Muziki wa dansi unakufa Tanzania

Muziki wa dansi unakufa Tanzania

Mmawia

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2013
Posts
123,242
Reaction score
98,235
Wanajamvi,inasikitisha kabisa kuona muziki wa dansi umesahaulika na kusababisha kufa kabisa. Miaka ya 1980 tulikuwa na bendi nyingi na walipiga miziki mizuri yenye ujumbe murua kwa jamii, kama vile, Juwata jazz band, sikinde, Dar international, magereza jazz band, JKT kimbunga, nk. Tunajiuliza wizara ya utamaduni nini mnafanya?
 
kweli unakufa ila unazikwa na bongo fleva na hip hop hakuna kitakacho dumu milele labda hip hop tu kabla ya dansi kulikuwa na twist twist imekufa kabla ya twist kulikuwa na aina yao ya miziki ndio hivyo hivyo ukirudi nyuma utakuta walitumia filimbi tu kabla ya ngoma.
Haya ni madhara ya teknolojia
lazima twende na teknolojia


mtamaduni hapa nasema
 
kila nabii na zama zake...nimekumbuka bendi kama vijana jazz, shikamoo jazz, bendi ya bima na nyinginezo...
 
IMG_0004.JPG



African Beat ilianzishwa mwaka 1998, baada ya Mafumu Bilali Bombenga kujiengua kutoka katika bendi ya African Stars ambayo nayo ilianzishwa mnamo mwaka 1994 kwenye Hoteli ya Bahari Beach, jijini Dar es Salaam, huku yeye akiwa ndiye muanzilishi.Bombenga anakumbuka kuwa, wakati akiwa na African Stars ambayo hata jina lake alilibuni yeye, walitamba na vibao kama ‘Sakatu Sakatu', ‘Mayanga', ‘Maya', ‘Afrika' na ‘Dance Dance'.


Baadhi ya wanamuziki waliokuwa wakiunda kundi hilo la African Stars linalojulikana zaidi hivi sasa kama ‘Twanga Pepeta', ni Bob Gady, Andy Swebe, Alfa Nyuki, Palmena Mahalu, Pamela pamoja na Kayumbu ‘Amigolas'.
"Historia yangu kimuziki, inaanzia mwaka 1972 nilipojiunga na bendi ya Morogoro Jazz, wakati huo nikitokea jeshini Makutupola," anasema Bombenga.


Mwaka 1973 aliingia na Western Jazz alioshiriki nao kupiga Saxophone, kwenye vibao kadhaa vya bendi hiyo, vikiwamo ‘Hakika', ‘Kazi ni Kazi' na ‘Sadaka', kabla ya mwaka 1978 kutimkia Dar International.
Pamoja na kupuliza kiustadi Saxophone pamoja na kuimba kwenye nyimbo kemkemu, zikiwamo ‘Mayasa' na ‘Zuena', lakini pia Bombenga alishiriki kucharaza gitaa la Solo katika kibao ‘Vick'.


Mwaka 1979 alibeba mabegi na kutua Vijana Jazz Band alikotunga kibao ‘Taabu' na pia kushiriki kukiimba, huku kadhalika akipuliza Saxophone kwenye vibao kama ‘Chiku' na ‘Matata Ndani ya Nyumba'.Mwaka 1980 alihamia Maquis ambapo alitesa kwa kupuliza Saxophone kwenye vibao viiingi, baadhi yake ni ‘Zoa', ‘Sina Ndugu', ‘Noel' pamoja na ‘Maige'."Nilikaa Maquis hadi mwaka 1984 nilipochomoka tena na kuhamia Bima Lee nilikokutana na wakali kama Jerry Nashon ‘Dudumizi', Shaaban Dede ‘Super Motisha', ‘Joseph Mulenga ‘Spoiller'," anasema Bombenga.


Mwaka 1985 Bombenga alikuwa mwanzilishi wa bendi ya MK Group ‘Ngoma za Maghorofani', kabla ya mwaka 1986 kuwa tena mmoja wa waanzilishi wa Tancut Almas ya Iringa.
Mwaka 1987 alirejea tena MK Group ambapo nyimbo yake ya kwanza kupuliza Saxophone awamu hii ya pili ilikuwa ni ‘Utakuja Kuanguka Kwenye Matope'.
Mwaka 1989, kaka yake Adam Kinguti alirudi nchini akitokea Sudan alipokuwa akifanyakazi kwenye ofisi za ubalozi, wakaanzisha Bicco Stars na yeye kushiriki kupuliza Saxophone kwenye vibao kadhaa kama vile; ‘Magret Mage', ‘Wapangaji' na Kisamvu'.


Mwaka 1991 alitoka Bicco akiwa na mpapasaji kinanda mahiri wa kike ambaye kwa sasa ni marehemu, Asia Daruweshi, baada ya kutokea hali ya kutoelewana kati yake na Kinguti, wakaanzisha Zanzibar Sound."Tukiwa na Zanzibar Sound, tulipata mkataba katika Hoteli ya Mount Meru, Arusha na mwaka mmoja baadaye mwanamuziki mwenzetu kwenye bendi hiyo, Kanku Kerry alipata mkataba Japan tukaondoka naye kwa sharti la sasa kujiita Kilimanjaro Connection," anasema Bombenga.Walizunguka nchi nyingi za bara la Asia wakiwa na Kilimanjaro Connection, waliporudi mwaka 1994 alijitoa na baadaye kidogo Asia naye alijitoa na kurudisha upya bendi yake ya Zanzibar Sound na kurejea mkataba wake Bahari Beach Hotel.


Bombenga wakati huu akabaki bila bendi, ambapo muda si muda Asia alipata kazi nchini Bahrain na kumuachia Bombenga mkataba wa Bahari Beach.Baada ya kuona ameachiwa mkataba wakati hana bendi, Bombenga ndipo alipomfuata Baraka Msirwa na kumuomba vyombo vya muziki ambapo alimpa kwavile havikuwa na kazi kutokana na kufa kwa bendi za MK Group, MK Beat na MK Sound zilizokuwa zikivitumia."Hicho ndio kilikuwa chanzo cha bendi ya African Stars niliyoibuni mwenyewe hadi jina, iliyoniletea uhasama mkubwa na dada yangu Asha Baraka baada ya kujitoa," anasema Bombenga.


Kwa upande wa warithi, Bombenga ana wanawe wawili wanaoonekana kufuata vema nyayo zake, ambao ni Feruzi (22) anayepapasa kinanda na Aziza (19) ambaye ni mwimbaji.Bombenga mwenye miaka 40 katika muziki na aliyejifunza mengi kupitia sanaa hiyo, anavutiwa na waimbaji; Isha Mashauzi, Nasseeb Abdul ‘Diamond', Flora Mbasha na Hassan Bitchuka. Anatoa ushauri kwa wanamuziki wa Dansi kuketi na vyombo vya habari na kuzungumza, ili kuangalia namna ya kuurejesha kwenye chati muziki wao ambao umekuwa ukiporomoka kila uchao.


Mikakati ya baadaye ya Bombenga ni kustaafu muziki na kujihusisha na ujasiriamali, baada ya kwenda nchini Kinshasa na kufanya maonesho na baadhi ya mastaa wa huko. "Mimi ni mtoto wa tano katika familia ya mzee Bilali Mafumu, niliyepata elimu yangu ya msingi katika shule ya H.H Agakhan, Kigoma nilikofaulu na kujiunga na shule ya sekondari Kazima, Tabora nilikosoma hadi kidato cha nne," anasema Bombenga.Baada ya kumaliza elimu ya sekondari, Bombenga aliyesoma shule moja ya sekondari na mbunge wa Tabora, Ismail Aden Rage, anasema kuwa 1972 alijiunga na JKT kwa mujibu wa sheria ya enzi hizo, alikojifunza kuimba na kupuliza Saxophone.


Anaishi Vingunguti, jijini Dar es Salaam na familia yake ambayo ni mkewe na watoto saba, huku akitamani kuongeza wake wengine hadi wawe watatu.
 
Wanajamvi,inasikitisha kabisa kuona muziki wa dansi umesahaulika na kusababisha kufa kabisa. Miaka ya 1980 tulikuwa na bendi nyingi na walipiga miziki mizuri yenye ujumbe murua kwa jamii, kama vile, Juwata jazz band, sikinde, Dar international, magereza jazz band, JKT kimbunga, nk. Tunajiuliza wizara ya utamaduni nini mnafanya?
Nimeipenda sana hii thread:

Kweli miziki ya zamani ilikuwa mizuri sana na ilikuwa na mafunzo sana, vilevile iliwajengea wanamuziki ufundi wa kupiga vyomba mbalimbali na kuwapa ubunifu wa kuteka mioyo ya mashabiki tofauti ilivyo hivi sasa.
1. Wanangu wote njooni kaeni chini niwambie maisha ya sasa ni magumu tofauti na ya zamani (Juwata Jazz)
2. Mwanameka ee, (Dar International)
3. Naomba wale wa 1980 wapitie hapa http://www.eastafricantube.com/media/9546/Bima_Lee_Orchestra_-_Mesenja_Kaleta_Balaa/

FIL14 (1).JPG
FIL15.JPG
 
Bendi umiliki wake na.uendeshaji unataka kipato cha uhakika, wakati huo unaona mashirika ndiyo yalimiliki hizo bendi pamoja na taasisi mbali mbali lakini mashirika yako wapi? ?!!!!! Taasisi nazo wapi???!!

Sidhani kama bongo fleva ndio inaua bendi ila kuwa tu vimetokea kwa wakati mmoja, sababu pia wapenzi wa bendi sio wapenzi wa bongo fleva! !!

Kaizer blaza unaitwa huku
 
Last edited by a moderator:
Nimeipenda sana hii thread:

Kweli miziki ya zamani ilikuwa mizuri sana na ilikuwa na mafunzo sana, vilevile iliwajengea wanamuziki ufundi wa kupiga vyomba mbalimbali na kuwapa ubunifu wa kuteka mioyo ya mashabiki tofauti ilivyo hivi sasa.
1. Wanangu wote njooni kaeni chini niwambie maisha ya sasa ni magumu tofauti na ya zamani (Juwata Jazz)
2. Mwanameka ee, (Dar International)
3. Naomba wale wa 1980 wapitie hapa http://www.eastafricantube.com/media/9546/Bima_Lee_Orchestra_-_Mesenja_Kaleta_Balaa/

View attachment 182688
View attachment 182690

Hicho kibao cha Maya,hats leo kikipigwa huwezi juwa kama ni zilipendwa.Inasikitisha
 
Bendi umiliki wake na.uendeshaji unataka kipato cha uhakika, wakati huo unaona mashirika ndiyo yalimiliki hizo bendi pamoja na taasisi mbali mbali lakini mashirika yako wapi? ?!!!!! Taasisi nazo wapi???!!

Sidhani kama bongo fleva ndio inaua bendi ila kuwa tu vimetokea kwa wakati mmoja, sababu pia wapenzi wa bendi sio wapenzi wa bongo fleva! !!
Kaizer blaza unaitwa huku

Kwakweli tumekosa kitu ambacho tulikipenda na hakuna jinsi ya kurudisha hizo enzi.
 
Last edited by a moderator:
Wanajamvi,inasikitisha kabisa kuona muziki wa dansi umesahaulika na kusababisha kufa kabisa. Miaka ya 1980 tulikuwa na bendi nyingi na walipiga miziki mizuri yenye ujumbe murua kwa jamii, kama vile, Juwata jazz band, sikinde, Dar international, magereza jazz band, JKT kimbunga, nk. Tunajiuliza wizara ya utamaduni nini mnafanya?

Usihofu sana; muziki wa dansi unapitia kitu kinaitwa middle age crisis; ukifuatilia kasi ya vijana hawa wa leo wanavyoshabikia Bakulutu;unaona kabisa kwamba wanaanza kujitambua na kuona tofauti ya muziki wao huu wa kileo na muziki wa dansi wa enzi hizo kwa kila kitu; maudhui, mantiki, uchezaji, staha, adabu; ujumbe nk nk; ndipo utakubali kwamba sooner rather than later muziki wa dansi utarejea jukwaani tena kwa kishindo sana.
Ni changamoto za mpito tu; historia itajirudia kama ilivyotokea 3 pc suit kutoweka na kurudi au kitu tulikuwa tunaita "Tina bull" au Tina yee! yaani zile suruali za kubana nyembamba miguuni; zikatoweka na sasa si unaona vijana ambao hawakuwepo wakati huo sasa kwao ndio mpango; the inn thing! relax bro.
 
Nimeipenda sana hii thread:

Kweli miziki ya zamani ilikuwa mizuri sana na ilikuwa na mafunzo sana, vilevile iliwajengea wanamuziki ufundi wa kupiga vyomba mbalimbali na kuwapa ubunifu wa kuteka mioyo ya mashabiki tofauti ilivyo hivi sasa.
1. Wanangu wote njooni kaeni chini niwambie maisha ya sasa ni magumu tofauti na ya zamani (Juwata Jazz)
2. Mwanameka ee, (Dar International)
3. Naomba wale wa 1980 wapitie hapa http://www.eastafricantube.com/media/9546/Bima_Lee_Orchestra_-_Mesenja_Kaleta_Balaa/

View attachment 182688
View attachment 182690

Rafiki yangu kama umechungulia moyoni mwangu kwa ufupi hivyo vibao ulivyo vitaja,we acha tu.1😛ongezi kwa wanakisomo...sikinde..kufuta ujinga mjini na vijijiniiiii ni jukumu kubwa sana kwa taifa leetu,nasi wanasikinde tunatoa pongezi kubwa kwenu kwa kuitikia kisomo cha watu wazima.
 
Kwakweli tumekosa kitu ambacho tulikipenda na hakuna jinsi ya kurudisha hizo enzi.

Utarudi mkuu sababu angalia wimbi la bongoflavians kuunda bendi linapata muitikio mzuri tu. Vionjo vitabadilika likini tutasikia bass, rhythm, solo, drums, tumba na vinginevyo!!!!
 
Bendi umiliki wake na.uendeshaji unataka kipato cha uhakika, wakati huo unaona mashirika ndiyo yalimiliki hizo bendi pamoja na taasisi mbali mbali lakini mashirika yako wapi? ?!!!!! Taasisi nazo wapi???!!

Sidhani kama bongo fleva ndio inaua bendi ila kuwa tu vimetokea kwa wakati mmoja, sababu pia wapenzi wa bendi sio wapenzi wa bongo fleva! !!

Kaizer blaza unaitwa huku


blaza acha kabisa mimi ni mpenzi wa muziki wa dansi lakini wakati umekuwa sio rafiki sana upande wa muziki huo

nakiona kifo cha muziki wa dansi kikiendana na kifo cha muziki kama muziki kwa ujumla, kwa maana ya wanamuziki wenye taaluma ya muziki.

bongo fleva nyingi hawana utaalamu wa muziki......na wala hawajihangaishi kwa vile teknologia inawaruhusu mtayarishaji kupiga vyombo vyotestudio na kisha "mwanamuziki" kuja kuingiza sauti tu

Muziki wa bendi bwana mtamu,, unaona drums zinavyopigwa, magitaa, matarumbeta, filimbi, kayamba, vinanda, nk vyote vikipigwa kwa mpangilio maalum unaovutia.

Naulilia muziki wa dansi, lakini nina hofu kwamba unazidi kupotea....kwa sababu wengi wa wanamuziki wa sasa hawajui muziki na hawataki kujifunza....
 
blaza acha kabisa mimi ni mpenzi wa muziki wa dansi lakini wakati umekuwa sio rafiki sana upande wa muziki huo

nakiona kifo cha muziki wa dansi kikiendana na kifo cha muziki kama muziki kwa ujumla, kwa maana ya wanamuziki wenye taaluma ya muziki.

bongo fleva nyingi hawana utaalamu wa muziki......na wala hawajihangaishi kwa vile teknologia inawaruhusu mtayarishaji kupiga vyombo vyotestudio na kisha "mwanamuziki" kuja kuingiza sauti tu

Muziki wa bendi bwana mtamu,, unaona drums zinavyopigwa, magitaa, matarumbeta, filimbi, kayamba, vinanda, nk vyote vikipigwa kwa mpangilio maalum unaovutia.

Naulilia muziki wa dansi, lakini nina hofu kwamba unazidi kupotea....kwa sababu wengi wa wanamuziki wa sasa hawajui muziki na hawataki kujifunza....

Hata mimi ninaumia sana kuona mziki wetu unapotea,huku wizara ambayo kimsingi ndio watu wakusimamia utamaduni wetu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom