge huyo ni shujaa kutokana na hoja zake za kupinga asihojiwe huku akisema kuwa hatua hiyo ilikuwa na ajenda ya siri.
Baada ya kuhojiwa sasa Dk. Mwakyembe ameibuka kwenye gazeti moja la Kiingereza na kutangaza kuwa alikubali kuhojiwa baada ya TAKUKURU kubadilisha taratibu za mahojiano ambayo awali yalikuwa yakienda kinyume na Katiba na Sheria za nchi.
Wakati Dk. Mwakyembe anasema hivyo, Mpendazoe yeye akasema kuwa hayakuwa mahojiano, bali yalikuwa mazungumzo tu. Ni mazungumzo gani hayo na TAKUKURU?
Hayo ni mambo ya kushangaza ambayo hayapaswi kujirudia kwa wabunge wetu, kwani wanapaswa kuwa mfano wa tabia na mwenendo mzuri unaozingatia weledi na si kukurupuka na kutoa matamshi mazito na yenye utata ambayo baadaye wanakuja kuyajutia.
Hili la matamshi mazuri yenye kufurahisha watu linamkumba pia Spika wa Bunge Samwel Sitta, ambaye aliwahi kujitokeza na kuwakingia kifua wabunge kuwa kuwahoji ni kuwadhalilisha, wakati yeye ndiye aliyetaka waheshimiwa hao wahojiwe.
Hii ina maana kuwa Spika Sitta hakuwa mkweli, aliwahadaa wabunge huku akijua kuwa yeye ndiye aliwasha moto huo bungeni baada ya kutakiwa kufanya hivyo na viongozi wa serikali.
Tuhuma za wabunge kuwa wanapokea posho mara mbili kwa kazi moja zilifikishwa TAKUKURU na ofisi ya Bunge la Jamhuri ya Tanzania Aprili 26, mwaka huu.
Kufuatia hali hiyo, Waziri Mkuu Mizengo Pinda alikaririwa akisema kuwa wabunge wanapaswa kuhojiwa kwani agizo hilo linatoka katika Ofisi ya Rais na si kwingineko.
Hata hivyo, kila jambo halikosi mtibuaji, kwani suala hilo lilikuja kutibuliwa na Spika mwenyewe aliposema kuwa watu wanawaonea wivu wabunge ambapo aliwataka wajiandae kuingia katika ulingo wa siasa na kugombea ubunge mwakani.
Hata hivyo, Spika Sitta alisema kuwa wabunge wataendelea kupokea fedha hizo mara mbili kwa kuwa ni takrima.
Wabunge waliokwishahojiwa na kamati hiyo hadi sasa ni pamoja na James Lembeli (Kahama), Chrisant Mzindakaya (Kwela), Fred Mpendazoe (Kishapu), Aloyce Kimaro (Vunjo) na Anthony Diallo (Ilemela).
Hakuna sababu hata moja ya Watanzania kujichanganya kwani TAKUKURU imekusudia kutekeleza wajibu wake na hakuna aliye juu ya sheria.
Hata hivyo, sheria na kanuni za malipo ya posho zinasema mtumishi, mtu au asasi haiwezi kulipwa zaidi ya mara moja kwa ajili ya kazi hiyo hiyo.
Sasa hawa wabunge wanalipwa posho za kujikimu (subsistence allowance) na Ofisi za Bunge, lakini wakienda kwenye taasisi au mashirika ya umma au serikali za mitaa wanalipwa tena posho za kujikimu kwa shughuli hiyo hiyo ambayo Bunge imeshawalipa.
Inaelezwa kwamba, wabunge wanapotembelea asasi, taasisi na mashirika ya umma anapaswa kupewa chakula, maji ya kunywa, vinywaji baridi au baada ya kikao kufanyiwa hafla.
Mchambuzi mmoja wa masuala ya kisiasa nchini aliwahi kusema kuwa Watanzania kila tunapotaka kufanya suala la maendeleo, huwa kuna urasimu unatokea, hivyo hadi unapokamilisha taratibu zake kunakuwa hakuna maana tena.
Dk. Mwakyembe alikataa kuhojiwa na TAKUKURU kama baadhi ya wabuge wengine walivyohojiwa na taasisi hiyo kwa madai kuwa hizo ni mbinu za kutaka kuwaziba midomo wabunge.
Katika mahojiano yake na vyombo vya habari hivi karibuni Dk. Mwakyembe alikaririwa akisema kuwa, TAKUKURU inawapigia simu wabunge mmoja mmoja na kuwahoji kwa takriban zaidi ya saa tatu.
Alisema kuwa hilo ni kosa na ni kinyume cha sheria kwani mahojiano hayo hayawekwi kwenye maandishi.
CHANZO: TAIFA Tanzania, Desemba 18, 2009
Nimeinasa kwenye mtandao wa kwanzajamii.com