Muziki wa dansi unarejea kwa kishindo

Muziki wa dansi unarejea kwa kishindo

sikuzamwisho

Member
Joined
Apr 12, 2019
Posts
48
Reaction score
185
Muziki wa dansi hakika Unarejea mdogo mdogo kwenye Hadhi yake kama ilivyokuwa zamani,pamoja na kupotezwa na Wadau ili muziki wa kizazi kipya ushike chati lakini ni faraja kubwa kwa Sisi wafia dansi kuona Vipindi vya dansi vimerudi maredioni na kwenye TV [emoji342] mbalimbali hakika Tunaona mwanga Jumamosi na jumapili ni sikukuu za muziki wa dansi vipindi kama vyote Tunajivunia Watangazaji na DJS ambao Wanadamu ya Muziki wa dansi na Wanajitoa kuupambania muziki huu mzuri,Wanamuziki pia hawapo nyuma kuachia ngoma kali ambazo pia Zinapatikana YouTube kama Mama wa Kambo na Nakuita wa Boggos Musica aka nyumba ya Baba chini ya Nyoshi El Sadaat aka Raisi wa milele,Yawe na mwisho wa mwezi za CP academia aka Ngwasuma full dose,Usiku wa manane wa mjengoni classic band,Samatta na Rekebisha za Twanga pepeta,2 way Traffic wa Ally Choki na Kaa la moto na Happy za Juma Kakere hakika dansi imerudi kama kawaida,Tunafurahia pia damu mpya za Kizazi kipya cha dansi kama Muu Bella wa Boggos,Kelly Hasso,Piano wa twanga na Wanamuziki wengine wanaokuja juu na kuifanya dansi ibaki kileleni,Nenda kwenye maonyesho ya Msondo Ngoma Uone Tx Moshi Junior na Rijo Voice wakiwasha moto hakika Utakubali japo bado Tunapambania viingilio kwenye maonyesho ya dansi Hatutaki KIINGILIO bia au kinywaji yaani huu muziki ni Mtamu balaa
IMG-20190827-WA0005.jpeg
IMG-20190822-WA0038.jpeg
IMG-20190711-WA0038.jpeg
IMG-20190712-WA0010.jpeg
IMG_20190716_190647_578.JPG
 
Kuna hawa jamaa wanaitwa mjengoni classic band wapo fire Sana kuna nyimbo yao inaitwa USIKU naitafuta Sana YouTube siipati Mwenye nayo tafadhar anijulishe
 
Juma kakele namkubali Sana huyu Baba
 
Nipo kambarage hapa nakula ladha za waluguru original music band
 
Kuna hawa jamaa wanaitwa mjengoni classic band wapo fire Sana kuna nyimbo yao inaitwa USIKU naitafuta Sana YouTube siipati Mwenye nayo tafadhar anijulishe
Jamaa wa mjengoni Arusha nawapata sana hao.
Kipindi kile Niko Arusha ilikuwa weekend lazima niende mjengoni au tripple A nilikuwa naenjoy sana.
 
Kwa kweli mziki wa dansi ni utabakia kuwa ndiyo mziki ninaoupenda zaidi tatizo tumetumia nguvu kubwa sana kuwaaminisha vijana wetu kuwa mziki wetu ni wa wazungu yaani yoyoyo .
 
Nimekubali sound engineer,studio, wanamuziki waimbaji na wapiga ala / vyombo wamevifanyia haki katika wimbo huu

Jimmya Golla ft Zagreb Butamu - Pardon



Source: Jimmy Tairo Tz
 
Song AFRICA ONE- Ubuntu tradition band



Source: Mahamud Rajab
 
wakowapi badi bakule,,salehe kupaza,cherles baba,muhina panduka.

Gitaa kuna jamaa alikuaga anaitwa Aldoph mbinga,mwili wake tu ulikuaga umekaaga kama solo gitaa,fundi sana yule mzee,
 
MJENGONI CLASSIC BAND MAPENZI YANAUMA OFFICIAL MUSIC VIDEO



Source: MJENGONI CLASSIC BAND
 
Salim Chimbende - Maneno Maneno (Watasema)



Source: Salim Chimbende
 
AY feat King Kiki - SAFARI (Official Audio)



Source: AyTanzania
 
Back
Top Bottom