Habari yenu Watanzania wenzangu,
Kila jambo na wakati wake kwa majira yake. Uchaguzi Mkuu unafanyika Oktoba, 2015 siku ya Jumapili. Si rahisi kubashiri nani ataibuka mshindi katika kinyang'anyiro cha Urais pengine tusubiri kuona nini kitatokea.
Mara baada ya tarehe 25 Oktoba tutakuwa na mjadala mpana juu ya Muundo wa Serikali ambayo Rais Mpya ataiunda. Nina mawazo ambayo ningependa Rais ajaye ayaweke katika fikra zake na kuyafanyia kazi. Nayo ni haya yafuatayo;
1. Serikali iliyopo ni kubwa mno na ufanisi ni Mdogo; hivyo afikirie kupunguza ukubwa wa Serikali kwa kiwango kikubwa.
2. Muundo wa Utawala hauna tija
Ufafanuzi
1. Ukubwa wa Serikali
Kwa sasa kwa upande wa Tanzania Bara kuna Mawaziri, Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya na wasaidizi wao. Kimsingi hawa wote kazi zao zinashabihiana. Hawa ni Wateule wa Rais na ni wawakilishi wa Taasisi ya Urais katika ngazi zao. Binafsi sioni kitu cha ziada na chenye manufaa kwa Wakuu wa Mikoa na Wilaya ambao kwa sehemu wanatumika kama Makada wa CCM. Ushauri wangu ni kuwa Cheo cha RC na DC kiondolewe tubaki na Watendaji ambao ni Makatibu Tawala na Wakurugenzi wa Halmashauri. Tutaokoa fedha nyingi sana kwa hatua hii tu.
2. Muundo wa Utawala usio na tija
Tumekuwa na Wizara nyingi lakini ufanisi bado mdogo sana. Makusanyo ya kodi na wigo wa kodi bado ni mdogo, Tija katika sekta za uzalishaji bado ipo chini nk. Ushauri wangu ni kuwa na Wizara chache lakini zenye tija. Ninapendekeza Wizara zisizozidi 15 kama ifuatavyo;
1. Wizara ya Fedha, Uchumi na Uwekezaji,
2. Wizara ya Nishati na Madini,
3. Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
4. Wizara Maji, Ardhi na Maendeleo ya Makazi
5. Wizara ya Ulinzi na JKT
6. Wizara ya Afya, Usafi wa Mazingira na Ustawi wa Jamii
7. Wizara ya Mazingira, Maliasili na Utalii
8. Wizara ya Kilimo, Mifugo, Ushirika na Masoko
9. Wizara ya Viwanda na Biashara
10.Wizara ya Katiba, Sheria na Haki za Binadamu
11.Wizara ya Michezo, Sanaa na Utamaduni
12. Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano
13. Wizara ya Elimu, Ufundi na Sayansi
14. Wizara ya Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana
15. Ofisi ya Rais-Utumishi wa Umma
Hatuna sababu ya kuwa na Wizara ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI). Halmashauri ziwajibike moja kwa moja kwa Katibu Tawala wa Mkoa (RAS). Kwa kufanya hivyo tutaokoa fedha nyingi sana na kuwa na utekelezaji wa haraka. Kwa hiyo Elimu bure kwa wote, Afya bure kwa wazee, watoto na wajawazito inawezekana kabisa.
Aidha, Rais akasimu Mamlaka yake ya uteuzi. Si busara kila uteuzi ufanywe chini ya Ofisi ya Rais. Hali hii imesababisha kujikweza na kuwa na kiburi kwa baadhi ya wateule. Mfano RC hawezi kumfanya chochote RAS kwa kuwa Mamlaka ya Uteuzi ni Rais; Wakuu wa Mashirika hawawezi kuwajibika moja kwa moja kwa Waziri husika badala yake hata wakivulunda inasubiliwa Mamlaka ya Uteuzi kutengua Uteuzi. Huu ni urasimu na ni kuchelewesha maendeleo.
Ninashauri Serikali ijayo izingatie haya. Sisi ni nchi changa lazima tuwe na namna bora zaidi ya kutumia raslimali zetu kwa matokeo makubwa.
Asanteni kwa michango yenu wana JF.
Kila jambo na wakati wake kwa majira yake. Uchaguzi Mkuu unafanyika Oktoba, 2015 siku ya Jumapili. Si rahisi kubashiri nani ataibuka mshindi katika kinyang'anyiro cha Urais pengine tusubiri kuona nini kitatokea.
Mara baada ya tarehe 25 Oktoba tutakuwa na mjadala mpana juu ya Muundo wa Serikali ambayo Rais Mpya ataiunda. Nina mawazo ambayo ningependa Rais ajaye ayaweke katika fikra zake na kuyafanyia kazi. Nayo ni haya yafuatayo;
1. Serikali iliyopo ni kubwa mno na ufanisi ni Mdogo; hivyo afikirie kupunguza ukubwa wa Serikali kwa kiwango kikubwa.
2. Muundo wa Utawala hauna tija
Ufafanuzi
1. Ukubwa wa Serikali
Kwa sasa kwa upande wa Tanzania Bara kuna Mawaziri, Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya na wasaidizi wao. Kimsingi hawa wote kazi zao zinashabihiana. Hawa ni Wateule wa Rais na ni wawakilishi wa Taasisi ya Urais katika ngazi zao. Binafsi sioni kitu cha ziada na chenye manufaa kwa Wakuu wa Mikoa na Wilaya ambao kwa sehemu wanatumika kama Makada wa CCM. Ushauri wangu ni kuwa Cheo cha RC na DC kiondolewe tubaki na Watendaji ambao ni Makatibu Tawala na Wakurugenzi wa Halmashauri. Tutaokoa fedha nyingi sana kwa hatua hii tu.
2. Muundo wa Utawala usio na tija
Tumekuwa na Wizara nyingi lakini ufanisi bado mdogo sana. Makusanyo ya kodi na wigo wa kodi bado ni mdogo, Tija katika sekta za uzalishaji bado ipo chini nk. Ushauri wangu ni kuwa na Wizara chache lakini zenye tija. Ninapendekeza Wizara zisizozidi 15 kama ifuatavyo;
1. Wizara ya Fedha, Uchumi na Uwekezaji,
2. Wizara ya Nishati na Madini,
3. Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
4. Wizara Maji, Ardhi na Maendeleo ya Makazi
5. Wizara ya Ulinzi na JKT
6. Wizara ya Afya, Usafi wa Mazingira na Ustawi wa Jamii
7. Wizara ya Mazingira, Maliasili na Utalii
8. Wizara ya Kilimo, Mifugo, Ushirika na Masoko
9. Wizara ya Viwanda na Biashara
10.Wizara ya Katiba, Sheria na Haki za Binadamu
11.Wizara ya Michezo, Sanaa na Utamaduni
12. Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano
13. Wizara ya Elimu, Ufundi na Sayansi
14. Wizara ya Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana
15. Ofisi ya Rais-Utumishi wa Umma
Hatuna sababu ya kuwa na Wizara ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI). Halmashauri ziwajibike moja kwa moja kwa Katibu Tawala wa Mkoa (RAS). Kwa kufanya hivyo tutaokoa fedha nyingi sana na kuwa na utekelezaji wa haraka. Kwa hiyo Elimu bure kwa wote, Afya bure kwa wazee, watoto na wajawazito inawezekana kabisa.
Aidha, Rais akasimu Mamlaka yake ya uteuzi. Si busara kila uteuzi ufanywe chini ya Ofisi ya Rais. Hali hii imesababisha kujikweza na kuwa na kiburi kwa baadhi ya wateule. Mfano RC hawezi kumfanya chochote RAS kwa kuwa Mamlaka ya Uteuzi ni Rais; Wakuu wa Mashirika hawawezi kuwajibika moja kwa moja kwa Waziri husika badala yake hata wakivulunda inasubiliwa Mamlaka ya Uteuzi kutengua Uteuzi. Huu ni urasimu na ni kuchelewesha maendeleo.
Ninashauri Serikali ijayo izingatie haya. Sisi ni nchi changa lazima tuwe na namna bora zaidi ya kutumia raslimali zetu kwa matokeo makubwa.
Asanteni kwa michango yenu wana JF.