Mwaka 2021, tokomeza uhaba wa madawati na madarasa Tanzania

Beatrice Kamugisha

JF-Expert Member
May 18, 2019
762
6,980
Taifa la Mungu elimu si Mali ya serikali Bali ni Mali yetu. Wanaosoma si watoto wa serikali bali Ni watoto na ndugu zetu. Wanaoshindwa kusoma kwa kukosa madarasa na madawati si watoto wa serikali bali ni wanetu. Serikali imepewa dhamana yakutuonyesha njia na vipaombele. Sisi tunadhamana ya kusaidia serikali ifikie malengo yaliyowekwa. Kwa mwaka 2021 tukubaliane kama Taifa kwenda na kauli mbiu "TOKOMEZA UHABA WA MADARASA NA MADAWATI TANZANIA."

Waziri wa elimu tusaidie kuyafanya haya;
1. Tuambie kwa Sasa tunahitaji madarasa mangapi ya shule za chekechea/ msingi na sekondari kwa nchi nzima ukituainishia mahitaji kwa kila shule na kata,tarafa,wilaya na mkoa kwa kila shule. List iwe in pdf ili kila mwananchi aipate kwa njia ya WhatsApp lengo nikuwaeleza wananchi huko walipotoka Kuna tatizo na wanapaswa kuwa sehemu ya kulitatua. Wapo watu hawajui kijiji chao kina tatizo gani. (Wekeni na gharama ya darasa moja shs ngapi kwa kila eneo)

2. Kwa mtiririko hapo juu tuambieni kila shule ina hitaji madawati kiasi gani na ikiwezekana price per dawati kwa kila eneo.

3. Kulingana na mchanganuo hapo juu, tuambieni serikali imejikita kufanya nn kwa mwaka 2021 ( calendar year not financial year) ili tujue sehemu iliyobaki.

4. Tuelekezeni utaratibu mzuri wa kuchangia huduma hii, ningependekeza fedha ziingizwe kwenye akaunti ya shule kulingana na mchangaji anataka kutatua tatizo la shule gani.

5. Kwa wale wanaotaka kutoa madawati yaliyokamilika waandaliwe daftari maalum ofisi na daftari hizo ziwe kwa mkuu wa shule. Hivyo hivyo kwa matofali na zitolewe risiti zakuthibisha mali hizo kupokelewa.

6. Kila Tarehe 01 ya mwezi mpya serikali itupe updates za michango kwa kila eneo.

7. Vyombo vya habari viombwe kuitangaza kampeni hii angalau kila siku bila gharama yoyote.

8. Kwa wale ambao watataka kuchangia bila kueleza wangependa msaada uende shule gani basi msaada wao utakapopokelewa eneo la kipaombele liwe ni eneo la kijijini ambapo uwezo wa kuchanga ni mdogo.

9. Projection ya Government iwe ya kutatua tatizo for ten to twenty years siyo tunafunga kampeni desemba 2021 tunaanza Tena kusikia uhaba wa madawati.

Huu ni mchango wangu wa mawazo kwa mwaka ujao, unaweza ukachukuliwa kitaifa au ukachukuliwa kiwilaya au shule mojamoja inaweza kuutumia kutatua tatizo la madarasa na madawati.

Siku zote lazima tatizo lifahamike ndipo litatuliwe. Tufahamu vijiji vyetu vinatatizo gani?
Nikiripoti kutoka Kanyigo ni Beatrice Kamugisha- mwalimu mstaafu.
 
Ni aibu kwa miaka 59 ya uhuru kuzungumzia madarasa, madawati, matundu ya vyoo, pedi za wasichana mashuleni. At the time of independence tulikuwa level moja na SK, Taiwan, Singapore, etc. Tumekwama wapi? Ardhi? Watu? Siasa safi? Uongozi bora? Au wapinzani wamekuwa wakituchelewesha?
 
Nikupe pongezi sana Mwalimu mstaafu, ulistahili kupata uteuzi. Umeweka mkakati mzuri sana ambao serikali ingewaza toka zamani kutumia wananchi kufikia malengo ya elimu ingefanikiwa.

Leo hii wapo watu wamekaa mijini lakini hawana taarifa kuhusu changamoto zilizopo vijijini walipozaliwa au kilipotoka kizazi chao.

Hii yakutengeneza taarifa ya tatizo la madawati na madarasa na kushare itatusaidia kukumbushana hasa tukiwa viti virefu tupunguze bia kidogo tukachangie madawati.

Hii itawafanya matajiri wa hapa mjini kujua tatizo la vijijini kwao na kutatua.

A good idea, naifananisha na mkakati wa kuondoa mifuko ya plastic. Ilikuwa inclusive na kila mtu akaona ni sehemu yakutokomeza mifuko ya plastic. Hatujachelewa serikali fanyeni kazi washirikisheni wananchi, wekeni taarifa na data wazi tuzichukue nakuzifanyia kazi.

Juzi Kuna tangazo lilitoka lakuwakataza vigogo kwenda likizo, Mimi sikuafiki maana tatizo Ni resources. Tunatakiwa tutafute resources.

Naamini wabunge wote Leo ukiwahita ukawaambia wakujie majimbo yao yana upungufu wa madawati mangapi na madarasa na ukataka akupe mahitaji kwa kila shule hawezi kutoa hizo data.

Tuanzie hapa kwa mwalimu mstaafu,tuboreshe mkakati huu januari moja tuanze kuinua vijiji vyetu.

Chamsingi uwepo uwazi katika zoezi hili na kila mkurugenzi awajibike kuandaa taarifa ya utekelezaji kwa eneo lake.

Tokomeza uhaba wa madarasa na madawati mashuleni.
 
Wazo zuri,kama litafanyiwa kazi ,bila shaka utakuwa umesogeza gurudum la maendeleo
 
Taifa la Mungu elimu si Mali ya serikali Bali ni Mali yetu. Wanaosoma si watoto wa serikali bali Ni watoto na ndugu zetu. Wanaoshindwa kusoma kwa kukosa madarasa na madawati si watoto wa serikali bali ni wanetu. Serikali imepewa dhamana yakutuonyesha njia na vipaombele. Sisi tunadhamana ya kusaidia serikali ifikie malengo yaliyowekwa. Kwa mwaka 2021 tukubaliane kama Taifa kwenda na kauli mbiu "TOKOMEZA UHABA WA MADARASA NA MADAWATI TANZANIA."

Waziri wa elimu tusaidie kuyafanya haya;
1. Tuambie kwa Sasa tunahitaji madarasa mangapi ya shule za chekechea/ msingi na sekondari kwa nchi nzima ukituainishia mahitaji kwa kila shule na kata,tarafa,wilaya na mkoa kwa kila shule. List iwe in pdf ili kila mwananchi aipate kwa njia ya WhatsApp lengo nikuwaeleza wananchi huko walipotoka Kuna tatizo na wanapaswa kuwa sehemu ya kulitatua. Wapo watu hawajui kijiji chao kina tatizo gani. (Wekeni na gharama ya darasa moja shs ngapi kwa kila eneo)
Serikali ina pesa ya kuwalipa wabunge 360+ milion 11 kila mwezi, 300,000 kila kikao, ikanunua ma V8 yenye thamani ya milion 400, kuanzia kwa wakurugenzi wakuu wa wilaya wakuu mikoa, mawaziri, wakati milion 400 inatosha kumaliza uhaba wa madawati kwa shule kadhaa.

Tatizo letu siyo pesa bali vipaumbele .....
Elimu bure hatuchangii
 
Wakurugenzi wa halmashauri wanafahamu upungufu uliopo kwenye halmashauri zao,Mfano wa Geita angeahirisha kununua V8 huenda angemaliza tatizo la madawati kwenye halmashauri yake.

Busara itumike na serikali kwenye kubana matumizi na kuzingatia vipaumbele itatusaidia Watanzania kuliko kurukiarukia vitu visivyo na tija kwa jamii.
 
Kwanza wewe unaisemea serikali Kama nani?Huenda serikali ikawa na pesa za kutosha.Shida siku hizi watu wanatafuta vyeo mtandaoni.
 
Acha ujinga tatizo kubwa hapo sio makalio hayo makalio ni yakupita tu Cha kudumu katika maisha ni ilimu , tatizo ni mifumo ya elimu inayozalisha graduate wasioweza kujikabili katika mazingira wanayoishi.
 
Kama viongozi waliopo wamepatikana kwa ridhaa ya waliowengi ni rahisi kushawishi wananchi kuchangia, sio hao viongozi waliongia kwa kupita kwa hila za wizi wa kura, ama kupita bila kupingwa. Na mimi kiongozi ambaye yuko madarakani kwa mbinu chafu hata anishawishi nichangie sitoi hata shilingi, na nitawashawishi watu wengine wasitoe hata elfu moja.

Katika mambo haya ya maendeleo, hapo ndio uhalali wa kiongozi kwa umma unapotakiwa. Mtaa wetu kuna kiongozi wa mtaa aliyepita kwenye ule uchaguzi wa kihuni, ameitisha vikao zaidi ya mara mbili watu wanatokea wachache sana, mpaka anaahirisha kikao, yote hayo ni madhara ya kuingia madarakani bila ridhaa ya umma.
 
Back
Top Bottom