Muundo wa Tume Huru ya Uchaguzi

Muundo wa Tume Huru ya Uchaguzi

Kuna suala la muundo na Kuna suala la kisheria na suala la utendaji. By default time ni hurry, Ila watendaji wanaweza kushindwa kutekeleza wajibu wao kwa kuingiliwa au incompetence vyote vinaweza kufanya uchaguzi usiwe huru.

Mfano walichokifanya DED 2020, sio matakwa ya time yetu (pamoja na mapungufu yake) ule ulikua utashi binafsi, kulinda cheo na hata kuingiliwa na mamlaka zingine. Hivyo uchaguzi inakosa Ile sifa tarajiwa
Sawia mkuu katika kuangalia independence ya nec ni muhimu kuangalia
Institution yenyewe
Watendaji/staff
Fund/budget

Kwa kuanzia tume iwe na watendaji wake yenyewe iachane na staff wa central n local government
 
Kama umemuamini niyeye huyohuyo anasema shithole kwa sababu tunaongozwa watu shithole
😂😂😂 so humuamini trump akisema kaibiwa kura lakini unamuamini lissu akisema kaibiwa kura!!??
Whts the difference they are all politicians!!??
 
Rejea kichwa cha habari hapo juu mara kibao tumewasikia wadau mbalimbal kutoka kada tofauti wakilalamika kuhusu utendaj kazi wa tume ya uchaguzi wengine wamefika mbali zaidi kwa kukosoa upatikanaji wa watendaji waandamizi wa tume ya uchaguzi.

Lakini wote hao sijawahi ona sehemu yoyote wakitoa mtazamo mbadala kuwa kipi kifanyike ili kupata namna ya kuweza kupata watendaji kuanzia waandamizi makao makuu ya tume mpaka wanaosimamia chaguzi za serikal za mitaa.

Kupitia bandiko hili napendekeza wanajamvi tujadiliane kistaarabu kama mara zote tunavyoamin katika demokrasia na uhuru wa kujieleza ukizingatia humu jamvini tuna wasomi wa kada tofauti naamin tutaongezeana maarifa.
Screenshot_20210414-123919.png
Screenshot_20210414-123941.png
 
Rejea kichwa cha habari hapo juu mara kibao tumewasikia wadau mbalimbal kutoka kada tofauti wakilalamika kuhusu utendaj kazi wa tume ya uchaguzi wengine wamefika mbali zaidi kwa kukosoa upatikanaji wa watendaji waandamizi wa tume ya uchaguzi.

Lakini wote hao sijawahi ona sehemu yoyote wakitoa mtazamo mbadala kuwa kipi kifanyike ili kupata namna ya kuweza kupata watendaji kuanzia waandamizi makao makuu ya tume mpaka wanaosimamia chaguzi za serikal za mitaa.

Kupitia bandiko hili napendekeza wanajamvi tujadiliane kistaarabu kama mara zote tunavyoamin katika demokrasia na uhuru wa kujieleza ukizingatia humu jamvini tuna wasomi wa kada tofauti naamin tutaongezeana maarifa.
Soma katiba kiongozi upatikanaji wa watendaji upo kwa kujibu wa katiba na Tume ipo huru katika kazi zake
Screenshot_20210414-123919.jpg
Screenshot_20210414-123941.jpg
 
Mapendekezo yangu na mimi sasa
Cheating is a bad habit, inabidi ikemewe kuanzia majumbani na shuleni.
Hii tabia inanzai majumbani mtoto anaiba hela, anaiba sukari nk
Kisha shuleni walimu wanaiba mitihani wanawapa wanafunzi shule zao zofaulishe.
Ofisini watu wanaiba stationaries na maziwa wanapeleka nyumbani.
Mahakamani karani anachomoa karatasi kwenye file la kesi.
My point is uaminifu na kutenda haki iwe tabia ya mtu binafsi kwanza kabla hatujaenda kwenye taasisi.

Pili
Muundo wa tume
Tutengeneze kamati ya uteuzi iundwe na watu wanaoheahimika na wenye sifa njema kwenye jamii, mf tunaweza kuchukua kutoka tec, kkkt, bakwata, wasabato, ngo wawakilishi.
Then kamati itangaze vacancy za mwenyekiti, makamo na mkurugenzi watu waombe (non political affiliated) wafanyiwe veting na kamati ipokee mapingamizi kutoka kwa vyama na watu binafsi.
Then kamati ipendekeze majina kwa rais kwaajili ya uteuzi then waapishwe na jaji mkuu.

Kisha kuapishwa mwenyekiti, naibu na mkurugenzi waunde secretariat watangaze nafasi za kazi ya utumishi wa tume.

Budget ya tume ipite bungeni bila marekebisho yani kama ilivyo.

Ukishakuwa mtumishi wa tume uwe disqualified kwa nafasi yeyote ile ya uteuzi.

Lets go digital katika kupiga na kuhesabu kura.

Uchaguzi wa urais utenganishwe na wabunge na madiwani. mfano tuanze na uchaguzi wa wabunge na madiwani then after a year tuchague rais (us wanatumia huu mfumo)

Matokeo yapingwe mahakamani na kuwe na registry maalum ya kesi za uchaguzi na kuwe na time frame (Kenya ni 14days for presidential petition)
Diwani, mbunge au rais asiapishwe mpka time frame ya kufungua case ipite.

Hya kazi iendelee
 
Kuwe na kamati maalum ya uteuzi, ihusishe jaji mkuu, mwenyekiti wa tume ya haki za binaadamu, tume ya utawala bora(iundwe sio sasahivi ambapo zimeunganishwa pamoja na tume ya haki za binaadamu).

Asasi za kiraia na vyama vya siasa ziruhusiwe kupeleka majina ya wanaoona wanafaa kwenye kamati ya uteuzi, na yoyote anaetaka kuwa mjumbe wa tume apeleke application kwenye kamati ya uteuzi. Baada ya hapo kamati inayapitia majina na kuwasilisha bungeni. Bungeni kuna kuwa na kamati inayohusisha wabunge toka pande zote. Upande wa serikali na upinzani. Hiyo kamati itayapitia tena hayo majina na kuwahoji. Baada ya hapo itawasilisha tena majina ya watu inayoona wanafaa kisha wanapitishwa kwa kupigiwa kura na bunge zima ili kuwa wajumbe wa tume. Rais yeye anakuja kuwaapisha tu.

Wajumbe wa tume ndo watachaguana wenyewe kati yao ili kumpata mwenyekiti na makamu mwenyekiti wa tume.

Ili kumpata mtendaji mkuu wa tume ambae ndo mkurugenzi wa uchaguzi. Watu watawasilisha maombi yao kwa tume ya uchaguzi, kisha tume itayapitia na kupeleka majina kwenye ile kamati ya bunge, nao watayapitia na kuwahoji kisha kuwasilisha jina moja litakalo pigiwa kura na bunge zima na kupitishwa. Baada ya hapo rais anakuja kumuapisha tu.

Tume iruhusiwe kuajiri watumishi wake. Ambao ndo hao hao watasimamia uchaguzi.

Mkurugenzi wa uchaguzi na watumishi wote watawajibika kwa tume na si mwingine. Mtu yoyote asiruhusiwe kuwapa maelekezo.

Wajumbe, mkurugenzi wa uchaguzi na watumishi wa tume wasiwe watu ambao waliwahi kuwa makada au viongozi wa chama chochote na pia kuwahi kuwa watumishi serikalini.

Tume pia iwe na uhuru wa kifedha. Ina wasilisha bajeti bungeni na fedha kuidhinishwa bila mjadala au kufanyiwa editing. Itakuwa ni kinyume cha sheria kwa hazina kushikilia au kuipa tume fedha pungufu kuliko ile iliyoidhinishwa na bunge.

Kumuondoa mjumbe wa tume ni mpaka jopo la kijaji liundwe, na huyo mjumbe apate nafasi ya kujitetea. Jopo la kijaji likifanya uchunguzi na kuthibitisha kuwa anafaa kuondolewa ndo huyo mjumbe aondolewe.

Mwisho kabisa watu waruhusiwe kuomba "admnisitrative review" kuhusu maamuzi ya tume. Kama mtu hajaridhishwa na maamuzi ya tume au mtumishi wake, aruhusiwe kuiomba tume ipitie tena maamuzi hayo. Na kama hajaridhika bado, aruhusiwe kufungua shauri mahakamani. Ambapo tume itabidi ifuate maamuzi ya mahakama.

Yote hayo yakifanyika. Tutakuwa na tume ambayo iko huru na ya haki.
 
Kuwe na kamati maalum ya uteuzi, ihusishe jaji mkuu, mwenyekiti wa tume ya haki za binaadamu, tume ya utawala bora(iundwe sio sasahivi ambapo zimeunganishwa pamoja na tume ya haki za binaadamu).

Asasi za kiraia na vyama vya siasa ziruhusiwe kupeleka majina ya wanaoona wanafaa kwenye kamati ya uteuzi, na yoyote anaetaka kuwa mjumbe wa tume apeleke application kwenye kamati ya uteuzi. Baada ya hapo kamati inayapitia majina na kuwasilisha bungeni. Bungeni kuna kuwa na kamati inayohusisha wabunge toka pande zote. Upande wa serikali na upinzani. Hiyo kamati itayapitia tena hayo majina na kuwahoji. Baada ya hapo itawasilisha tena majina ya watu inayoona wanafaa kisha wanapitishwa kwa kupigiwa kura na bunge zima ili kuwa wajumbe wa tume. Rais yeye anakuja kuwaapisha tu.

Wajumbe wa tume ndo watachaguana wenyewe kati yao ili kumpata mwenyekiti na makamu mwenyekiti wa tume.

Ili kumpata mtendaji mkuu wa tume ambae ndo mkurugenzi wa uchaguzi. Watu watawasilisha maombi yao kwa tume ya uchaguzi, kisha tume itayapitia na kupeleka majina kwenye ile kamati ya bunge, nao watayapitia na kuwahoji kisha kuwasilisha jina moja litakalo pigiwa kura na bunge zima na kupitishwa. Baada ya hapo rais anakuja kumuapisha tu.

Tume iruhusiwe kuajiri watumishi wake. Ambao ndo hao hao watasimamia uchaguzi.

Mkurugenzi wa uchaguzi na watumishi wote watawajibika kwa tume na si mwingine. Mtu yoyote asiruhusiwe kuwapa maelekezo.

Wajumbe, mkurugenzi wa uchaguzi na watumishi wa tume wasiwe watu ambao waliwahi kuwa makada au viongozi wa chama chochote na pia kuwahi kuwa watumishi serikalini.

Tume pia iwe na uhuru wa kifedha. Ina wasilisha bajeti bungeni na fedha kuidhinishwa bila mjadala au kufanyiwa editing. Itakuwa ni kinyume cha sheria kwa hazina kushikilia au kuipa tume fedha pungufu kuliko ile iliyoidhinishwa na bunge.

Kumuondoa mjumbe wa tume ni mpaka jopo la kijaji liundwe, na huyo mjumbe apate nafasi ya kujitetea. Jopo la kijaji likifanya uchunguzi na kuthibitisha kuwa anafaa kuondolewa ndo huyo mjumbe aondolewe.

Mwisho kabisa watu waruhusiwe kuomba "admnisitrative review" kuhusu maamuzi ya tume. Kama mtu hajaridhishwa na maamuzi ya tume au mtumishi wake, aruhusiwe kuiomba tume ipitie tena maamuzi hayo. Na kama hajaridhika bado, aruhusiwe kufungua shauri mahakamani. Ambapo tume itabidi ifuate maamuzi ya mahakama.

Yote hayo yakifanyika. Tutakuwa na tume ambayo iko huru na ya haki.
Kwa mujibu wa katiba Ibara ya 74(7), (11) inaainisha kuwa Tume na idara huru na haipokei maelekezo toka kwa kiongozi yoyote
 
Tunataka Mkurugenzi wa Tume asiteuliwe na Raisi
Position yake itangazwe na watanzania waiombe - wale wenye sifa. Kigezo muhimu asiwe kada mwandamizi wa chama chochote cha siasa au kushiriki moja kwa moja kwenye kazi cha chama chochote cha siasa.
 
Position yake itangazwe na watanzania waiombe - wale wenye sifa. Kigezo muhimu asiwe kada mwandamizi wa chama chochote cha siasa au kushiriki moja kwa moja kwenye kazi cha chama chochote cha siasa.
Nahofia isije wasiojulikana wakahodh hiyo nafas
 
Kuna suala la muundo na Kuna suala la kisheria na suala la utendaji. By default tume ni huru, Ila watendaji wanaweza kushindwa kutekeleza wajibu wao kwa kuingiliwa au incompetence vyote vinaweza kufanya uchaguzi usiwe huru.

Mfano walichokifanya DED 2020, sio matakwa ya time yetu (pamoja na mapungufu yake) ule ulikua utashi binafsi, kulinda cheo na hata kuingiliwa na mamlaka zingine. Hivyo uchaguzi inakosa Ile sifa tarajiwa
Ingawa Wajumbe wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi huteuliwa na kuapishwa na Rais lakini bado Tume ipo huru kwa mujibu wa Ibara ya 74 (11) inayosema kuwa wakati inatekeleza majukumu yake , Tume ya Uchaguzi haitalazimika kufuata amri au maagizo ya mtu yeyotea au Idara yoyote ya Serikali au maoni yoyote ya Siasa. Mbona kuna Majimbo na Kata Vyama vingine vimeshinda. Mbona Taasisi nyingine za Serikali kama Mahakama, Majaji huteuliwa na kuapishwa na Rais lakini hawaingiliwi wakati wa utendaji wao wa hukumu na kila mtu mwenye haki yake hupata mahakamani? Hongera Tume kwa kuendelee kuchapa kazi kwa kufuata Katiba ya nchi na Sheria za Uchaguzi.
 
Back
Top Bottom