Mwai Kibaki Rd-Kamanda Kenyela Chukua Hatua Please

Mwai Kibaki Rd-Kamanda Kenyela Chukua Hatua Please

Bobby

JF-Expert Member
Joined
Jan 10, 2008
Posts
2,182
Reaction score
1,898
Kumekuwapo na tabia inayokera sana katika barabara ya Mwai Kibaki zamani Old Bagamoyo. Watumiaji wa barabara wanaotoka Kawe kwa sababu wanazozijua wao wanahisi wao ndio wana haraka zaidi na may be ndio wenye umuhimu zaidi kuliko wale tunaoelekea Kawe. Pasipo aibu wamekuwa wakitumia lane ya wale wanaoenda Kawe na kusababisha usumbufu na pengine ajali ambazo zingeweza kuzuilika. Kadri siku zinavyoenda ndivyo tabia hii imekuwa ikiota mizizi, infact kuna maeneo mengi tu mida hii ya asubuhi ni kama vile lane ya kwenda Kawe inakuwa imekufa kwani lanes zote zinakuwa zinatumiwa na wanaoenda mjini. Kama nilivyosema nimeshuhudia ajali kadhaa ambazo zingine zimesababisha vifo kutokana na upuuzi huu.

Nimeamua kuliweka hili kwani nimeona hakuna juhudi zozote zinazochukuliwa kukomesha tabia hii mbaya ya ubinafsi isiyokuwa na tija yeyote kwani yeyote mwenye akili timamu atakubaliana na mimi kwamba mwisho wa siku hasara ya jambo hili ni kubwa kuliko faida ambayo pia si halisi. I know hiki ni kilio cha watumiaji wa barabara nyingi jijini so Kamanda Kenyela ambaye najua ni member humu na wenzako wa mikoa ya kipolisi ya Dar tafadhali tunaomba mchukue hatua haraka inavyowezekena.
 
mkuu hiyo barabara me naitumia kila siku asubuhi na jioni so kama unataka kuwa fair sema hata jioni inakuwa the opposite,yaani wanaoenda kawe ndo wanajiona wao tu ndo wana haraka!na kwa taarifa yako sio barabara hiyo tu wanaofanya hivyo coz kwa foleni za bongo dsm asbh na jioni huwa ni mtifuano kila kona hasa jamaa zetu wa daladala!
 
Kama unamanisha mpigie simu, namba yake hii hapa 0754485911,hana muda wa kuja JF na wasaidizi wake hawawezi kumwambia
 
Kama unamanisha mpigie simu, namba yake hii hapa 0754485911,hana muda wa kuja JF na wasaidizi wake hawawezi kumwambia
sioni haja ya nyie kulumbani hapa ni askari wa usalama barabarani wasimamie sheria anaevunja achukuliwe hatua
 
sioni haja ya nyie kulumbani hapa ni askari wa usalama barabarani wasimamie sheria anaevunja achukuliwe hatua

Thanks kwa kuliona hili maana nimeona sikusomeka kabisa kwani kuna mmoja kasema si Mwai Kibaki Rd peke yake kitu ambacho nimekisema pia kwenye post sikuona sababu ya kukirudia. Nia ilikuwa kueleza kwamba issue hii haiko kwenye barabara moja peke yake ndio maana nimewaomba makamanda wa mikoa mingine ya Dar wachukue hatua pia, kwangu mimi issue hapa ni zaidi ya kupiga simu kwa Kenyela kwani issue ni pana kuliko.
 
ndo visa vya kwa matajiri hivyo,
sie kwetu uswazi ni mwenye nguvu mpishe,
daladala zinaptia hata juu ya mitaro ya maji ili mradi
wawahi na uzuri wenyewe hata askari kanzu hakuna.
 
sioni haja ya nyie kulumbani hapa ni askari wa usalama barabarani wasimamie sheria anaevunja achukuliwe hatua
askari usalama barabarani wanajitahidi sana,tatizo jiji la dar karibu barabara zote ni nyembamba sana.... kama ilivyo hiyo kibaki road!
 
Back
Top Bottom