Mvua Dar balaa tupu!

Mvua Dar balaa tupu!

Sasa wakishalewa inakuaje wakati wa kukanyaga matofali ili waende nyumbani kunausalama kweli ?
...Mkuu walevi wazoefu hata ukimwambia atembee juu ya kamba anasepa vizuri kabisa...sembuse humo kwenye matofali???
 
Kweli bongo tambarare sio mabonde miundo mbinu toka baba wataifa haija rekebishwa zaidi ya kuongeza magorofa tutafika tuu!! itabidi kununua boti badala ya gari
 
Hapo sasa wenye vyoo vya shimo hasa ,maeneo ya shopers plaza ndio muda wao wa kuteki advanteji.we suburi utasikia tu.
 
Hapo ilikuwa ni jana. Je masaa 24 baadaye hali ikoje? Nimepita baadhi ya maeneo kunatisha (samahani sikuchukua picha). tena bado inaendelea imesshanyesha masaa 48 inaelekea inaweza kunyesha hata masaa 72 kwa hali ilivyo. Hali ya hewa kwa leo wametabiri mvua kubwa Dar. Sasa ndiyo tunaona madhara ya kujenga kwenye mabonde na mikondo ya maji, pamoja na kuziba njia za asili za maji kwa kisingizio kuwa "maji hukimbia watu"!!
 
Mtava ndio wapi?

Kaeneo kamoja kako barabara ya nyerere huko mbezi cha mtoto kuna Ziwa pale ukipita na gari ya chini inazima, Rav-4 zinazima gari zinazopita ni Landcruiser na madaladala makubwa tu. Aisee ni hatari.
 
Back
Top Bottom