Mhache
JF-Expert Member
- Jun 20, 2008
- 345
- 24
Mvua iliyoanza kunyesha jana katika jiji la Dar es Salaam imekuwa ni ahueni kwa tulio wengi. Wengi tulikuwa tukilala nje ya nyumba zetu kutokana na joto kuwa kali na watu kuwashwa kutokana na joto kali. Watoto walikuwa wakishindwa kupata usingizi kutokana na joto kali. Pia mvua hiyo imetupa ahueni kwani tumepata maji ya kutumia hata siku mbili kama sio tatu kwa wale wenye vyombo vya kutosha. Mvua hii iwe ni ahueni kwelikweli sio watu waanze kuzibua vyoo vyao na kumwaga uchafu/takataka ovyo . Kinyume chake tutapata magonjwa ya milipuka kama kuhara na kutapika.
Vombo vya hali ya hewa sijasikia vikisema lolote kuhusiana na mvua hii. Au nyie wanajamii mmesikia chochote kuhusiana na mvua hii. Je mvua hii itaendelea kwa muda mrefu au ni ile ya kusafisha mwezi na kuingia mitini. Ninasema hivyo ili sisi watu wa mabondeni tuangalie ustaarabu au tuanze kuagiza mitumbwi?
Vombo vya hali ya hewa sijasikia vikisema lolote kuhusiana na mvua hii. Au nyie wanajamii mmesikia chochote kuhusiana na mvua hii. Je mvua hii itaendelea kwa muda mrefu au ni ile ya kusafisha mwezi na kuingia mitini. Ninasema hivyo ili sisi watu wa mabondeni tuangalie ustaarabu au tuanze kuagiza mitumbwi?